Luka 21:1-38
21 Sasa alipotazama juu aliwaona matajiri wakitumbukiza zawadi zao ndani ya masanduku ya hazina.+
2 Ndipo akaona mjane fulani mwenye uhitaji akitumbukiza humo sarafu ndogo mbili za thamani ndogo sana,+
3 naye akasema: “Ninawaambia ninyi kwa kweli, Mjane huyu, ijapokuwa ni maskini, ametumbukiza ndani zaidi kuliko hao wote.+
4 Kwa maana wote hawa walitumbukiza zawadi kutokana na ziada yao, lakini mwanamke huyu kutokana na uhitaji wake alitumbukiza ndani riziki yote aliyokuwa nayo.”+
5 Baadaye, watu fulani walipokuwa wakisema kuhusu hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe mazuri na vitu vilivyowekwa wakfu,+
6 akasema: “Vitu hivi ambavyo ninyi mnaviona, siku zitakuja ambapo hakuna jiwe litakaloachwa hapa juu ya jiwe nalo lisiangushwe chini.”+
7 Ndipo wakamuuliza, wakisema: “Mwalimu, kwa kweli mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakayokuwa ishara ya wakati ambapo mambo hayo yatatukia?”+
8 Akasema: “Jihadharini msipotoshwe;+ kwa maana wengi watakuja kwa msingi wa jina langu, wakisema, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati unaofaa umekaribia.’+ Msiwafuate.
9 Zaidi ya hayo, wakati mnaposikia juu ya vita na machafuko, msiogope.+ Kwa maana mambo hayo lazima yatukie kwanza, lakini ule mwisho hautatokea mara moja.”
10 Ndipo akaendelea kuwaambia: “Taifa litasimama kupigana na taifa,+ na ufalme kupigana na ufalme;+
11 na kutakuwa na matetemeko makubwa ya nchi, na katika mahali pamoja baada ya pengine kutakuwa na tauni na upungufu wa chakula;+ kutakuwa na mambo yenye kuogopesha na ishara kubwa kutoka mbinguni.+
12 “Lakini kabla ya mambo yote hayo watu watawakamata na kuwatesa,+ wakiwakabidhi ninyi kwenye masinagogi na magereza, mkikokotwa na kupelekwa mbele ya wafalme na magavana kwa ajili ya jina langu.+
13 Utakuwa ushahidi kwenu.+
14 Kwa hiyo azimieni mioyoni mwenu kwamba hamtafanya mazoezi mapema ya jinsi mtakavyojitetea,+
15 kwa maana nitawapa ninyi kinywa na hekima, ambayo wapinzani wenu wote wakiwa pamoja hawataweza kushindana nayo wala kubisha.+
16 Zaidi ya hayo, mtatolewa hata na wazazi+ na ndugu na jamaa zenu na rafiki zenu, nao watafanya wengine kati yenu wauawe;+
17 nanyi mtachukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu.+
18 Na bado hata unywele+ mmoja wa vichwa vyenu hautaangamia.
19 Nanyi kwa kuvumilia mtajipatia nafsi zenu.+
20 “Zaidi ya hayo, mtakapoona Yerusalemu limezingirwa+ na majeshi yaliyopiga kambi, ndipo jueni kwamba kufanywa ukiwa kwake kumekaribia.+
21 Ndipo wale walio katika Yudea waanze kukimbilia milimani, na wale walio katikati yake na waondoke, nao wale walio katika sehemu za mashambani wasiingie ndani;+
22 kwa sababu hizi ni siku za kupatiliza haki, ili mambo yote yaliyoandikwa yatimizwe.+
23 Ole wao wanawake wenye mimba na wale wanaonyonyesha mtoto mchanga katika siku hizo!+ Kwa maana kutakuwa na uhitaji mkubwa juu ya nchi na ghadhabu juu ya watu hawa;
24 nao wataanguka kwa makali ya upanga na watapelekwa mateka katika mataifa yote;+ na Yerusalemu litakanyagwa-kanyagwa na mataifa, mpaka nyakati zilizowekwa+ za mataifa zitimie.
25 “Pia, kutakuwa na ishara katika jua+ na mwezi na nyota, na juu ya dunia maumivu makali ya mataifa, bila kujua njia ya kutokea kwa sababu ya kunguruma kwa bahari+ na msukosuko+ wake,
26 huku watu wakizimia kwa woga+ na tarajio la mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa;+ kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.+
27 Na ndipo watakapomwona Mwana wa binadamu+ akija katika wingu akiwa na nguvu na utukufu mwingi.+
28 Lakini mambo haya yanapoanza kutukia, simameni wima na kuinua vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu unakaribia.”
29 Ndipo akawaambia mfano: “Angalieni mtini na miti mingine yote:+
30 Wakati inapokuwa tayari imechipuka, kwa kuangalia mnajua wenyewe kwamba sasa kiangazi kiko karibu.+
31 Vivyo hivyo ninyi pia, wakati mnapoona mambo hayo yakitukia, jueni kwamba ufalme wa Mungu uko karibu.+
32 Kwa kweli nawaambia ninyi, Kizazi hiki hakitapitilia mbali kamwe mpaka mambo yote yatukie.+
33 Mbingu na dunia zitapitilia mbali,+ lakini maneno yangu hayatapitilia mbali kamwe.+
34 “Lakini jiangalieni ninyi wenyewe kwamba mioyo yenu isilemewe kamwe na kula kupita kiasi na kunywa sana+ na mahangaiko+ ya maisha, na kwa ghafula siku hiyo iwe juu yenu mara moja+
35 kama mtego.+ Kwa maana itakuja juu ya wale wote wanaokaa juu ya uso wa dunia yote.+
36 Basi, endeleeni kukesha+ wakati wote mkiomba dua+ ili mpate kufanikiwa kuponyoka mambo yote hayo yaliyokusudiwa kutukia, na kusimama mbele ya Mwana wa binadamu.”+
37 Kwa hiyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha katika hekalu,+ lakini wakati wa usiku alikuwa akitoka kwenda na kukaa juu ya mlima unaoitwa Mlima wa Mizeituni.+
38 Na watu wote+ walikuwa wakimjia asubuhi katika hekalu ili wamsikie.

