Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umesoma kwa makini makala za hivi karibuni za Mnara wa Mlinzi? Ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:

Bibliomancy ni nini, na Wakristo wanapaswa kuonaje zoea hilo?

Bibliomancy ni zoea la kufungua Biblia bila kufikiri na kusoma andiko ambalo mtu analiona kwanza, akiamini kwamba maneno hayo yatampa msaada anaohitaji. Wakristo wa kweli hawatafuti ishara za bahati. Badala yake, wanajifunza Biblia ili kupata ujuzi sahihi na mwongozo wa Mungu.12/15, ukurasa wa 3.

Ni “ulimwengu” gani utakaopitilia mbali?

“Ulimwengu” utakaopitilia mbali ni wanadamu ambao hawaishi kupatana na mapenzi ya Mungu. (1 Yoh. 2:17) Dunia na wanadamu waaminifu wataokoka.—1/1, ukurasa wa 5-7.

Ijapokuwa Abeli alikufa, ni katika maana gani bado anasema nasi? (Ebr. 11:4)

Anafanya hivyo kupitia imani. Tunaweza kuiga imani yake na kujitahidi kuifuata. Mfano wake unaendelea kuishi nao ni kiwango imara tunachoweza kuiga.1/1, ukurasa wa 12.

Hatupaswi kuruhusu chochote kitutenganishe na Mungu katika sehemu gani?

Baadhi ya sehemu hizo ni: kazi yetu ya kimwili, tafrija na burudani tunazochagua, jinsi tunavyoshughulika na mshiriki wa familia aliyetengwa na ushirika, matumizi ya vifaa vya kielektroniki, kuhangaikia afya yetu, maoni yasiyofaa kuhusu pesa, na kufikiri kwamba mapendeleo au maoni yetu ni yenye thamani sana.1/15, ukurasa wa 12-21.

Tunaweza kujifunza nini kutokana na unyenyekevu wa Musa?

Musa hakujivuna alipopata mamlaka, naye alimtegemea Mungu badala ya kujitegemea mwenyewe. Hatupaswi kuruhusu uwezo, mamlaka, wala vipawa vyetu vifanye tuwe na kiburi; badala yake tunapaswa kumtegemea Yehova. (Met. 3:5, 6)2/1, ukurasa wa 5.

Wale watakaofufuliwa wataishi wapi?

Hesabu ndogo, yaani, 144,000, wataishi mbinguni. Hata hivyo, wengi watafufuliwa na kuishi duniani, wakifurahia uzima wa milele duniani.3/1, ukurasa wa 6.

Waisraeli “hawakutahiriwa moyoni” katika maana gani? (Yer. 9:26)

Walikuwa na mioyo migumu na yenye kuasi, nao walihitaji kuondolea mbali mambo yaliyofanya mioyo yao iwe migumu, yaani, mawazo, nia, au mapendezi yaliyopingana na ya Mungu. (Yer. 5:23, 24)3/15, ukurasa wa 9-10.

Yesu aliwekaje mfano katika kuwa na maisha yenye kusudi?

Alikuwa na kusudi maishani, yaani, kufanya mapenzi ya Mungu. Alimpenda sana Baba yake, na watu pia. Pia, Yesu alijua kwamba alipendwa na kukubaliwa na Baba yake. Hayo ni mambo muhimu ili kuwa na maisha yenye kusudi.4/1, ukurasa wa 4-5.

Sehemu ya kidunia ya tengenezo la Mungu inatia ndani nini?

Inatia ndani Baraza Linaloongoza, halmashauri za tawi, waangalizi wanaosafiri, mabaraza ya wazee, makutaniko, na Shahidi mmoja-mmoja.4/15, ukurasa wa 29.

Kwa nini tunaweza kusema kwamba Mungu hakuwa mkatili alipotekeleza hukumu zake?

Yehova hafurahii kifo cha mwovu. (Eze. 33:11) Matendo yake ya zamani yanaonyesha kwamba kwa upendo Mungu huwaonya watu kabla ya kutekeleza hukumu. Jambo hilo linatupa tumaini la kuokoka hukumu zake za wakati ujao.5/1, ukurasa wa 5-6.

Je, Waisraeli waliwaua wahalifu kwa kuwatundika juu ya miti?

Hapana. Mataifa mengine katika nyakati za kale yalifanya hivyo, lakini Waisraeli hawakufanya hivyo. Katika Maandiko ya Kiebrania, watenda maovu waliuawa kwanza, labda kwa kupigwa kwa mawe. (Law. 20:2, 27) Kisha, huenda maiti hiyo ilitundikwa juu ya mti ili kuwa onyo kwa wengine.5/15, ukurasa wa 13.

Kwa nini wanadamu wameshindwa kuleta amani duniani?

Ingawa wanadamu wametimiza mambo mengi, hawana uwezo wa kuongoza hatua zao wenyewe. (Yer. 10:23) Kwa kuwa Shetani anatawala ulimwengu, wanadamu hawataweza kuleta amani. (1 Yoh. 5:19)6/1, ukurasa wa 16.