Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 21

Uko Mwenye Shukrani kwa Ajili ya Zawadi Zenye Mungu Amekupatia?

Uko Mwenye Shukrani kwa Ajili ya Zawadi Zenye Mungu Amekupatia?

Mambo yenye umefanya ni mengi sana, Ee Yehova Mungu wangu, kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea.”​ZB. 40:5.

WIMBO 5 Kazi za Mungu za Ajabu

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Kulingana na Zaburi 40:5, Yehova ametupatia zawadi gani, na juu ya nini tutazungumuzia zawadi hizo?

YEHOVA ni Mungu mukarimu. Fikiria zawadi fulani zenye ametupatia: dunia yetu ya muzuri sana, makao yetu ya pekee; ubongo wetu wenye umeumbwa kwa njia ya ajabu; na Neno lake la maana sana, Biblia. Kwa sababu Yehova ametupatia zawadi hizo tatu, tuko na nafasi ya kuishi, tuko na uwezo wa kufikiri na kuzungumuza, na zaidi sana tuko na majibu ya maulizo ya maana sana yenye tunaweza kujiuliza.​—Soma Zaburi 40:5.

2 Katika habari hii, tutazungumuzia kwa kifupi zawadi hizo tatu. Kadiri tunafikiri sana juu ya zawadi hizo, ni vile tutazifurahia zaidi na tutatamani zaidi kumufurahisha Yehova, Muumbaji wetu mwenye upendo. (Ufu. 4:11) Tutaweza pia kusaidia wale wenye wamedanganywa na fundisho la uongo la mageuzi.

SAYARI YETU YA PEKEE

3. Juu ya nini dunia ni ya pekee?

3 Hekima ya Mungu inaonekana wazi kupitia namna ameumba dunia, makao yetu. (Ro. 1:20; Ebr. 3:4) Haiko dunia tu njo sayari (planète) yenye inazungukaka jua, lakini dunia iko ya pekee kwa sababu iko na hali zenye kufaa ili kuendeleza uzima wa mwanadamu.

4. Juu ya nini tunaweza kusema kama dunia ni ya muzuri kuliko mashua yoyote yenye kutengenezwa na mwanadamu?

4 Katika hali fulani, dunia iko kama mashua ya maji yenye kusafiri mu bahari kubwa. Lakini, kuko tofauti kubwa kati ya dunia na mashua yenye kutengenezwa na mwanadamu yenye kujaa watu. Kwa mufano, watu wenye kuwa mu mashua wanaweza kuishi kwa muda gani ikiwa wanapaswa kujitengenezea oksijeni (ao hewa ya muzuri yenye tunapumua), chakula, na maji yao wenyewe na ikiwa hawawezi kutupa uchafu inje ya mashua? Watu wenye kuwa mu mashua hiyo wanaweza kufa haraka. Tofauti na ile mashua ya maji, dunia iko na uwezo wa kufanya mamiliare ya watu na wanyama waendelee kuishi. Inatoa oksijeni, chakula, na maji yote yenye tuko nayo lazima, na vitu hivyo vya maana haviishe hata siku moja. Hata kama hatuwezi kutupa uchafu inje ya dunia, dunia inaendelea kuwa yenye kupendeza na mahali pa muzuri pa kuishi. Jambo hilo linawezekana namna gani? Yehova ameumba dunia na uwezo wa kugeuza uchafu kuwa kitu fulani cha muzuri chenye kinaweza kutumiwa tena. Tutazungumuzia kwa kifupi mizunguko mbili ya muzuri sana: muzunguko wa oksijeni na muzunguko wa maji.

5. Muzunguko wa oksijeni ni nini, na unatuhakikishia jambo gani?

5 Oksijeni ni gaze yenye watu na wanyama wako nayo lazima ili waendelee kuishi. Watu na wanyama wanapumua oksijeni mingi sana kila mwaka. Viumbe hivyo vyenye uzima vinatoa hewa chafu yenye kuitwa karboni dioksidi. Lakini, viumbe hivyo vyenye uzima havimalizake oksijeni yote, na angahewa (atmosphère) haijajaa hata siku moja hewa chafu ao karboni dioksidi. Juu ya nini? Ni juu Yehova ameumba pia aina mbalimbali za mimea yenye ukubwa tofauti-tofauti yenye inavuta karboni dioksidi na kutoa oksijeni. Kwa sababu muzunguko huo unatoa hewa yenye tunapumua, jambo hilo linahakikisha kama maneno ya andiko la Matendo 17:24, 25 ni ya kweli. Andiko hilo linasema hivi: “Mungu . . . anapatia watu wote uzima na pumuzi.”

