Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA 8

Vyombo kwa Ajili ya Kazi ya Kuhubiri—Vichapo kwa Ajili ya Kazi ya Kuhubiri Duniani Pote

Vyombo kwa Ajili ya Kazi ya Kuhubiri—Vichapo kwa Ajili ya Kazi ya Kuhubiri Duniani Pote

WAZO KUBWA KATIKA SURA HII

Yehova anaendelea kututolea vyombo ambavyo tunahitaji ili kufundisha watu wa kila taifa, kabila, na luga

1, 2. (a) Wakati wa mitume, ni nini ilifanya habari njema ienee katika utawala wote wa Roma? (b) Tuna ushuhuda gani kwamba Yehova anategemeza watumishi wake leo? (Soma pia kisanduku “ Habari Njema Katika Luga Zaidi ya 670.”)

WATU ambao wanatembelea Yerusalemu wanashangaa sana, kwa sababu Wagalilaya wanazungumuza luga za kigeni bila magumu, na ujumbe ambao wanatangaza unawapendeza wasikilizaji wao. Jambo hilo lilifanyika wakati wa Pentekoste mwaka wa 33, wakati wanafunzi wa Yesu walipokea zawadi ya kuzungumuza luga mbalimbali kimuujiza. Huo ulikuwa ushuhuda kwamba Mungu alikuwa anawategemeza. (Soma Matendo 2:1-8, 12, 15-17.) Habari njema ambayo walihubiri siku hiyo, iliwafikia watu wa maeneo tofauti na ilienea katika Utawala wote wa Roma.​—Kol. 1:23.

2 Leo, watumishi wa Mungu hawazungumuze luga mbalimbali kimuujiza. Hata hivyo, ili kuhubiri katika luga nyingi kuliko wakati wa mitume, wanatafsiri ujumbe wa Ufalme katika luga zaidi ya 670. (Mdo. 2:9-11) Watu wa Mungu wamechapa vichapo vingi sana na katika luga nyingi; na kwa hiyo, ujumbe wa Ufalme umewafikia watu katika sehemu zote za dunia. * Huo pia ni ushuhuda ulio wazi kwamba Yehova anatumia Mufalme Yesu Kristo ili kuongoza kazi ya kuhubiri. (Mt. 28:19, 20) Kwa hiyo, wakati tutazungumuzia tena vyombo fulani ambavyo tumetumia ili kutimiza kazi ya kuhubiri katika miaka zaidi ya 100 iliyopita, fikiria vizuri namna Mufalme ameendelea kutuzoeza ili tupendezwe na kila mutu kipekee, na namna ametuchochea ili tuwe waalimu wa Neno la Mungu.​—2 Tim. 2:2.

Mufalme Anawapatia Watumishi Wake Vyombo Ili Kupanda Mbegu ya Ile Kweli

3. Sababu gani tunatumia vyombo mbalimbali katika kazi yetu ya kuhubiri?

3 Yesu alifananisha “neno la Ufalme” na mbegu, na alifananisha moyo wa mutu na udongo. (Mt. 13:18, 19) Mulimaji anaweza kutumia vyombo mbalimbali ili kuregeza na kutayarisha udongo mbele ya kupanda mbegu. Vilevile watu wa Yehova wametumia vyombo mbalimbali ili kutayarisha mioyo ya mamilioni ya watu kupokea ujumbe wa Ufalme. Hata hivyo, kuna vyombo ambavyo walitumia kwa wakati fulani tu. Lakini vingine, kama vile vitabu na magazeti, vinaendelea kufanya kazi ya maana sana. Katika Sura ya 7, tulitaja vyombo na njia mbalimbali zilizotumiwa ili kuhubiria vikundi vikubwa vya watu. Lakini vyombo vyote ambavyo tutazungumuzia katika sura hii vilisaidia wahubiri wa Ufalme kuzungumuza na watu moja kwa moja.​—Mdo. 5:42; 17:2, 3.

Mahali pa kutengenezea mashini za kupiga foto na vikuza sauti katika Toronto, Canada

4, 5. Namna gani fono zenye kuwa na hotuba za Biblia zenye kurekodiwa zilitumiwa, lakini kazi ya fono ilikosa ufundi gani?

