Luka 1:1-80

1  Kwa kuwa wengi wamechukua daraka la kukusanya habari za mambo ya hakika+ tunayosadiki kikamili kati yetu,  sawa na vile wale ambao tangu mwanzo+ walikuwa mashahidi wa kujionea+ na watumishi wa ujumbe+ walivyotuletea haya,  mimi pia niliazimia, kwa sababu nimefuata kwa uangalifu mambo yote tangu mwanzo kwa usahihi, kukuandikia hayo kwa utaratibu wenye kufuatana,+ mtukufu+ Theofilo,+  ili upate kujua kabisa uhakika wa mambo ambayo umefundishwa kwa mdomo.+  Katika siku za Herode,+ mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani aliyeitwa Zekaria wa mgawanyo wa Abiya,+ naye alikuwa na mke kutoka kwa binti za Haruni,+ na jina lake lilikuwa Elisabeti.  Wote wawili walikuwa waadilifu+ mbele za Mungu kwa sababu ya kutembea bila lawama+ kulingana na amri+ zote na matakwa ya kisheria+ ya Yehova.+  Lakini hawakuwa na mtoto, kwa sababu Elisabeti alikuwa tasa,+ nao wote wawili walikuwa wamesonga sana katika miaka.  Basi alipokuwa akitenda akiwa kuhani katika mgawo wa mgawanyo+ wake mbele za Mungu,  kulingana na desturi ya cheo cha kikuhani ikawa zamu yake kutoa uvumba+ alipoingia katika patakatifu pa Yehova;+ 10  na umati wote wa watu ulikuwa ukisali nje katika saa hiyo ya kutoa uvumba.+ 11  Malaika wa Yehova akamtokea, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya uvumba.+ 12  Lakini Zekaria akataabishwa na jambo hilo aliloona, na woga ukamwingia.+ 13  Hata hivyo, malaika akamwambia: “Usiogope, Zekaria, kwa sababu dua yako imekubaliwa,+ na mke wako Elisabeti atamzaa mwana wako, nawe utamwita jina lake Yohana.+ 14  Nawe utakuwa na shangwe na furaha kubwa, na wengi watashangilia+ kuzaliwa kwake; 15  kwa maana atakuwa mkuu mbele za Yehova.+ Lakini asinywe divai na kileo hata kidogo,+ naye atajazwa roho takatifu akiwa katika tumbo la uzazi la mama yake;+ 16  naye atawarudisha wengi wa wana wa Israeli kwa Yehova+ Mungu wao. 17  Pia, atakwenda mbele zake kwa roho na nguvu za Eliya,+ ili kurudisha mioyo+ ya akina baba kwa watoto na wale wasiotii kwenye hekima inayotumika ya waadilifu, ili kuweka tayari kwa ajili ya Yehova+ watu waliotayarishwa.”+ 18  Naye Zekaria akamwambia malaika: “Nitakuwaje na uhakika juu ya jambo hili? Kwa maana nina umri mkubwa+ na mke wangu amesonga sana katika miaka.” 19  Malaika akamjibu akamwambia: “Mimi ni Gabrieli,+ anayesimama karibu mbele za Mungu, nami nilitumwa kusema+ na wewe na kukutangazia habari njema ya mambo hayo. 20  Lakini, tazama! utakuwa kimya+ nawe hutaweza kusema mpaka siku ambayo mambo hayo yatatendeka, kwa sababu hukuamini maneno yangu, ambayo yatatimizwa katika wakati wake uliowekwa.” 21  Wakati huohuo watu wakaendelea kumngoja Zekaria,+ nao wakaanza kustaajabia kukawia kwake katika patakatifu. 22  Lakini alipotoka hakuweza kusema nao, nao wakafahamu kwamba alikuwa ameona maono yanayozidi nguvu za asili+ ndani ya patakatifu; naye akawa anawatolea ishara, lakini akaendelea kuwa bubu. 23  Basi, siku za utumishi wake wa watu wote zilipotimia,+ akaenda nyumbani kwake. 