Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu ya Maswali ya Biblia

Majibu ya Maswali ya Biblia

Je, unaweza kuelewa Biblia?

Biblia ni Neno la Mungu. Ni kama barua kutoka kwa baba mwenye upendo. (2 Timotheo 3:16) Katika Biblia, Mungu anatueleza jinsi tunavyoweza kumpendeza, kwa nini anaruhusu uovu uendelee, na mambo atakayowafanyia wanadamu wakati ujao. Lakini walimu wa dini wamepindua mafundisho ya Biblia; hivyo watu wengi wanaona kwamba hawawezi kuielewa.—Matendo 20:29, 30.

Yehova Mungu anataka tujue ukweli kumhusu. Kwa hiyo, ametupatia kitabu tunachoweza kukielewa.—Soma 1 Timotheo 2:3, 4.

Unawezaje kuelewa Biblia?

Mbali na kutupatia Biblia, Yehova anatupatia msaada wa kuielewa. Alimtuma Yesu ili atufundishe. (Luka 4:16-21) Yesu aliwasaidia wasikilizaji wake kuyaelewa Maandiko, na alirejezea mistari mbalimbali.—Soma Luka 24:27, 32, 45.

Yesu alianzisha kutaniko la Kikristo ili kuendeleza kazi aliyoanzisha. (Mathayo 28:19, 20) Leo, wafuasi wa kweli wa Yesu huwasaidia watu kuelewa yale ambayo Biblia inafundisha kumhusu Mungu. Ikiwa ungependa kuelewa Biblia, Mashahidi wa Yehova wako tayari kukusaidia.—Soma Matendo 8:30, 31.