4 Hotuba ambazo zilirekodiwa. Kuanzia mwaka wa 1930 mupaka mwaka wa 1940, wahubiri walitumia fono ambazo zilikuwa rahisi kubeba kwa mukono, na zilikuwa na hotuba za Biblia ambazo zilirekodiwa. Kila hotuba haikuwa inapita dakika 5. Wakati mwingine hotuba hizo zilikuwa tu na vichwa vifupi, kama vile “Utatu,” “Matohara,” ao “Ufalme.” Hotuba hizo zenye kurekodiwa zilitumiwa namna gani? Ndugu Clayton Woodworth ambaye alibatizwa katika mwaka wa 1930, Amerika, alisema hivi: “Nilibeba kwa mukono kisanduku kidogo chenye kuwa na fono, na nilitayarisha mambo yote ili niweze kuchezesha fono bila kuchelewa. Wakati nilikaribia mulango fulani, nilifungua kisanduku hicho, nilitia mukono wa fono juu ya diske, na kisha niligonga kwenye mulango. Wakati mwenye nyumba alifungua mulango, nilimuambia hivi: ‘Nina ujumbe wa maana sana ambao ningependa usikilize.’” Watu walionyesha hali gani? Ndugu Woodworth alisema hivi: “Mara nyingi watu walipendezwa na ujumbe huo. Na wakati mwingine, watu walikuwa wanatufungia mulango. Kuna wakati pia watu walifikiri kwamba tulikuwa tunauzisha fono.”

Kufikia mwaka wa 1940, tulikuwa tumepata hotuba mbalimbali zaidi ya 90 ambazo zilirekodiwa, na diske zaidi ya milioni moja zilikuwa zimetengenezwa

5 Kufikia mwaka wa 1940, tulikuwa na hotuba mbalimbali zaidi ya 90 ambazo zilirekodiwa na diske zaidi ya milioni moja ambazo zilikuwa zimetengenezwa. Ndugu John E. Barr, ambaye alikuwa painia wakati huo katika inchi ya Uingereza, na ambaye kisha alitumika katika Baraza Lenye Kuongoza, alisema hivi: “Kuanzia mwaka wa 1936 mupaka mwaka wa 1945, fono ilikuwa rafiki yangu wa siku zote. Katika siku hizo zote, nilijisikia kuwa singeweza kufanya kitu bila fono. Kusikiliza sauti ya Ndugu Rutherford kwenye mulango ilitutia moyo sana; ilikuwa kama vile ulikuwa unahubiri naye. Hata hivyo, kazi ya fono ilikosa ufundi fulani wa kuhubiri, ni kusema, ufundi wa kugusa mioyo ya watu.”

6, 7. (a) Kutumia karte za kutoa ushahidi kulikuwa na faida gani, na sababu gani tunasema zilikuwa na mipaka? (b) Namna gani Yehova alitia maneno katika vinywa vyetu?

6 Karte za kutoa ushahidi. Kuanzia mwaka wa 1933, wahubiri walitiwa moyo kutumia karte za kutoa ushahidi katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba. Karte moja ya kutoa ushahidi, ilikuwa na upana wa karibu santimetre 8 na urefu wa karibu santimetre 13. Ilikuwa na ujumbe mufupi wa Biblia na ilionyesha kichapo chenye kutegemea Biblia ambacho mwenye nyumba angeweza kupata. Muhubiri alikuwa tu anamupatia mwenye nyumba karte hiyo na kumuomba aisome. Dada Lilian Kammerud ambaye kisha alikuwa misionere katika Puerto Rico na Argentina alisema hivi: “Nilifurahia sana kutumia karte ya kutoa ushahidi.” Sababu gani dada Lilian alisema hivyo? Alisema hivi: “Si kila mutu angeweza kutoa ujumbe kwa njia yenye kuvutia. Kwa hiyo, karte ilinisaidia nizoee kuwakaribia watu.”

Karte ya kutoa ushahidi (katika luga ya Kiitaliano)

7 Ndugu David Reusch ambaye alibatizwa katika mwaka wa 1918, alisema hivi: “Karte za kutoa ushahidi zilisaidia ndugu, kwa sababu wengi hawakuwa na uwezo wa kusema mambo kama inavyostahili.” Hata hivyo, karte hizo zilikuwa na mipaka. Ndugu Reusch alisema tena hivi: “Wakati fulani watu walifikiri kwamba hatungeweza kusema. Kwa sababu, wengi wetu hawakuwa wanasema jambo lolote. Lakini, kwa sababu sisi ni watumishi wa Yehova, yeye alikuwa anatutayarisha ili tuwe na uwezo wa kuhubiria watu wengi. Kisha muda mufupi alitia maneno katika kinywa chetu kwa kutufundisha namna ya kutumia Maandiko kwenye mulango. Jambo hilo lilitimia kupitia Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi ambayo yalianza katika mwaka wa 1940.”​—Soma Yeremia 1:6-9.

