Majibu ya Maswali ya Biblia
Je, unaweza kuelewa Biblia?
Biblia ni Neno la Mungu. Ni kama barua kutoka kwa baba mwenye upendo. (2 Timotheo 3:16) Katika Biblia, Mungu anatueleza jinsi tunavyoweza kumpendeza, kwa nini anaruhusu uovu uendelee, na mambo atakayowafanyia wanadamu wakati ujao. Lakini walimu wa dini wamepindua mafundisho ya Biblia; hivyo watu wengi wanaona kwamba hawawezi kuielewa.—Matendo 20:29, 30.
Yehova Mungu anataka tujue ukweli kumhusu. Kwa hiyo, ametupatia kitabu tunachoweza kukielewa.—Soma 1 Timotheo 2:3, 4.
Unawezaje kuelewa Biblia?
Mbali na kutupatia Biblia, Yehova anatupatia msaada wa kuielewa. Alimtuma Yesu ili atufundishe. (Luka 4:16-21) Yesu aliwasaidia wasikilizaji wake kuyaelewa Maandiko, na alirejezea mistari mbalimbali.—Soma Luka 24:27, 32, 45.
Yesu alianzisha kutaniko la Kikristo ili kuendeleza kazi aliyoanzisha. (Mathayo 28:19, 20) Leo, wafuasi wa kweli wa Yesu huwasaidia watu kuelewa yale ambayo Biblia inafundisha kumhusu Mungu. Ikiwa ungependa kuelewa Biblia, Mashahidi wa Yehova wako tayari kukusaidia.—Soma Matendo 8:30, 31.