Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Upendezwe Sana na Zawadi Yako ya Uhuru wa Kuchagua

Upendezwe Sana na Zawadi Yako ya Uhuru wa Kuchagua

“Mahali palipo na roho ya Yehova, pana uhuru.” 2 WAKORINTHO 3:17.

NYIMBO: 62, 65

1, 2. (a) Watu wako na mawazo gani mbalimbali juu ya uhuru wa kuchagua? (b) Biblia inatufundisha nini juu ya uhuru wetu wa kuchagua, na tutachunguza maulizo gani?

WAKATI alipenda kukamata uamuzi fulani, mwanamuke mumoja aliambia rafiki yake hivi: “Usinifanye nifikiri, uniambe tu jambo la kufanya. Hilo litakuwa mwepesi sana.” Mwanamuke huyo alipenda wengine wamuambie jambo la kufanya kuliko kutumikisha uhuru wake wa kuchagua, zawadi ya maana sana yenye Muumbaji wake alimupatia. Halafu wewe? Unapenda kukamata maamuzi yako mwenyewe, ao unapenda wengine wakamate maamuzi pa nafasi yako? Uko na mawazo gani juu ya uhuru wa kuchagua?

2 Watu wako na mawazo mbalimbali juu ya uhuru wa kuchagua. Wamoja wanasema kama hatuna kabisa uhuru wa kuchagua kwa sababu Mungu amekwisha kupanga mambo yote yenye tunafanya. Wengine wanasema kama tunaweza kuwa na uhuru wa kuchagua ikiwa tu tuko na uhuru wenye hauna mipaka. Lakini, Biblia inatufundisha kama wakati Mungu alituumba alitupatia uwezo na uhuru wa kukamata maamuzi yenye hekima. (Soma Yoshua 24:15.) Pia, Biblia inatoa majibu kwa maulizo haya: Uhuru wetu wa kuchagua uko na mipaka? Namna gani tunapaswa kutumikisha uhuru wetu wa kuchagua ili kukamata maamuzi? Namna gani maamuzi yetu yanaonyesha kama tunamupenda kabisa Yehova? Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia maamuzi ya wengine?

MUFANO WA YEHOVA NA YESU UNAWEZA KUTUFUNDISHA NINI?

3. Namna gani Yehova anatumia uhuru wake wenye hauna mipaka?

3 Yehova ana uhuru wenye hauna mipaka, na namna anatumia uhuru wake inaweza kutufundisha mambo fulani. Kwa mufano, Yehova alichagua taifa la Israeli ili likuwe watu wake, ni kusema, “mali [yake] ya pekee.” (Kumbukumbu la Torati 7:6-8) Alikuwa na sababu ya kukamata uamuzi huo. Yehova alipenda kutimiza ahadi yenye alimupatia rafiki yake Abrahamu. (Mwanzo 22:15-18) Zaidi ya hilo, Yehova anatumia sikuzote uhuru wake kwa upendo na haki. Tunaweza kuona jambo hilo kupitia namna aliwapatia Waisraeli nizamu wakati walikosa kumutii. Wakati walihuzunika kabisa juu ya mambo yenye walikuwa wamefanya, Yehova aliwaonyesha upendo na rehema. Alisema hivi: “Nitaponya ukosefu wao wa uaminifu. Nitawapenda kwa kupenda kwangu mwenyewe.” (Hosea 14:4) Yehova alituonyesha mufano muzuri kwa kutumikisha uhuru wake ili kusaidia wengine!

4, 5. (a) Ni nani alikuwa mutu wa kwanza mwenye Mungu alipatia zawadi ya uhuru wa kuchagua, na aliitumikisha namna gani? (b) Kila mumoja wetu anapaswa kujiuliza ulizo gani?

