Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 8

Fuatilia Amani kwa Kupiganisha Wivu

Fuatilia Amani kwa Kupiganisha Wivu

“Tufuatilie mambo yenye yanafanya kukuwe amani na mambo ya kujengana mumoja na mwingine.”​—RO. 14:19.

WIMBO 113 Amani Tuliyo Nayo

KIFUPI CHA HABARI *

1. Wivu ulileta matokeo gani katika familia ya Yosefu?

YAKOBO alipenda watoto wake wanaume wote, lakini alimupenda sana Yosefu, mwenye wakati huo alikuwa na miaka 17. Ndugu za Yosefu walitenda namna gani? Walimusikilia wivu, na wivu huo ulifanya wamuchukie. Yosefu hakufanya kitu chochote chenye kilifanya ndugu zake wamuchukie. Hata hivyo, walimuuzisha Yosefu katika utumwa na wakamudanganya baba yao, kwa kusema kama munyama wa pori alimuua mutoto wake mupendwa. Wivu uliwachochea waharibu amani ya familia na kumuvunja baba yao moyo.​—Mwa. 37:3, 4, 27-34.

2. Kulingana na Wagalatia 5:19-21, juu ya nini wivu ni hatari sana?

2 Katika Maandiko, wivu * unatajwa kati ya “matendo ya mwili” yenye kuleta kifo yenye inaweza kufanya mutu akose kuriti Ufalme wa Mungu. (Soma Wagalatia 5:19-21.) Mara mingi, wivu unaleta matunda yenye sumu kama vile uadui, mizozo, na milipuko ya kasirani.

3. Tutazungumuzia nini mu habari hii?

3 Mufano wa ndugu za Yosefu unaonyesha namna wivu unaweza kuharibu urafiki na kuvuruga amani yenye ilikuwa katika familia. Hata kama hatuwezi kufanya jambo lenye ndugu za Yosefu walifanya, sisi wote tuko na moyo mudanganyifu na wenye haukamilike. (Yer. 17:9) Njo maana wakati fulani tunaweza kusikilia wengine wivu. Tuone basi mifano fulani ya Biblia yenye kutuonya yenye inaweza kutusaidia tujue sababu gani wivu unaweza kukomaa katika moyo wetu. Kisha, tutaona mambo yenye tunaweza kufanya ili kupiganisha wivu na kuendeleza amani.

MAMBO YENYE INAWEZA KULETA WIVU

4. Juu ya nini Wafilisti walimusikilia Isaka wivu?

4 Utajiri wa kimwili. Isaka alikuwa mwanaume tajiri, na Wafilisti walimusikilia wivu kwa sababu ya utajiri wake. (Mwa. 26:12-14) Walifunika hata visima vyenye Isaka alikuwa anatumia ili kunywesha wanyama wake. (Mwa. 26:15, 16, 27) Kama Wafilisti, watu fulani leo wanasikilia wivu wale wenye wako na vitu mingi kuwapita. Hawatamani tu vitu vyenye wengine wako navyo lakini pia hawapendi wengine wakuwe na vitu hivyo.

5. Juu ya nini viongozi wa dini walimusikilia Yesu wivu?

5 Kupendwa na wengine. Viongozi wa dini ya Wayahudi walimusikilia Yesu wivu kwa sababu watu wa kawaida walikuwa wanamupenda sana. (Mt. 7:28, 29) Yesu alikuwa mwakilishi wa Mungu, na alikuwa anafundisha kweli. Hata hivyo, viongozi hao wa dini walieneza mambo ya uongo juu ya Yesu ili kumuharibishia sifa. (Mk. 15:10; Yoh. 11:47, 48; 12:12, 13, 19) Habari hiyo inaweza kutufundisha nini? Tunapaswa kujikaza ili tusisikilie wivu wale wenye wanapendwa na ndugu na dada mu kutaniko kwa sababu ya sifa zao za muzuri. Kuliko kuwasikilia wivu, tunapaswa kujikaza ili kuiga sifa zao za muzuri.​—1 Ko. 11:1; 3 Yo. 11.

6. Namna gani Diotrefe alionyesha wivu?

6 Mapendeleo katika kutaniko. Wakati wa mitume, Diotrefe alisikilia wivu wale wenye walikuwa wanaongoza katika kutaniko la Kikristo. Alipenda “kuwa wa kwanza” kati ya ndugu na dada wa kutaniko, kwa hiyo, alieneza habari za uongo ili kumuharibishia sifa mutume Yohana na ndugu wengine wenye walikuwa na madaraka. (3 Yo. 9, 10) Hata kama hatutafanya hata kidogo mambo yenye Diotrefe alifanya, sisi pia tunaweza kuanza kusikilia wivu Mukristo mwenzetu mwenye anapata mugao wenye tulitumaini kupata, zaidi sana kama tunaona kuwa tunaweza kufanya muzuri mugao huo kama vile yeye ao muzuri zaidi kumupita.

