Methali 4:1-27
4 Enyi wana, sikilizeni nidhamu ya baba+ na kutega sikio, ili mpate kujua uelewaji.+
2 Kwa maana hakika nitawapa ninyi mafundisho mema.+ Sheria yangu msiiache.+
3 Kwa maana nilikuwa mwana halisi kwa baba yangu,+ mchanga na wa pekee kwa mama yangu.+
4 Naye baba alikuwa akinifundisha+ na kuniambia: “Moyo+ wako upate kushika sana maneno yangu.+ Shika amri zangu, uendelee kuishi.+
5 Jipatie hekima,+ jipatie uelewaji.+ Usisahau, wala usiache maneno ya kinywa changu.+
6 Usiiache, nayo itakutunza. Ipende, nayo itakulinda.
7 Hekima ndilo jambo kuu. Jipatie hekima;+ na pamoja na vyote unavyojipatia, jipatie uelewaji.+
8 Iheshimu sana, nayo itakuinua. Itakutukuza+ kwa sababu unaikumbatia.+
9 Itakuvika shada lenye kuvutia kichwani pako;+ na kukuvika taji lenye kupendeza.”+
10 Mwanangu, sikia maneno yangu na kuyakubali.+ Ndipo miaka ya maisha yako itakuwa mingi.+
11 Nitakufundisha katika njia ya hekima;+ nitakufanya utembee katika mapito ya unyoofu.+
12 Unapotembea, mwendo wako hautasongwa;+ na ukikimbia, hutajikwaa.+
13 Shika nidhamu;+ usiiache.+ Ilinde, kwa maana hiyo ndiyo uzima wako.+
14 Usiingie katika pito la waovu,+ wala usitembee na kuingia moja kwa moja katika njia ya wabaya.+
15 Iepuke,+ usiipite;+ geuka mbali nayo, nawe uende zako.+
16 Kwa maana hawalali wasipotenda jambo baya,+ nao hawapati usingizi wasipomkwaza mtu.+
17 Kwa maana wamekula mkate wa uovu,+ nao hunywa divai ya matendo ya jeuri.+
18 Lakini njia ya waadilifu ni kama nuru inayong’aa, inayozidi kuongezeka mpaka mchana mkamilifu.+
19 Njia ya waovu ni kama giza;+ hawajui ni nini kinachoendelea kuwakwaza.+
20 Mwanangu, sikiliza kwa makini maneno yangu.+ Tega sikio lako kwa maneno yangu.+
21 Na yasiondoke machoni pako.+ Yaweke katikati ya moyo wako.+
22 Kwa maana ni uzima kwa wale wanaoyapata+ na afya kwa mwili wao wote.+
23 Linda moyo wako kuliko vitu vingine vyote vinavyopaswa kulindwa,+ kwa maana ndiko zinakotoka chemchemi za uzima.+
24 Ujiepushe na maneno yaliyopotoka;+ na hila ya midomo uiweke mbali nawe.+
25 Macho yako yatazame mbele moja kwa moja,+ naam, macho yako yenye kung’aa yanapaswa kutazama mbele yako moja kwa moja.+
26 Lainisha mapito ya mguu wako,+ nazo njia zako zote na zifanywe imara.+
27 Usielekee mkono wa kuume wala wa kushoto.+ Ondoa mguu wako kutoka katika jambo baya.+