4 Wakati Yehova aliumba malaika na wanadamu, aliamua kuwapatia uhuru wa kuchagua. Yesu ndiye alikuwa kiumbe wa kwanza wa Yehova. Aliumbwa kwa mufano wa Mungu na alikuwa na uhuru wa kuchagua. (Wakolosai 1:15) Namna gani Yesu alitumia uhuru wake? Mbele akuje katika dunia, Yesu alichagua kubakia mushikamanifu kwa Mungu na hakuunga Shetani mukono na uasi wake. Wakati Yesu alikuja katika dunia, aliamua kukataa majaribu ya Shetani. (Mathayo 4:10) Kisha, usiku wenye ulitangulia kifo chake, Yesu alihakikishia Baba yake kama alipenda kufanya mapenzi Yake. Alisema hivi: “Baba, ikiwa unataka, niondolee kikombe hiki. Hata hivyo, acha, si mapenzi yangu, bali yako yatendeke.” (Luka 22:42) Je, tunaweza kabisa kumuiga Yesu na kutumikisha uhuru wetu wa kuchagua ili kumuletea Yehova utukufu na kufanya mapenzi yake?

5 Ndiyo, tunaweza kuiga mufano wa Yesu kwa sababu sisi pia tuliumbwa kwa mufano wa Mungu. (Mwanzo 1:26) Lakini tofauti na Yehova, sisi hatuna uhuru wenye hauna mipaka. Neno la Mungu linaeleza kama Yehova amewekea uhuru wetu mipaka na anapenda tuheshimie mipaka hiyo. Kwa mufano, katika familia, bibi wanapaswa kujitiisha kwa bwana zao, na watoto wanapswa kutii wazazi wao. (Waefeso 5:22; 6:1) Mipaka hiyo iko na matokeo gani juu ya namna tunatumikisha uhuru wetu wa kuchagua? Jibu la ulizo hilo linaweza kuwa na matokeo juu ya uzima wetu wa milele wa wakati unaokuja.

KUTUMIKISHA MUZURI NA KUTUMIKISHA MUBAYA UHURU WA KUCHAGUA

6. Sababu gani ni jambo la maana uhuru wetu ukuwe na mipaka? Toa mufano.

6 Uhuru wenye kuwa na mipaka unaweza kabisa kuwa uhuru wa kweli? Ndiyo! Sababu gani? Kwa sababu mipaka inaweza kutulinda. Kwa mufano, tunaweza kuamua kutumia motokari ili kuenda katika muji fulani wenye kuwa mbali sana. Lakini fikiria kuwa hakuna sheria za barabara, na kila mutu anaweza kuamua kukimbiza motokari yake namna anapenda na kuamua kutembezea ngambo ya barabara yenye anapenda. Utajisikia salama kusafiri katika barabara hiyo? Hapana kabisa. Mipaka ni ya lazima ili watu wote wapate faida za uhuru wa kweli. Tuzungumuzie basi mifano fulani ya Biblia yenye kuonyesha namna mipaka yenye Yehova ameweka inaweza kutuletea faida.

7. (a) Kulikuwa tofauti gani moja kati ya Adamu na wanyama? (b) Eleza njia moja yenye Adamu alitumikisha uhuru wake wa kuchagua.

7 Wakati Yehova aliumba mutu wa kwanza, Adamu, alimupatia zawadi ileile yenye alikuwa amepatia malaika, ni kusema, uhuru wa kuchagua. Lakini Mungu hakupatia wanyama uhuru wa kuchagua. Namna gani Adamu alitumikisha muzuri uhuru wake wa kuchagua? Adamu alifurahia kazi ya kupatia wanyama majina. Mungu ‘akaanza kumuletea huyo mutu ili aone atawaitaje kila mumoja wao.’ Kisha kuangalia kila munyama kwa uangalifu, Adamu alimupatia jina lenye kuwa na maana. Yehova hakubadilisha jina la munyama yeyote mwenye Adamu alikuwa amepatia jina. Lakini, ‘jina ambalo huyo mutu aliita kila nafsi hai [kiumbe chenye kuwa na uzima], kila mumoja, hilo likakuwa jina lake.’—Mwanzo 2:19.