8. Namna gani unaweza kumuacha Kristo akuzoeze?

8 Vitabu. Tokea mwaka wa 1914, watu wa Yehova walikuwa wamechapa vitabu zaidi ya 100 ambavyo vilikuwa vinazungumuzia habari mbalimbali za Biblia. Kati ya vitabu hivyo, vingine vilichapishwa tu ili kuzoeza wahubiri wapate matokeo mazuri katika mahubiri. Dada Anna Larsen wa inchi ya Danemark, na ambaye amekuwa muhubiri kwa miaka 70 hivi, alisema hivi: “Kupitia Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi na vichapo vingine, Yehova ametusaidia kupata matokeo zaidi katika mahubiri. Ninakumbuka kitabu cha kwanza kutokea kati ya vitabu hivyo, ni kitabu Aide théocratique pour les proclamateurs du Royaume, ambacho kilitokea katika mwaka wa 1945. Kisha katika mwaka wa 1946 kulitokea kitabu “Équipé pour toute œuvre bonne.” Leo, tunatumia kitabu Faidika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, ambacho kilitolewa katika mwaka wa 2001.” Bila shaka, kitabu Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na vitabu vingine vimetusaidia ili tuwe wahudumu [wahubiri] wa Yehova wenye kustahili vya kutosha. (2 Kor. 3:5, 6) Umejiandikisha kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi? Kila juma kwenye mukutano wa Masomo ya Kiteokrasi unaleta kitabu chako Shule ya Huduma ili ufuate wakati mwangalizi ambaye anaongoza masomo anakitumia? Ikiwa unafanya hivyo, utamupatia Kristo nafasi ya kukuzoeza ili uwe mwalimu muzuri.​—2 Kor. 9:6; 2 Tim. 2:15.

9, 10. Vitabu vimefanya kazi gani katika kupanda na kumuangia mbegu za ile kweli maji?

9 Pia, Yehova ametusaidia kupitia tengenezo lake, ambalo linachapisha vichapo ambavyo vinasaidia wahubiri kufasiria mafundisho ya musingi ya Biblia. Kwa mufano: Kitabu Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele kilikuwa na matokeo mazuri katika mahubiri. Kilitolewa kwa mara ya kwanza katika mwaka wa 1968 na watu walipendezwa sana na kitabu hicho. Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 11, 1968, ilisema kwamba, “katika Mwezi wa 9, kwenye kazi ya kuchapisha vichapo ya Brooklyn, waliongeza kikundi cha ndugu ili kutumika usiku, kwa sababu maombi ya kitabu Kweli Iongozayo yaliongezeka sana.” Huduma hiyo iliendelea kusema hivi: “Wakati fulani katika Mwezi wa 8, maombi ya vitabu Kweli Iongozayo yaliongezeka kufikia zaidi ya milioni moja na nusu!” Kufikia mwaka wa 1982, kulichapishwa vitabu zaidi ya milioni 100, katika luga 116. Katika miaka 14, ni kusema, kuanzia mwaka wa 1968 mupaka mwaka wa 1982, kitabu Kweli Iongozayo kilisaidia kuwe na ongezeko la wahubiri wa Ufalme zaidi ya milioni moja. *

10 Katika mwaka wa 2005, kulitokea kitabu kingine cha pekee ambacho kinasaidia watu kujifunza Biblia, ni kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Vitabu milioni 200 hivi vimechapishwa katika luga 256! Matokeo ni gani? Katika miaka saba tu, ni kusema, kuanzia mwaka wa 2005 mupaka mwaka wa 2012, watu zaidi ya milioni moja wamekuwa wahubiri wa habari njema. Pia katika kipindi hicho, hesabu ya watu ambao wanajifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova, imeongezeka kutoka milioni 6 mupaka karibu milioni 9. Ni wazi kwamba Yehova amebariki bidii yetu ya kupanda na kumuangia maji mbegu za ile kweli ya Ufalme.​—Soma 1 Wakorintho 3:6, 7.

11, 12. Kwa kutumia maandiko ambayo yanatajwa, fasiria ni kwa ajili ya watu gani mbalimbali magazeti yetu yanachapishwa.

11 Magazeti. Mwanzoni, gazeti Munara wa Mulinzi lilichapishwa kwanza kwa ajili ya ‘kundi ndogo,’ ni kusema, wale wanaoitwa na Mungu kuenda mbinguni. (Lu. 12:32; Ebr. 3:1) Tarehe 1 Mwezi wa 10, 1919, tengenezo la Yehova lilichapisha gazeti lingine ambalo lingetumiwa ili kuhubiria watu wengi tofauti. Gazeti hilo lilipendwa sana na Wanafunzi wa Biblia na vilevile watu wengine. Kwa hiyo, kwa miaka mingi liligawanywa sana kuliko Munara wa Mulinzi. Gazeti hilo liliitwa kwanza L’Âge d’Or. Katika mwaka wa 1937, liliitwa Consolation. Kisha katika mwaka wa 1946, likaitwa Amuka!