24  Lakini baada ya siku hizo Elisabeti mke wake akapata mimba;+ naye akajitenga kwa miezi mitano, akisema: 25  “Hivi ndivyo Yehova ameshughulika nami siku hizi wakati amenipa uangalifu wake ili kuondolea mbali shutuma yangu katikati ya watu.”+ 26  Katika mwezi wake wa sita malaika Gabrieli+ alitumwa kutoka kwa Mungu mpaka jiji moja la Galilaya linaloitwa Nazareti, 27  kwa bikira aliyechumbiwa na mwanamume anayeitwa Yosefu wa nyumba ya Daudi; na jina la bikira+ huyo lilikuwa Maria.+ 28  Na Gabrieli alipoingia mbele yake akasema: “Siku njema,+ uliyependelewa sana, Yehova+ yuko pamoja nawe.”+ 29  Lakini Maria akashtushwa sana na maneno hayo na kuanza kuwaza hiyo ingeweza kuwa ni salamu ya namna gani. 30  Kwa hiyo malaika akamwambia: “Usiogope, Maria, kwa maana umepata kibali+ cha Mungu; 31  na, tazama! utachukua mimba katika tumbo lako la uzazi na kuzaa mwana,+ nawe utamwita jina lake Yesu.+ 32  Huyo atakuwa mkuu+ naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi;+ na Yehova Mungu atampa kiti cha ufalme+ cha Daudi baba yake,+ 33  naye atatawala akiwa mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.”+ 34  Lakini Maria akamwambia malaika: “Hilo litawezekanaje, kwa kuwa silali+ na mwanamume?” 35  Malaika akamjibu akamwambia: “Roho takatifu+ itakuja juu yako, na nguvu za Aliye Juu Zaidi zitakufunika. Kwa sababu hiyo pia kile kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu,+ Mwana wa Mungu.+ 36  Na, tazama! Elisabeti mtu wa jamaa yako, yeye pia amechukua mimba ya mwana, katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye ambaye huitwa mwanamke tasa;+ 37  kwa sababu kwa Mungu hakuna tangazo lolote lisilowezekana.”+ 38  Ndipo Maria akasema: “Tazama! Kijakazi+ wa Yehova! Na itendeke kwangu kulingana na tangazo lako.” Ndipo malaika akaondoka. 39  Basi Maria akaondoka katika siku hizo akaenda haraka katika nchi yenye milima, mpaka jiji moja la Yuda, 40  naye akaingia nyumbani mwa Zekaria akamsalimu Elisabeti. 41  Basi, Elisabeti aliposikia salamu za Maria, yule mtoto mchanga katika tumbo lake la uzazi akaruka; na Elisabeti akajazwa roho takatifu, 42  naye akapaaza sauti kubwa na kusema: “Wewe ni mbarikiwa kati ya wanawake, na uzao wa tumbo lako la uzazi umebarikiwa!+ 43  Basi imewezekanaje nikapata pendeleo hili, kwamba mama ya Bwana+ wangu aje kwangu? 44  Kwa maana, tazama! Niliposikia salamu zako, mtoto katika tumbo langu la uzazi aliruka kwa furaha kubwa.+ 45  Mwenye furaha pia ni yule aliyeamini, kwa sababu kutakuwa utimizo kamili+ wa mambo aliyoambiwa kutoka kwa Yehova.”+ 46  Naye Maria akasema: “Nafsi yangu inamtukuza Yehova,+ 47  na roho yangu haiwezi kuacha kumfurahia+ Mungu Mwokozi+ wangu; 48  kwa sababu ametazama hali ya chini ya kijakazi+ wake. Kwa maana, tazama! tangu sasa na kuendelea vizazi vyote vitanitangaza kuwa mwenye furaha;+ 49  kwa sababu Mwenye nguvu amenitendea makuu, nalo jina lake ni takatifu;+ 50  na kwa vizazi baada ya vizazi rehema yake iko juu ya wale wanaomwogopa.