8. Namna gani Adamu alitumikisha mubaya uhuru wake wa kuchagua, na hilo lilikuwa na matokeo gani?

8 Yehova alimupatia Adamu daraka la kufanya dunia ikuwe paradiso. Alimuambia hivi: ‘Muzae, mukuwe wengi, mujaze dunia na kuitiisha, na mutawale samaki wa baharini na viumbe vinavyoruka vya mbinguni na kila kiumbe hai kinachotambaa juu ya dunia.’ (Mwanzo 1:28) Lakini Adamu aliamua kukula tunda lenye Mungu alimukataza, na wakati alifanya hivyo, hakuheshimia mipaka yenye Yehova aliweka. Kwa sababu Adamu alitumikisha mubaya uhuru wake wa kuchagua, wanadamu wameteseka kwa maelfu ya miaka. (Waroma 5:12) Tukumbuke matokeo ya mubaya sana yenye uamuzi wa Adamu umeleta. Hilo litatuchochea tutumikishe muzuri uhuru wetu wa kuchagua na kuheshimia mipaka yenye Yehova ametuwekea.

9. Yehova alipatia watu wake Israeli nafasi ya kukamata uamuzi gani, na waliahidi kufanya nini?

9 Wanadamu wote wameriti kutokamilika na kifo kutoka kwa Adamu na Eva. Hata hivyo, tungali na haki ya kutumikisha zawadi ya uhuru wa kuchagua. Tunaweza kuona jambo hilo kupitia namna Yehova alitendea taifa la Israeli. Yehova aliwapatia nafasi ya kuchagua kuwa mali yake ya pekee ao hapana. (Kutoka 19:3-6) Taifa hilo lilichagua kuwa watu wa Mungu na kuheshimia mipaka yenye Mungu aliweka. Walisema hivi: “Yote ambayo Yehova amesema tuko tayari kuyafanya.” (Kutoka 19:8) Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, kisha wakati fulani Waisraeli waliamua kuvunja ahadi yao kwa Yehova. Mufano huo unaweza kutufundisha mambo ya maana. Tupendezwe sikuzote na zawadi yetu ya uhuru wa kuchagua na tuendelee kushikamana sana na Yehova na kutii sheria zake.​—1 Wakorintho 10:11.

10. Ni mifano gani yenye kupatikana katika sura ya 11 ya kitabu cha Waebrania yenye kuonyesha kama wanadamu wenye hawakamilike wanaweza kutumikisha uhuru wao wa kuchagua ili kumuletea Mungu utukufu? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

10 Sura ya 11 ya kitabu cha Waebrania, inazungumuzia wanaume na wanawake waaminifu 16 wenye walichagua kuheshimia mipaka yenye Yehova aliweka. Kwa hiyo, walipata baraka nyingi na tumaini la ajabu kwa ajili ya wakati unaokuja. Kwa mufano, Noa alikuwa na imani kubwa na alichagua kutii maagizo ya Mungu ya kujenga safina ili kuokoa familia yake na vizazi vya wakati unaokuja. (Waebrania 11:7) Abrahamu na Sara walikuwa tayari kumutii Mungu na kuenda katika inchi yenye aliahidi kuwapatia. Hata kama walikuwa na “nafasi ya kurudi” katika muji wa Uru, walikaza akili yao juu ya ahadi za Mungu za wakati unaokuja. Biblia inasema kama walikuwa “wanajitahidi [wanajikaza] kufikia mahali palipo bora.” (Waebrania 11:8, 13, 15, 16) Musa alikataa utajiri wa inchi ya Misri na kuchagua ‘kutendewa vibaya pamoja na watu wa Mungu badala ya kufurahia zambi kwa muda.’ (Waebrania 11:24-26) Tuige basi wanaume na wanawake hao waaminifu na tupendezwe na zawadi yetu ya uhuru wa kuchagua, kwa kuitumikisha ili kufanya mapenzi ya Mungu.