12 Kwa miaka mingi, ukubwa na namna ya kuandika habari katika Munara wa Mulinzi na Amuka! imeendelea kubadilika, lakini kusudi limebaki lilelile, ni kusema, kutangaza Ufalme wa Mungu na kufanya watu watumainie Biblia. Leo, tuna gazeti Munara wa Mulinzi kwa ajili ya funzo na lingine kwa ajili ya watu wote. Gazeti la funzo linachapishwa kwa ajili ya “watumishi wa nyumbani,” ni kusema, ‘kundi ndogo’ na “kondoo wengine.”[3] (Mt. 24:45; Yoh. 10:16) Gazeti la watu wote linatayarishwa hasa kwa ajili ya wale ambao hawajajua kweli lakini wanaheshimu Biblia na wanamuheshimu Mungu. (Mdo. 13:16) Gazeti Amuka! linatayarishwa hasa kwa ajili ya wale ambao hawajue mengi juu ya Biblia na juu ya Mungu wa kweli Yehova.​—Mdo. 17:22, 23.

13. Ni nini unaona kuwa jambo la ajabu kuhusu magazeti yetu? (Muzungumuzie pia kisanduku “ Vichapo Ambavyo Vinachapishwa Zaidi Duniani.”)

13 Kufikia mwanzo wa mwaka wa 2014, kila mwezi kumechapishwa gazeti Amuka! zaidi ya milioni 44 na gazeti Munara wa Mulinzi zaidi ya milioni 46. Gazeti Amuka! limetafsiriwa katika luga 100 hivi, na gazeti Munara wa Mulinzi katika luga zaidi ya 200. Kwa hiyo, magazeti Amuka! na Munara wa Mulinzi ndiyo magazeti ambayo yanatafsiriwa na kugawanywa sana kuliko magazeti mengine duniani pote! Hilo halipaswe kutushangaza hata kidogo. Kwa sababu magazeti hayo yana ujumbe ambao Yesu alisema utahubiriwa katika dunia yote inayoikaliwa.​—Mt. 24:14.

14. Ni jambo gani tumefanya kwa bidii, na sababu gani?

14 Biblia. Katika mwaka wa 1896, Ndugu Russell na wenzake walibadilisha jina la shirika ambalo walitumia ili kuchapisha vichapo. Kufanya hivyo, kuliwasaidia watie katika jina hilo neno Biblia. Kwa hiyo, shirika hilo lilichukua jina la Watch Tower Bible and Tract Society. Mabadiliko hayo yalikuwa ya maana sana kwa sababu Biblia ndicho chombo cha kwanza ambacho tunatumia sana ili kutangaza habari njema ya Ufalme. (Lu. 24:27) Kulingana na jina hilo ambalo lilikubaliwa kisheria, kwa bidii watumishi wa Mungu walilipia wenyewe garama za kugawanyia watu Biblia na kuwatia moyo wasome Biblia. Kwa mufano, katika mwaka 1926 tulichapa kupitia mashine yetu, Biblia Emphatic Diaglott, tafsiri ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, ambayo ilitafsiriwa na Benjamin Wilson. Kuanzia mwaka wa 1942, tulichapa na kugawanya Biblia ya King James Version, 700000 hivi. Kisha miaka mbili tu, tulianza kuchapisha Biblia ya American Standard Version, ambayo ilitumia jina Yehova mara 6 823. Kufikia mwaka wa 1950, tulikuwa tumegawanya Biblia 250000.

15, 16. (a) Ni jambo gani linakufurahisha wakati unasoma Tafsiri ya Ulimwengu Mpya? (Muzungumuzie pia kisanduku “ Kuharakisha Kazi ya Kutafsiri Biblia.”) (b) Namna gani unaweza kumuacha Yehova aguse moyo wako?

15 Katika mwaka wa 1950, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ilitolewa. Tafsiri nzima katika buku moja ya Biblia Takatifu​—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ilitolewa katika mwaka wa 1961. Tafsiri hiyo inamutukuza Yehova kwa kurudisha jina lake mahali pake kama vile ilikuwa katika maandishi ya kwanza-kwanza ya Kiebrania. Vilevile jina la Mungu linapatikana mara 237 katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Ili kuhakikisha kwamba Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ni tafsiri iliyo sahihi (isiyokuwa na makosa) na yenye kusomwa kwa urahisi, imekaguliwa ao kutafsiriwa upya mara nyingi, na imefanyiwa hivyo hivi karibuni katika mwaka wa 2013. Kufikia mwaka wa 2013, Biblia zaidi ya milioni 201 ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya zimechapishwa kwa sehemu ao yote nzima katika luga 121.