+ 51  Ametenda kwa nguvu kwa mkono wake,+ amewatawanya kotekote wale wenye majivuno katika kusudi la mioyo yao.+ 52  Amewashusha watu wenye nguvu+ kutoka katika viti vya ufalme na kuwainua watu wa hali ya chini;+ 53  amewashibisha kabisa wenye njaa kwa vitu vyema+ na wale waliokuwa na mali amewaacha waende mikono mitupu.+ 54  Amekuja kumsaidia Israeli mtumishi wake,+ kukumbuka rehema,+ 55  sawa na vile alivyowaambia mababu zetu, Abrahamu na uzao wake, milele.”+ 56  Maria akakaa pamoja naye kwa karibu miezi mitatu, akarudi nyumbani kwake. 57  Sasa wakati ukafika wa Elisabeti kuzaa, naye akazaa mwana. 58  Nao majirani na watu wa jamaa yake wakasikia kwamba Yehova alikuwa ameitukuza rehema+ yake kwake, nao wakaanza kushangilia+ pamoja naye. 59  Na katika siku ya nane wakaja kumtahiri huyo mtoto mchanga,+ nao walitaka kumwita kwa jina la baba yake, Zekaria. 60  Lakini mama yake akajibu akasema: “Sivyo hata kidogo! bali ataitwa Yohana.” 61  Ndipo wakamwambia: “Hakuna yeyote kati ya watu wa jamaa yako anayeitwa kwa jina hilo.” 62  Ndipo wakaanza kumuuliza baba yake kwa ishara jina ambalo alitaka aitwe. 63  Naye akaomba bamba na kuandika: “Yohana+ ndilo jina lake.” Ndipo wote wakastaajabu. 64  Kinywa chake kikafunguka+ mara moja na ulimi wake ukalegea naye akaanza kuongea, akimbariki Mungu. 65  Na wale wote waliokuwa wakiishi katika ujirani wao wakaingiwa na woga; na katika nchi yote ya milima ya Yudea mambo yote hayo yakaanza kuzungumzwa pande zote, 66  na wote waliosikia wakaliweka mioyoni+ mwao, wakisema: “Kwa kweli mtoto huyu mchanga atakuwa wa namna gani?” Kwa maana kwa kweli mkono+ wa Yehova ulikuwa pamoja naye. 67  Na Zekaria baba yake akajazwa roho takatifu,+ naye akatoa unabii,+ akisema: 68  “Na abarikiwe Yehova Mungu wa Israeli,+ kwa sababu ameelekeza uangalifu wake na kufanya ukombozi+ kuelekea watu wake.+ 69  Naye ametuinulia pembe+ ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake, 70  sawa na vile, kupitia kinywa cha manabii wake watakatifu tangu zamani za kale,+ amesema 71  juu ya wokovu kutoka kwa adui zetu na kutoka katika mkono wa wale wote wanaotuchukia;+ 72  kufanya rehema kuhusiana na mababu zetu na kulikumbuka agano lake takatifu,+ 73  kiapo ambacho alimwapia Abrahamu babu yetu,+ 74  kutupa sisi, baada ya kuokolewa kutoka katika mikono ya adui,+ pendeleo la kumtolea utumishi mtakatifu bila woga+ 75  kwa ushikamanifu na uadilifu mbele zake siku zetu zote.+ 76  Na wewe, mtoto mchanga, utaitwa nabii wa Aliye Juu Zaidi, kwa maana utakwenda mbele za Yehova ili kutayarisha njia zake,+ 77  kuwapa watu wake ujuzi wa wokovu kwa msamaha wa dhambi zao,+ 78  kwa sababu ya huruma nyororo za Mungu wetu. Kwa huruma hizo tutapata pambazuko+ kutoka juu,+ 79  kuwapa nuru wale wanaokaa katika giza na katika kivuli+ cha kifo, kuelekeza kwa mafanikio miguu yetu katika njia ya amani.” 80  Na huyo mtoto mchanga akaendelea kukua+ na kupata nguvu katika roho, naye akakaa katika majangwa mpaka siku ya kujionyesha waziwazi kwa Israeli.

Maelezo ya Chini