11. (a) Uhuru wa kuchagua unatutolea baraka gani kubwa zaidi? (b) Ni nini inakuchochea kutumikisha muzuri uhuru wako wa kuchagua?

11 Inaweza kuwa vyepesi kuomba mutu mwengine akamate uamuzi pa nafasi yetu, lakini hatutapata hata kidogo baraka moja kati ya baraka kubwa zaidi za uhuru wa kuchagua. Ni baraka gani hiyo? Biblia inatoa maelezo kwenye Kumbukumbu la Torati 30:19, 20. (Soma.) Katika mustari wa 19, tunasoma kama Mungu alipatia Waisraeli nafasi ya kuchagua. Katika mustari wa 20, tunajifunza kama Yehova aliwapatia nafasi ya kuonyesha ikiwa wanamupenda sana. Sisi pia tunaweza kuchagua kumuabudu Yehova. Na pia tuko na nafasi ya pekee ya kutumikisha zawadi yetu ya uhuru wa kuchagua ili kumutukuza Yehova na kuonyesha kama tunamupenda sana!

USITUMIKISHE MUBAYA UHURU WAKO WA KUCHAGUA

12. Ni katika njia gani hatuwezi hata kidogo kutumikisha uhuru wetu wa kuchagua?

12 Fikiria kwamba unapatia rafiki yako zawadi fulani ya maana sana. Utajisikia namna gani ikiwa anatupa zawadi yako mahali pa kutupa uchafu ao, hata mubaya zaidi, anatumikisha zawadi hiyo ili kutendea mutu mwingine mubaya? Utahuzunika. Yehova ametupatia zawadi ya uhuru wa kuchagua. Kwa hiyo, anapaswa kuhuzunika wakati anaona watu wanatumikisha mubaya uhuru wao na kukamata maamuzi ya mubaya, ao wakati wanatendea wengine mubaya. Biblia ilisema kama katika “siku za mwisho,” watu watakuwa “wasio na shukrani.” (2 Timotheo 3:1, 2) Kwa hiyo, namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya zawadi ya maana sana yenye Yehova ametupatia? Na namna gani tunaweza kuepuka kuitumikisha mubaya?

13. Ni katika njia gani moja tunapaswa kuepuka kutumikisha mubaya uhuru wetu wa Kikristo?

13 Sisi wote tuko na uhuru wa kuchagua marafiki, manguo na namna yetu ya kujipamba, na mambo ya kujifurahisha. Lakini, tunaweza kutumikisha uhuru wetu kuwa sababu ya kukamata maamuzi yenye Mungu hapendi ao ili kuiga tabia za watu wa ulimwengu. (Soma 1 Petro 2:16.) Kuliko kutumikisha uhuru wetu kuwa nafasi ya kufanya mambo ya mubaya, tunapaswa kuutumikisha kuwa nafasi ya ‘kufanya mambo yote kwa utukufu wa Mungu.’—1 Wakorintho 10:31; Wagalatia 5:13.

14. Sababu gani tunapaswa kumutegemea Yehova wakati tunatumikisha uhuru wetu wa kuchagua?

14 Yehova alisema hivi: “Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, Yeye anayekufanya uende katika njia unayopaswa kutembea ndani yake.” (Isaya 48:17) Ili tukamate maamuzi ya muzuri, tunapaswa kumutegemea Yehova na kuheshimia mipaka yenye ameweka. Tunakubali kwa unyenyekevu kama ‘njia ya mutu wa udongo haimo katika uwezo wake. Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.’ (Yeremia 10:23) Adamu na Waisraeli wenye kukosa uaminifu waliamua kuvunja mipaka yenye Yehova aliweka na walijitegemea wao wenyewe. Mufano wao wa mubaya unaweza kutufundisha jambo fulani. Kuliko kujitegemea sisi wenyewe, tunapaswa ‘kumutegemea Yehova kwa moyo [wetu] wote.’—Methali 3:5.

