Methali 1:1-33

1  Methali+ za Sulemani+ mwana wa Daudi,+ mfalme wa Israeli,+  ili mtu ajue hekima+ na nidhamu,+ na kutambua maneno ya uelewaji,+  apokee nidhamu+ ambayo humpa mtu ufahamu,+ uadilifu+ na haki+ na unyoofu,+  kuwapa werevu wale wasio na uzoefu,+ kumpa kijana ujuzi+ na uwezo wa kufikiri.+  Mtu mwenye hekima atasikiliza na kupata mafundisho zaidi,+ naye mtu mwenye uelewaji ndiye anayepata mwongozo stadi,+  ili kuelewa methali na mafumbo,+ maneno ya watu wenye hekima+ na vitendawili vyao.+  Kumwogopa Yehova ndio mwanzo wa ujuzi.+ Wapumbavu wamedharau hekima na nidhamu.+  Mwanangu, sikiliza nidhamu ya baba yako,+ wala usiiache sheria ya mama yako.+  Kwa maana hizo ni shada lenye kuvutia kichwani pako+ na mkufu bora shingoni pako.+ 10  Mwanangu, watenda-dhambi wakijaribu kukushawishi, usikubali.+ 11  Wakizidi kusema: “Haya, njoo pamoja nasi. Na tuvizie ili kumwaga damu.+ Na tujifiche ili kuwashambulia, bila sababu, watu wasio na hatia.+ 12  Na tuwameze wakiwa hai+ kama Kaburi,*+ naam, wakiwa wazima, kama wale wanaoshuka shimoni.+ 13  Na tupate namna zote za vitu vyenye thamani.+ Na tujaze nyara katika nyumba zetu.+ 14  Unapaswa kupiga kura yako katikati yetu. Nasi sote tuwe na mfuko mmoja tu”+ 15  mwanangu, usiende njiani pamoja nao.+ Zuia mguu wako usiende katika barabara yao.+ 16  Maana miguu yao hukimbilia ubaya mtupu,+ nao huharakisha kwenda kumwaga damu.+ 17  Kwa maana wavu hutandikwa pasipo kusudi mbele ya macho ya kiumbe chochote chenye mabawa.+ 18  Basi wao wenyewe huwavizia ili kumwaga damu yao;+ hujificha ili wazishambulie nafsi zao.+ 19  Hayo ndiyo mapito ya kila mtu anayepata faida isiyo ya haki.+ Huiondoa nafsi yao walio nayo.+ 20  Hekima ya kweli+ huendelea kulia kwa sauti kubwa barabarani.+ Hutoa sauti yake katika viwanja vya watu wote.+ 21  Inaita penye mwisho wa upande wa juu wa barabara yenye kelele.+ Husema maneno yake katika mahali pa kuingilia malango ya jiji:+ 22  “Ninyi msio na uzoefu mtaendelea mpaka wakati gani kupenda kutokuwa na ujuzi?+ Nanyi wenye dhihaka mtaendelea mpaka wakati gani kujitakia dhihaka tupu?+ Nanyi wajinga mtaendelea mpaka wakati gani kuchukia ujuzi?+ 23  Geukeni mpate karipio langu.+ Ndipo mimi nitafanya roho yangu ibubujike juu yenu;+ nitawajulisha maneno yangu.+ 24  Kwa sababu nimewaita lakini mnaendelea kukataa.+ Nimenyoosha mkono wangu lakini hakuna yeyote anayetazama.+ 25  Nanyi mnazidi kupuuza mashauri yangu yote,+ wala hamkukubali karipio langu.+ 26  Mimi pia, kwa upande wangu, nitacheka taabu yenu wenyewe,+ na jambo mnalohofu litakapokuja nitafanya mzaha,+ 27  jambo mnalohofu litakapokuja kama dhoruba, na taabu yenu wenyewe itakapofika kama upepo wa dhoruba,+ na shida na nyakati ngumu zitakapowapata.+ 28  Wakati huo wataendelea kuniita, lakini sitaitika;+ wataendelea kunitafuta, lakini hawatanipata,+ 29  kwa sababu walichukia ujuzi,+ nao hawakuchagua kumwogopa Yehova.+ 30  Hawakukubali shauri langu;+ walipuuza makaripio yangu yote.+ 31  Basi watakula matunda ya njia yao,+ nao watashiba mashauri yao wenyewe.+ 32  Kwa maana uasi+ wa wasio na uzoefu utawaua wao,+ na kutojali kwa wajinga kutawaangamiza wao.+ 33  Kwa habari yake mtu anayenisikiliza, yeye atakaa salama+ wala hatasumbuliwa na hofu ya msiba.”+

Maelezo ya Chini

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.