Moyo wetu uko kama udongo, na sifa zetu za muzuri ziko kama maua ya muzuri. Lakini wivu uko kama magugu ao mimea yenye sumu. Wivu unaweza kutuzuia tusikomalishe sifa za muzuri kama vile upendo, huruma, na fazili (Ona fungu la 7)

7. Wivu unaweza kutuletea matokeo gani?

7 Wivu uko kama vile magugu ao mimea yenye sumu. Wakati mbegu za wivu zinaota katika moyo wetu, inaweza kuwa nguvu kuziharibu. Tabia zingine za mubaya kama vile kiburi na kujipenda mwenyewe zinaweza kukomalisha wivu. Wivu unaweza kutuzuia tusikomalishe sifa za muzuri kama vile upendo, huruma, na fazili. Wakati tu tunaona wivu unaanza kuota katika moyo wetu, tunapaswa kuondoa wivu huo. Namna gani tunaweza kupiganisha wivu?

KOMALISHA SIFA YA UNYENYEKEVU NA KUTOSHEKA

Namna gani tunaweza kupiganisha wivu wenye uko kama vile magugu? Kwa musaada wa roho takatifu ya Mungu, tunaweza kuondoa mizizi ya wivu na kukomalisha sifa ya unyenyekevu na kutosheka (Ona fungu la 8-9)

8. Ni sifa gani zenye zinaweza kutusaidia kupiganisha wivu?

8 Tunaweza kupiganisha wivu kwa kukomalisha sifa ya unyenyekevu na kutosheka. Kama sifa hizo zinajaa katika moyo wetu, wivu hautakuwa na nafasi. Sifa ya unyenyekevu itatusaidia tusijifikirie kupita kiasi. Mutu munyenyekevu haone kama anastahili mingi zaidi ya wengine wote. (Gal. 6:3, 4) Mutu fulani mwenye kutosheka anafurahia vitu vyenye iko navyo na hajilinganishe na wengine. (1 Ti. 6:7, 8) Wakati mutu munyenyekevu na mwenye kutosheka anaona mutu mwingine anapewa jambo fulani la muzuri, anafurahi pamoja naye.

9. Kulingana na Wagalatia 5:16 na Wafilipi 2:3, 4, roho takatifu itatusaidia kufanya nini?

9 Tuko na lazima ya roho takatifu ya Mungu ili tuepuke wivu na kukomalisha sifa ya unyenyekevu na kutosheka. (Soma Wagalatia 5:16; Wafilipi 2:3, 4.) Roho takatifu ya Yehova inaweza kutusaidia tuchunguze mawazo na nia zetu za ndani kabisa. Kwa musaada wa Mungu, tunaweza kuachana na mawazo na hisia za mubaya na kuwa na mawazo na hisia za muzuri. (Zb. 26:2; 51:10) Fikiria mufano wa Musa na Paulo, wanaume wenye waliweza kabisa kupiganisha tabia ya wivu.

Kijana mumoja Mwisraeli anakimbilia kwenye Musa na Yoshua wako ili kuwaambia kama wanaume wawili mu kambi wanajiendesha kama manabii. Yoshua anamuambia Musa awakataze, lakini Musa anakataa. Kuliko kuwakataza, anaambia Yoshua kama anafurahi kuona kuwa Yehova alitia roho yake juu ya wanaume hao wawili (Ona fungu la 10)

10. Ni hali gani yenye ingemufanya Musa akuwe na wivu? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

10 Musa alikuwa na mamlaka makubwa juu ya watu wa Mungu, lakini hakujaribu kuzuia wengine wasipate mamlaka hiyo. Kwa mufano, wakati fulani, Yehova alichukua sehemu fulani ya roho takatifu yenye Musa alikuwa nayo na akaipatia kikundi cha wazee Waisraeli wenye walikuwa wanasimama karibu na hema ya mukutano. Wakati kidogo kisha pale, Musa alisikia kama wazee wawili wenye hawakuenda ku hema ya mukutano walikuwa wamepata pia roho takatifu na walikuwa wameanza kujiendesha kama manabii. Musa alitenda namna gani wakati Yoshua alimuomba akataze wazee hao wawili? Musa hakusikia wivu kwa sababu Yehova alipatia pia wanaume hao pendeleo hilo. Lakini, kwa sababu alikuwa munyenyekevu, alifurahi pamoja nao juu ya pendeleo lenye walipata. (Hes. 11:24-29) Mufano wa Musa unatufundisha nini?