TUHESHIMIE UHURU WA KUCHAGUA WA WENGINE

15. Kanuni yenye kupatikana kwenye Wagalatia 6:5 inatufundisha nini?

15 Tunapaswa pia kuheshimia uhuru wa wengine wa kukamata maamuzi yao katika maisha. Sababu gani? Kwa sababu sisi wote tuko na zawadi ya uhuru wa kuchagua, Wakristo wawili hawatakamata sikuzote maamuzi yenye kufanana kabisa. Kati ya maamuzi hayo, kuko maamuzi yenye kuhusu mwenendo na ibada yetu. Ukumbuke kanuni yenye kupatikana kwenye Wagalatia 6:5. (Soma.) Ikiwa tunakumbuka kama kila Mukristo ana daraka la kukamata maamuzi yake mwenyewe, tutaheshimia uhuru wa wengine wa kutumikisha uhuru wao wa kuchagua.

Tunaweza kukamata maamuzi yetu bila kukaza wengine wakamate maamuzi yaleyale (Picha hii inapatana na fungu la 15)

16, 17. (a) Namna gani uhuru wa kuchagua ulileta tatizo katika kutaniko la Korintho? (b) Namna gani mutume Paulo alisaidia Wakristo hao, na hilo linatufundisha nini?

16 Tuzungumuzie basi mufano mumoja wa Biblia wenye kuonyesha sababu gani tunapaswa kuheshimia uhuru wa kuchagua wa ndugu na dada zetu. Wakristo wa kutaniko la Korintho walibishana juu ya kula nyama pengine yenye ilikuwa imetolewa kwa sanamu, na kisha iliuzishwa katika soko. Zamiri ya Wakristo fulani iliwaruhusu kula nyama hiyo kwa sababu walijua kama sanamu haikukuwa kitu. Lakini, wengine wenye walizoea kuabudu sanamu kama hizo zamani waliona kuwa kula nyama hiyo, ilikuwa kama vile kuabudu sanamu. (1 Wakorintho 8:4, 7) Hilo lilikuwa tatizo kubwa lenye lingeleta mugawanyiko katika kutaniko. Namna gani mutume Paulo alisaidia Wakristo kumaliza tatizo hilo kubwa?

17 Kwanza, mutume Paulo alikumbusha vikundi hivyo viwili kama chakula hakingeweza kutia nguvu urafiki wao pamoja na Mungu. (1 Wakorintho 8:8) Tena, mutume Paulo aliwaonya kuwa wasiache uhuru wao wa kuchagua ukwaze zamiri za wale wenye walikuwa wazaifu. (1 Wakorintho 8:9) Kisha, aliambia wale wenye walikuwa na zamiri yenye kukwazika haraka kama wasihukumu wale wenye waliamua kula nyama kama hiyo. (1 Wakorintho 10:25, 29, 30) Kwa hiyo, katika hali za maana zenye zilihusu ibada, kila Mukristo alipaswa kukamata maamuzi yake mwenyewe. Sisi pia, tunapaswa kuheshimia uhuru wa ndugu na dada wa kukamata maamuzi yao hata katika mambo madogo-madogo.—1 Wakorintho 10:32, 33.

18. Namna gani utaonyesha kama unapendezwa sana na zawadi yako ya uhuru wa kuchagua?

18 Yehova ametupatia zawadi ya uhuru wa kuchagua, na zawadi hiyo inatutolea uhuru wa kweli. (2 Wakorintho 3:17) Tunapendezwa sana na zawadi hiyo kwa sababu inaturuhusu kukamata maamuzi yenye kuonyesha kama tunamupenda sana Yehova. Kwa hiyo, tuendelee basi kukamata maamuzi yenye kumutukuza, na tuendelee kuheshimia haki ya wengine ya kuamua namna ya kutumikisha zawadi hiyo ya maana sana.