16 Namna gani watu wanajisikia wakati wanasoma Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika luga yao? Mwanaume mumoja wa Nepal alisema hivi: “Kwa miaka mingi, ilikuwa vigumu kuelewa tafsiri iliyokuwa katika luga ya Nepal, kwa sababu ilitumia luga ya watu wenye elimu wa zamani. Lakini sasa tunaweza kuelewa Biblia vizuri sana kwa sababu inatumia luga ambayo watu wanazungumuza kila siku.” Mwanamuke fulani wa Jamuhuri ya Afrika ya Kati alipata Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika luga ya Sango, na wakati alianza kuisoma alitoa machozi na kusema: “Hii ni luga ya moyo wangu.” Kama huyo mwanamuke, kila mutu anaweza kuacha Yehova aguse moyo wake, kwa kusoma Neno lake kila siku.​—Zab. 1:2; Mt. 22:36, 37.

Kuonyesha Shukrani Juu ya Vyombo na Mazoezi Yanayotolewa

17. Namna gani unaweza kuonyesha kwamba unafurahia vyombo na mazoezi ambayo unapata, na utapata faida gani kwa kufanya hivyo?

17 Unafurahia vyombo na mazoezi ya kila siku ambayo Mufalme Yesu Kristo anatupatia? Unajipatia wakati ili kusoma vichapo ambavyo tengenezo la Mungu linatutolea, na unavitumia ili kusaidia wengine? Ikiwa unafanya hivyo, utakuwa kama Dada Opal Betler, ambaye alibatizwa tarehe 4 Mwezi wa 10, 1914. Dada Opal alisema hivi: “Kwa miaka mingi mimi na bwana yangu [Edward] tulitumia fono na karte za kutoa ushahidi. Tulitoa ushahidi nyumba kwa nyumba kwa kutumia vitabu, vijitabu na magazeti. Tulifanya kampanye na tulitembea kama watu ambao wanafanya maandamano, na tuligawanya ujumbe mbalimbali wenye kuchapishwa. Kisha muda kidogo tulizoezwa kufanya marudio ao kurudilia watu na kuongoza mafunzo ya Biblia na watu ambao walipendezwa. Maisha hayo yenye mambo mengi yalituletea furaha.” Yesu aliahidi kwamba raia wake wangekuwa na mengi ya kufanya katika kupanda, kuvuna, na wangefurahi. Kama dada Opal, ndugu na dada wengi wanaweza kushuhudia ukweli wa ahadi hiyo ya Yesu.​—Soma Yohana 4:35, 36.

18. Tuna pendeleo gani leo?

18 Watu wengi ambao hawajamutumikia Mufalme wanaweza kuwaona watu wa Mungu kuwa watu “wasio na elimu na watu wa kawaida.” (Mdo. 4:13) Lakini fikiri kidogo! Mufalme ametumia watu hao wa kawaida kuwa nyumba yenye nguvu ambayo inachapisha vichapo ambavyo vinatafsiriwa na kugawanywa sana kuliko vichapo vingine katika historia! Jambo la maana sana ni kwamba, ametuzoeza na kutuchochea kutumia vyombo hivyo mbalimbali ili kutangaza habari njema kwa watu wa mataifa yote. Bila shaka, ni pendeleo kubwa kutumika pamoja na Kristo katika kupanda mbegu za ile kweli na kuvuna wanafunzi!

^ fu. 2 Katika miaka kumi tu iliyopita, watu wa Yehova wamechapisha vichapo vyenye kutegemea Biblia zaidi ya miliare 20. Zaidi ya hiyo, tuna adresi yetu ya Internete ambayo watu karibu miliare 3 duniani wanaweza kufungua.

^ fu. 9 Kulikuwa pia na vitabu fulani vyenye kutegemea Biblia ambavyo vilisaidia wahubiri kufundisha kweli ya Biblia. Vitabu hivyo ni: La Harpe de Dieu (kilichapishwa mwaka wa 1921), “Que Dieu soit reconnu pour vrai!” (kilichapishwa mwaka wa 1946), Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani (kilichapishwa mwaka wa 1982), na Ujuzi Uongozao Kwenye Uzima wa Milele (kilichapishwa mwaka wa 1995).

Soma habari katika gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi wa 7, 2013, ukurasa wa 23, fungu la 13, ambayo inatutolea mafasirio yaliyo wazi juu ya “watumishi wa nyumbani.”