Methali 29:1-27

29  Mtu anayekaripiwa+ tena na tena lakini anayeifanya shingo yake kuwa ngumu+ atavunjika ghafula, na hivyo pasipo kuponywa.+  Waadilifu wanapokuwa wengi, watu hushangilia;+ lakini mtu yeyote mwovu anapotawala, watu huugua.+  Mtu anayependa hekima humfanya baba yake ashangilie,+ lakini yeye anayeshirikiana na makahaba huharibu vitu vyenye thamani.+  Mfalme hufanya nchi iendelee kusimama kupitia haki,+ lakini mtu anayekula rushwa huibomoa.+  Mwanamume anayembembeleza rafiki yake+ anatandika wavu kwa ajili ya hatua zake.+  Katika kosa la mtu mbaya kuna mtego,+ lakini mwadilifu hupaaza sauti kwa shangwe na kufurahi.+  Mwadilifu anajua malalamiko halali ya watu wa hali ya chini.+ Aliye mwovu haufikirii ujuzi huo.+  Watu wenye maneno ya kujisifu huwasha mji+ moto, lakini wenye hekima hugeuzia mbali hasira.+  Mtu mwenye hekima akiisha kuingia katika hukumu pamoja na mtu mpumbavu—amesisimuka na pia amecheka, na hapana pumziko.+ 10  Watu wenye kiu ya damu humchukia yeyote asiye na lawama;+ nao wanyoofu, huendelea kuitafuta nafsi ya kila mmoja.+ 11  Mtu mjinga huiachilia roho yake yote, lakini mwenye hekima huituliza mpaka mwisho.+ 12  Mahali ambapo mtawala anasikiliza maneno ya uwongo, wote wanaomhudumia watakuwa waovu.+ 13  Maskini na mtu mwenye kukandamiza wamekutana;+ lakini Yehova anayatia nuru macho yao wote wawili.+ 14  Mfalme anapohukumu watu wa hali ya chini kwa ukweli,+ kiti chake cha ufalme kitafanywa imara kwa wakati wote.+ 15  Fimbo na karipio ndivyo hutia hekima;+ lakini mvulana aliyeachiliwa atamletea mama yake aibu.+ 16  Waovu wanapokuwa wengi, makosa huwa tele; lakini waadilifu watatazama anguko lao.+ 17  Mtie adabu mwana wako naye atakupumzisha na kukupa raha nyingi nafsini mwako.+ 18  Mahali pasipo na maono watu hujiachilia,+ lakini wenye furaha ni wale wanaoishika sheria.+ 19  Mtumishi hatakubali kurekebishwa kwa maneno tu,+ kwa maana anaelewa lakini hajali.+ 20  Je, umemwona mtu mwenye haraka kwa maneno yake?+ Kuna tumaini zaidi kwa mjinga kuliko kwake.+ 21  Mtu akimbembeleza mtumishi wake tangu ujanani, katika maisha yake ya baadaye hata atakuwa mtu asiye na shukrani. 22  Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi,+ na mtu yeyote mwenye mwelekeo wa ghadhabu ana makosa mengi.+ 23  Majivuno ya mtu wa udongo yatamshusha,+ lakini yeye aliye na roho ya unyenyekevu atapata utukufu.+ 24  Anayeshirikiana na mwizi anachukia nafsi yake mwenyewe.+ Huenda akasikia kiapo chenye laana, lakini asitoe habari yoyote.+ 25  Kutetemeshwa na wanadamu ndiko huleta mtego,+ lakini yeye anayemtegemea Yehova atalindwa.+ 26  Ni wengi wanaoutafuta uso wa mtawala,+ lakini hukumu ya mtu hutoka kwa Yehova.+ 27  Mtu asiyetenda kwa haki ni chukizo kwa waadilifu,+ na mtu mnyoofu katika njia yake ni chukizo kwa mwovu.+

Maelezo ya Chini