6. Muzunguko wa maji ni nini, na unatuhakikishia jambo gani? (Ona pia kisanduku “ Zawadi ya Yehova ya Muzunguko wa Maji.”)

6 Kwa sababu dunia iko kwenye umbali wenye kufaa kutoka kwenye jua, iko na hali ya joto yenye kufaa yenye inafanya maji isigande wala kuyeyuka. Kama dunia ingekuwa karibu kidogo na jua, maji yote ingekuwa muvuke na dunia yote ingekuwa joto na hakuna kiumbe chenye kingeweza kuishi ku dunia. Kama dunia ingekuwa tena mbali kidogo tu na jua, maji yote ingeganda na kufanya dunia ikuwe jiwe kubwa la barafu. Kwa sababu Yehova ametia dunia pa nafasi yenye kufaa kabisa, muzunguko wa maji unafanya uzima uendelee. Jua linapiga maji yenye kuwa mu bahari na ku dunia na linafanya ile maji kuwa muvuke ili kufanyiza mawingu. Kila mwaka, jua linafanya mamilioni ya mamilioni ya litre za maji ikuwe muvuke. Ile maji inabakia katika angahewa kwa siku karibu kumi mbele ianguke tena kuwa mvua ao teluji. Kisha, ile maji inarudia tena mu bahari ao mu mito ingine, na muzunguko unaendelea. Yehova amefanya muzunguko huo ili dunia iendelee kuwa na maji. Jambo hilo linahakikisha kama Yehova ni mwenye hekima na mwenye nguvu.​—Yob. 36:27, 28; Muh. 1:7.

7. Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha shukrani kwa ajili ya zawadi yenye kuzungumuziwa mu Zaburi 115:16?

7 Tunaweza kufanya nini ili tukuwe wenye shukrani zaidi kwa ajili ya dunia yetu ya ajabu na mambo yote ya muzuri yenye kuwa ndani? (Soma Zaburi 115:16.) Jambo moja ni kufikiri sana juu ya vitu vyenye Yehova amefanya. Kufanya vile kutatuchochea tumushukuru Yehova kila siku kwa ajili ya mambo ya muzuri yenye anatupatia. Pia, tunaonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya dunia yenye Mungu ametupatia wakati tunajikaza sana ili kufanya mahali kwenye tunaishi kuendelee kuwa safi.

UBONGO WETU WA AJABU

8. Juu ya nini tunaweza kusema kama ubongo wetu umeumbwa kwa njia ya ajabu?

8 Ubongo wa mwanadamu umeumbwa kwa njia ya ajabu. Wakati ulikuwa katika tumbo la uzazi la mama yako, ubongo wako ulikomaa kwa njia yenye ilipangwa muzuri, na maelfu ya chembe za mupya za ubongo ilikuwa inaundwa kila dakika! Wachunguzi wanakadiria kama ubongo wa mutu muzima uko na chembe za pekee karibu miliare 100 zenye kuitwa nyuroni (neurones). Chembe hizo zinafanyiza ubongo wetu wenye kuwa na uzito wa kilograme 1 na nusu. Fikiria uwezo fulani tu wa ajabu wa ubongo wetu.

