Yeremia 5:1-31

  • Watu wakataa nidhamu ya Yehova (1-13)

  • Wataharibiwa lakini hawataangamizwa kabisa (14-19)

  • Yehova awaadhibu watu (20-31)

5  Tembeeni huku na huku katika barabara za Yerusalemu. Tazameni pande zote mwone. Tafuteni katika viwanja vyake vya jijiIkiwa mnaweza kumpata mtu anayetenda haki,+Yeyote anayejitahidi kuwa mwaminifu,Nami nitalisamehe jiji hilo.   Hata wakisema: “Kwa hakika kama Yehova anavyoishi!” Bado wataapa kwa uwongo.+   Ee Yehova, je, macho yako hayatafuti uaminifu?+ Uliwapiga, lakini hawakusikia.* Uliwaangamiza, lakini walikataa kukubali nidhamu.+ Walizifanya nyuso zao kuwa ngumu kuliko mwamba,+Nao wakakataa kugeuka.+   Lakini nilisema moyoni: “Kwa hakika hawa ni watu wa hali ya chini. Wanatenda kwa upumbavu, kwa sababu hawaijui njia ya Yehova,Hukumu ya Mungu wao.   Nitaenda kwa watu mashuhuri na kuzungumza nao,Kwa maana lazima wameijua njia ya Yehova,Hukumu ya Mungu wao.+ Lakini wote walikuwa wameivunja niraNa kuvikata vizuizi.”*   Ndiyo sababu simba kutoka msituni anawashambulia,Mbwamwitu wa majangwa tambarare anaendelea kuwararua,Chui anakaa macho kwenye majiji yao. Kila mtu anayetoka humo anararuliwa vipandevipande. Kwa maana makosa yao ni mengi;Matendo yao ya ukosefu wa uaminifu ni mengi sana.+   Ninawezaje kukusamehe kwa jambo hili? Wana wako wameniacha,Nao wanaapa kwa kitu ambacho si Mungu.+ Nilitosheleza mahitaji yao,Lakini waliendelea kufanya uzinzi,Na kukusanyika katika nyumba ya kahaba.   Wao ni kama farasi wenye tamaa na uchu,Kila mmoja anamlilia mke wa mwenzake.+   “Je, sipaswi kuwafanya wawajibike kwa sababu ya mambo haya?” asema Yehova. “Je, sipaswi* kujilipizia kisasi dhidi ya taifa kama hili?”+ 10  “Pandeni mshambulie matuta yake ya mizabibu na kuyaharibu,Lakini msiyaharibu kabisa.+ Ondoeni machipukizi yake yanayoenea,Kwa maana si ya Yehova. 11  Kwa sababu watu wa nyumba ya Israeli na watu wa nyumba ya YudaWamenitendea kwa hila kabisa,” asema Yehova.+ 12  “Wamemkana Yehova, nao wanaendelea kusema,‘Hatafanya chochote.*+ Hatutapatwa na msiba wowote;Hatutaona upanga wala njaa kali.’+ 13  Manabii wamejaa upepo,Na neno* halimo ndani yao. Na iwe hivyo kwao!” 14  Kwa hiyo, Yehova, Mungu wa majeshi, anasema hivi: “Kwa sababu watu hawa wanasema jambo hilo,Ninayafanya maneno yangu kuwa moto kinywani mwako,+Na watu hawa ndio kuni,Nao utawateketeza.”+ 15  “Tazameni, ninaleta dhidi yenu taifa kutoka mbali, Enyi watu wa nyumba ya Israeli,”+ asema Yehova. “Ni taifa linalodumu. Ni taifa la zamani za kale,Taifa ambalo lugha yake hamwijui,Na hamwezi kuelewa wanachosema.+ 16  Podo lao ni kama kaburi lililo wazi;Wote ni mashujaa. 17  Watakula mavuno yenu na mkate wenu.+ Watawala wana wenu na mabinti wenu. Watayala makundi yenu na mifugo yenu. Wataila mizabibu yenu na mitini yenu. Watayaangamiza kwa upanga majiji yenu yenye ngome mnayoyatumaini.” 18  “Lakini hata katika siku hizo,” asema Yehova, “sitawaangamiza kabisa.+ 19  Na wakiuliza, ‘Kwa nini Yehova Mungu wetu ametutendea mambo haya yote?’ mtawajibu, ‘Kama mlivyoniacha ili kumtumikia mungu wa kigeni katika nchi yenu, ndivyo mtakavyowatumikia wageni katika nchi isiyo yenu.’”+ 20  Tangazeni jambo hili katika nyumba ya Yakobo,Na kulitangaza Yuda, mkisema: 21  “Sikieni jambo hili, ninyi watu wajinga na wasio na akili:*+ Wana macho lakini hawawezi kuona;+Wana masikio lakini hawawezi kusikia.+ 22  ‘Je, hamniogopi mimi?’ asema Yehova,‘Je, hampaswi kutetemeka mbele zangu? Mimi ndiye niliyeweka mchanga kuwa mpaka wa bahari,Sheria inayodumu isiyoweza kukiukwa na bahari. Ingawa mawimbi yake yanasukasuka, hayawezi kushinda;Ingawa yananguruma, bado hayawezi kuvuka.+ 23  Lakini watu hawa wana moyo mgumu unaoasi;Wamegeuka kando na kuifuata njia yao wenyewe.+ 24  Nao hawasemi moyoni mwao: “Sasa na tumwogope Yehova Mungu wetu,Yule anayeleta mvua katika majira yake,Mvua ya vuli na mvua ya masika,Yule anayetulindia majuma yaliyowekwa ya mavuno.”+ 25  Makosa yenu wenyewe yalizuia mambo haya yasije;Dhambi zenu wenyewe zimewanyima mambo mema.+ 26  Kwa maana kati ya watu wangu kuna watu waovu. Wanaendelea kuchungulia, kama wawindaji wa ndege wanapochutama. Wanatega mtego hatari. Wanawanasa watu. 27  Kama kizimba kilichojaa ndege,Ndivyo nyumba zao zilivyojaa udanganyifu.+ Ndiyo sababu wamekuwa wenye nguvu na matajiri. 28  Wamenenepa na kuwa laini;Wanafurika uovu. Hawawatetei mayatima katika kesi,+Wanatafuta mafanikio yao wenyewe;Nao wanawanyima haki maskini.’”+ 29  “Je, sipaswi kuwafanya wawajibike kwa sababu ya mambo haya,” asema Yehova. “Je, sipaswi* kujilipizia kisasi dhidi ya taifa kama hili? 30  Jambo la kutisha na kuchukiza limetokea nchini: 31  Manabii wanatabiri uwongo,+Nao makuhani wanakandamiza kwa mamlaka yao wenyewe. Na watu wangu wanapenda mambo yawe hivyo.+ Lakini mtafanya nini mwisho ukifika?”

Maelezo ya Chini

Tnn., “hawakudhoofika.”
Tnn., “vifungo.”
Au “nafsi yangu haipaswi.”
Au labda, “Hayuko.”
Yaani, neno la Mungu.
Tnn., “ninyi watu wajinga msio na moyo.”
Au “nafsi yangu haipaswi.”