Namna gani wazee Wakristo wanaweza kuiga unyenyekevu wa Musa? (Ona fungu la 11-12) *

11. Namna gani wazee wanaweza kumuiga Musa?

11 Kama uko muzee, umekwisha kuombwa uzoeze mutu mwingine ili ashugulikie mugao fulani mu kutaniko wenye unapendaka sana? Kwa mufano, unaweza kupenda mugao wa kuongoza Funzo la Munara wa Mulinzi kila juma. Lakini, kama uko munyenyekevu kama vile Musa, hautaona kwamba hautakuwa tena mutu wa maana, ikiwa unaombwa uzoeze ndugu mwingine, mwenye atashugulikia mugao huo kisha wakati fulani. Lakini, utafurahi kusaidia ndugu yako.

12. Namna gani Wakristo wengi leo wako wanaonyesha sifa ya unyenyekevu na kutosheka?

12 Fikiria hali ingine yenye ndugu wengi wenye kuzeeka wako wanapambana nayo. Kwa miaka mingi, wamekuwa waratibu wa mabaraza ya wazee. Lakini wakati wanakuwa na miaka 80, wako tayari kuachia wengine pendeleo hilo. Waangalizi wa muzunguko wenye wanaeneza miaka 70, wanaacha kwa unyenyekevu mugao huo na wanakubali kupewa mugao mwingine wa utumishi. Na mu miaka ya hivi karibuni, Wanabeteli wengi mu dunia yote wamepewa migao ya mupya katika shamba. Ndugu na dada hao waaminifu hawasikilie kinyongo wale wenye pengine wanashugulikia sasa migao yenye walikuwa nayo.

13. Juu ya nini Paulo angesikilia wivu mitume 12 wa Yesu?

13 Mutume Paulo ni mufano mwingine muzuri wa mutu mwenye alikomalisha sifa ya unyenyekevu na kutosheka. Paulo hakuruhusu wivu ukomae mu moyo wake. Alitumika kwa bidii mu kazi ya kuhubiri, lakini alisema kwa unyenyekevu hivi: “Mimi ni mudogo zaidi kati ya mitume, na sistahili kuitwa mutume.” (1 Ko. 15:9, 10) Mitume 12 walienda pamoja na Yesu wakati wa utumishi wake hapa ku dunia, lakini ni kisha kifo cha Yesu na ufufuo wake njo Paulo alifikia kuwa Mukristo. Hata kama Paulo alifikia kuwekwa kuwa “mutume kwa mataifa,” hakupata pendeleo hilo la pekee la kuwa kati ya mitume 12 wa Yesu. (Ro. 11:13; Mdo. 1:21-26) Kuliko kusikilia wivu wale wanaume 12 na urafiki wa sana wenye walikuwa nao pamoja na Yesu, Paulo aliendelea kutosheka na mambo yenye alikuwa nayo.

14. Kama tuko wanyenyekevu na wenye kutosheka, tutafanya nini?

14 Kama tuko wanyenyekevu na wenye kutosheka, tutakuwa kama Paulo na tutaheshimia mamlaka yenye Yehova amepatia wengine. (Mdo. 21:20-26) Amefanya mupango ili wanaume wenye wamewekwa waongoze mu kutaniko la Kikristo. Hata kama hawakamilike, Yehova anawaona kuwa “zawadi katika wanadamu.” (Efe. 4:8, 11) Wakati tunaheshimia wanaume hao wenye wamewekwa na kufuata kwa unyenyekevu muongozo wenye wanatupatia, tunabakia karibu na Yehova na tunaishi kwa amani pamoja na Wakristo wenzetu.

‘FUATILIA MAMBO YENYE YANAFANYA KUKUWE AMANI’

15. Tunapaswa kufanya nini?

15 Hatuwezi kuwa na amani kama tuko tunasikiliana wivu. Tunapaswa kungoa wivu mu moyo wetu na kuepuka kupanda wivu mu mioyo ya wengine. Tunapaswa kufanya ile mambo ya lazima kama tunapenda kutii sheria ya Yehova ya ‘kufuatilia mambo yenye yanafanya kukuwe amani na mambo ya kujengana mumoja na mwingine.’ (Ro. 14:19) Tunaweza kufanya nini kabisa ili kusaidia wengine wapiganishe wivu, na tunaweza kufanya nini ili kuendeleza amani?