9. Ni nini inaonyesha kama uwezo wetu wa kusema ni zawadi yenye Mungu ametupatia?

9 Uwezo wetu wa kusema ni muujiza. Fikiria kidogo mambo yenye inafanyika wakati tunasema. Ili kusema kila neno, ubongo wako unapaswa kuongoza kwa wakati uleule misuli (muscles) 100 hivi yenye kuwa katika ulimi, koo, midomo, taya (mufupa wa kinywa wenye kubeba meno), na kifua. Ile misuli yote inapaswa kutumika kulingana na utaratibu fulani ili uweze kusema maneno yenye itaeleweka. Kuhusu uwezo wa kusema luga mbalimbali, uchunguzi fulani wenye ulichapishwa mu mwaka wa 2019 ulionyesha kama watoto wadogo wanaweza kutambua neno moja moja. Uchunguzi huo unaunga mukono wazo hili lenye wachunguzi wengi wanaamini: tunazaliwa na uwezo wa kutambua na kujifunza luga mbalimbali. Kwa kweli, uwezo wetu wa kusema ni zawadi yenye Mungu ametupatia.​—Kut. 4:11.

10. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya zawadi ya kusema yenye Mungu ametupatia?

10 Njia moja ya kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya zawadi yetu ya kusema ni kuelezea wale wenye wanaamini mageuzi sababu gani tunaamini kama Mungu njo aliumba vitu vyote. (Zb. 9:1; 1 Pe. 3:15) Wale wenye kuamini fundisho la mageuzi wanaweza kupenda tuamini kama dunia na uzima vimejitokeza vyenyewe. Kwa kutumia Biblia na mawazo fulani yenye tumezungumuzia katika habari hii, tunaweza kutetea Baba yetu wa mbinguni na kusaidia wale wenye kuwa tayari kusikiliza wajue juu ya nini tuko hakika kama Yehova njo Muumbaji wa mbingu na dunia.​—Zb. 102:25; Isa. 40:25, 26.

11. Taja sababu moja yenye kuonyesha kama ubongo wetu ni wa ajabu.

11 Uwezo wetu wa kukumbuka mambo ni wa ajabu. Zamani, muandikaji mumoja alikadiria kwamba ubongo wa mwanadamu uko na uwezo wa kukumbuka habari zenye zinaweza kujaza vitabu milioni 20. Lakini, leo inawaziwa kama ubongo uko na uwezo mukubwa zaidi. Kwa sababu ya uwezo wetu wa kukumbuka mambo, sisi wanadamu tuko na uwezo gani mwingine wa pekee?

12. Sisi wanadamu tuko na uwezo wa kujifunza namna tunapaswa kuishi. Namna gani jambo hilo linafanya tukuwe tofauti na wanyama?

12 Kati ya viumbe vyote ku dunia, wanadamu tu njo wako na uwezo wa kujifunza namna wanapaswa kuishi, kwa kukumbuka na kwa kufikiria mambo yenye iliwafikia zamani. Kwa sababu tuko na uwezo huo, tunaweza kujifunza kanuni za muzuri na kubadilisha namna yetu ya kuwaza na kuishi. (1 Ko. 6:9-11; Kol. 3:9, 10) Kwa kweli, tunaweza kuzoeza zamiri yetu kufanya tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa. (Ebr. 5:14) Tunaweza kujifunza kuonyesha upendo, huruma, na rehema. Na tunaweza kujifunza kuiga haki ya Yehova.

13. Kulingana na Zaburi 77:11, 12, namna gani tunapaswa kutumia uwezo wetu wa kukumbuka mambo?

13 Njia moja ya kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya zawadi ya uwezo wa kukumbuka mambo, ni kujikaza kukumbuka kila wakati namna Yehova ametusaidia na kutufariji wakati wenye umepita. Kama tunafanya vile, tutakuwa hakika kama atatusaidia pia wakati wenye kuja. (Soma Zaburi 77:11, 12; 78:4, 7) Njia ingine ni kukumbuka mambo ya muzuri yenye watu wengine wanatufanyia na kuwa wenye shukrani kwa ajili ya mambo yenye wanafanya. Wachunguzi wamevumbua kama mara mingi watu wenye kuonyesha shukrani ni watu wenye furaha. Ni muzuri pia tumuige Yehova kwa kuamua kusahau mambo fulani. Kwa mufano, Yehova iko na uwezo wa kukumbuka mambo kwa ukamilifu, lakini kama tunatubu, anaamua kusamehe na kusahau makosa yenye tunamufanyia. (Zb. 25:7; 130:3, 4) Na anapenda tutendee wengine vile wakati wanatuomba musamaha juu ya makosa yenye wamefanya, yenye inatuumiza.​—Mt. 6:14; Lu. 17:3, 4.

Tunaonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya zawadi ya ubongo wakati tunaitumia ili kumutukuza Yehova (Ona fungu la 14) *

14. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya zawadi ya muzuri ya ubongo?

14 Tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya zawadi ya muzuri ya ubongo kwa kuitumia ili kumutukuza Mungu mwenye alitupatia ile zawadi. Watu fulani wanaamua kutumia ubongo wao ili kutafuta faida zao wenyewe, ni kusema, wanajiwekea kanuni zao wenyewe juu ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa. Lakini, kwa sababu Yehova njo mwenye alituumba, ni jambo lenye kupatana na akili kuona kanuni zake kuwa za muzuri zaidi kupita kanuni zote zenye tunaweza kujiwekea wenyewe. (Ro. 12:1, 2) Wakati tunafuata kanuni za Yehova, tunakuwa na amani. (Isa. 48:17, 18) Na tunatambua mambo yenye anapenda tufanye katika maisha yetu, ni kusema, kumutukuza Muumbaji wetu na Baba yetu na kumufurahisha.​—Mez. 27:11.

BIBLIA NI ZAWADI YA MAANA SANA

15. Namna gani zawadi ya Biblia inaonyesha kama Mungu anatupenda?

15 Biblia ni zawadi yenye Mungu ametupatia yenye kuonyesha kama anatupenda. Baba yetu wa mbinguni aliongoza watu kupitia roho yake ili waandike Biblia kwa sababu anatuhangaikia sana. Kupitia Biblia, Yehova anajibu maulizo ya maana sana yenye tunaweza kujiuliza; maulizo kama vile: Tulitoka wapi? Juu ya nini tunaishi? Na maisha itakuwa namna gani wakati wenye kuja? Yehova anapenda sisi wote tupate majibu ya ile maulizo, kwa hiyo, amechochea watu watafsiri Biblia katika luga mingi. Leo, Biblia inapatikana, ikiwa nzima ao sehemu, katika luga zaidi ya 3 000! Katika historia yote, Biblia njo kitabu chenye kutafsiriwa na kugawanywa zaidi kuliko vitabu vingine vyote. Hata kama watu wanaishi wapi ao wanazungumuza luga gani, wengi wako na nafasi ya kujifunza Biblia katika luga zao wenyewe.​—Ona kisanduku “ Kutafsiri Biblia Katika Luga za Afrika.”

16. Kulingana na Matayo 28:19, 20, namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya Biblia?

16 Tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya Biblia kwa kuisoma kila siku, kufikiri sana juu ya mambo yenye inafundisha, na kujikaza sana kutumia mambo yenye tunajifunza. Tena, tunaonyesha kama tuko wenye shukrani kwa Mungu kwa kufanya yote yenye tunaweza ili kuambia watu wengi kadiri inawezekana juu ya ujumbe wa Biblia.​—Zb. 1:1-3; Mt. 24:14; soma Matayo 28:19, 20.

17. Katika habari hii, tumezungumuzia zawadi gani, na tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

17 Katika habari hii, tumezungumuzia zawadi mbalimbali zenye Mungu ametupatia, kwa mufano dunia, makao yetu; ubongo wetu wenye umeumbwa kwa njia ya ajabu; na Biblia, Neno la Mungu lenye liliongozwa na roho yake. Lakini kuko zawadi zingine zenye Yehova ametupatia zenye hatuwezi kuona. Katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia zawadi hizo zenye hatuwezi kuona.

WIMBO 12 Mungu Mkuu, Yehova

^ fu. 5 Habari hii itatusaidia tukuwe wenye shukrani zaidi kwa Yehova na kwa ajili ya zawadi tatu zenye ametupatia. Itatuonyesha pia namna ya kufikiri na watu wenye wako na mashaka ikiwa Mungu iko.

^ fu. 64 MAFASIRIO YA PICHA: Dada anajifunza luga mupya ili kufundisha watu wenye wametoka katika inchi ingine kweli za Neno la Mungu.