16. Namna gani tunaweza kusaidia wengine wapiganishe wivu?

16 Tabia yetu na matendo yetu vinaweza kuchochea wengine sana. Ulimwengu unapenda ‘tuonyeshe’ vitu vyenye tuko navyo. (1 Yo. 2:16) Lakini tabia hiyo inachochea wengine wakuwe na wivu. Tunaweza kuepuka kupanda wivu mu moyo wa wengine kama tunaepuka kuzungumuzia kila mara vitu vyenye tuko navyo ao vyenye tunapanga kuuza. Njia ingine ya kuepuka kueneza wivu ni kuwa na kiasi juu ya mapendeleo yenye tuko nayo mu kutaniko. Kama tunaendelea kuzungumuzia mapendeleo yenye tuko nayo, tunatayarisha udongo wenye mbolea ambamo wivu unaweza kukomaa. Lakini, kama tunapendezwa kabisa na watu wengine na kuona mambo ya muzuri yenye wanafanya, tunawasaidia wajisikie kuwa wenye kutosheka na tunaendeleza umoja na amani mu kutaniko.

17. Ndugu za Yosefu waliweza kufanya nini, na juu ya nini?

17 Tunaweza kushinda vita yenye tunapigana ya kuacha wivu! Fikiria tena mufano wa ndugu za Yosefu. Miaka fulani kisha kumutendea Yosefu mubaya, walikutana naye mu inchi ya Misri. Mbele ya kujitambulisha kwa ndugu zake, aliwajaribu ili kujua ikiwa walikuwa wamebadilika. Alifanya mupango ili wakule pamoja, na wakati walikuwa wanakula, alimupatia Benyamini, ndugu yake mudogo, chakula zaidi kupita wengine. (Mwa. 43:33, 34) Lakini, hakuna jambo lenye kuonyesha kama ndugu zake walimusikilia Benyamini wivu. Lakini, walionyesha kama walihangaikia kabisa ndugu yao na baba yao Yakobo. (Mwa. 44:30-34) Kwa sababu ndugu za Yosefu hawakukuwa tena na wivu, walisaidia ili kurudisha amani mu familia yao. (Mwa. 45:4, 15) Vilevile, kama tunaondoa kabisa mizizi ya wivu mu moyo wetu, tutasaidia ili familia yetu na kutaniko letu viendelee kuwa na amani.

18. Kulingana na Yakobo 3:17, 18, tutapata matokeo gani kama tunasaidia kufanya hali zenye amani?

18 Yehova anapenda tupiganishe wivu na tufuatilie amani. Tunapaswa kujikaza sana ili kufanya ile mambo mbili. Kama vile tumeona katika habari hii, tuko na mwelekeo wa kuwa na wivu. (Yak. 4:5) Na tunazungukwa na ulimwengu wenye unachochea watu wakuwe na wivu. Lakini, kama tunakomalisha sifa ya unyenyekevu, kutosheka, na kuwa wenye shukrani, wivu hautakuwa na nafasi. Tutasaidia kufanya hali zenye amani ambamo tunda la haki linaweza kukomaa.​—Soma Yakobo 3:17, 18.

WIMBO 130 Uwe Mwenye Kusamehe

^ fu. 5 Tengenezo la Yehova ni lenye amani. Lakini, tunaweza kuvuruga amani hiyo kama tunaanza kusikilia wengine wivu. Katika habari hii, tutazungumuzia mambo yenye kuleta wivu. Pia, tutazungumuzia namna ya kupiganisha tabia hiyo ya mubaya na namna ya kuendeleza amani.

^ fu. 2 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Kama vile Biblia inaonyesha, wivu hauwezi tu kuchochea mutu atamani vitu vya wengine lakini pia unaweza kufanya asipende wakuwe na vitu hivyo.

^ fu. 61 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati wa mukutano wa baraza la wazee, ndugu mwenye kuzeeka mwenye anaongozaka Funzo la Munara wa Mulinzi mu kutaniko anaombwa azoeze muzee kijana ili ashugulikie mugao huo. Hata kama ndugu mwenye kuzeeka anapenda mugao wake, anaunga mukono kwa moyo wote uamuzi wa wazee kwa kumupatia ndugu kijana mashauri yenye kufaa na anamushukuru kwa moyo wake wote.