Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia

Furahia kusoma hadithi 116 kutoka kwenye Biblia. Ni hadithi za kweli, rahisi kueleweka, na zimesimuliwa kwa njia inayopendeza.

Utangulizi

Hadithi za kweli kutoka katika Biblia, kitabu kikubwa zaidi ulimwenguni, zinatoa historia ya ulimwengu kuanzia uumbaji na kuendelea.

HADITHI YA 1

Mungu Aanza Kufanyiza Vitu

Hadithi ya uumbaji ya kitabu cha Mwanzo inaeleweka na kuwagusa moyo—hata watoto wadogo.

HADITHI YA 2

Bustani Nzuri

Kulingana na kitabu cha Mwanzo, Mungu alitengeneza bustani ya Edeni kuwa mahali pa kipekee. Mungu anataka dunia yote iwe kama tu bustani ile nzuri.

HADITHI YA 3

Mwanamume na Mwanamke wa Kwanza

Mungu alimuumba Adamu na Hawa na kuwaweka katika bustani ya Edeni. Walikuwa wenzi wa kwanza wa ndoa.

HADITHI YA 4

Sababu Walipoteza Makao Yao

Kitabu cha Biblia cha Mwanzo kinatueleza jinsi paradiso ilivyopotezwa.

HADITHI YA 5

Maisha ya Taabu Yanaanza

Nje ya bustani ya Edeni, Adamu na Hawa walipata taabu nyingi. Laiti wangemsikiliza Mungu, maisha yangekuwa ya furaha kwao na kwa watoto wao pia.

HADITHI YA 6

Mwana Mzuri na Mbaya

Hadithi ya Kaini na Abeli, iliyoandikwa katika Mwanzo, inatufundisha tunapaswa kuwa watu wa namna gani na pia mitazamo tunayopaswa kubadili kabla haijawa kuchelewa mno.

HADITHI YA 7

Mtu Hodari

Mfano wa Henoko unaonyesha kwamba unaweza kufanya yaliyo mema hata ikiwa watu wanaokuzunguka wanafanya yaliyo mabaya.

HADITHI YA 8

Watu Wakubwa Mno Duniani

Mwanzo sura ya 6 inasimulia kuhusu watu wakubwa mno ambao waliwaumiza watu. Watu hao ambao waliitwa Wanefili, walikuwa watoto wa malaika waliotoka mbinguni na wakajivika miili ya kibinadamu.

HADITHI YA 9

Nuhu Anajenga Safina

Nuhu na familia yake waliokoka Gharika kwa sababu walimsikiliza Mungu ingawa wengine hawakumsikiliza Mungu.

HADITHI YA 10

Gharika Kuu

Watu walicheka Nuhu alipowaambia ujumbe wa hukumu. Lakini hawakucheka maji ya gharika yaliposhuka kutoka mbinguni! Jifunze jinsi safina ya Nuhu ilimwokoa Nuhu, familia yake na wanyama wengi.

HADITHI YA 11

Upinde wa Mvua wa Kwanza

Unapoona upinde wa mvua, unapaswa kukumbuka nini?

HADITHI YA 12

Watu Wanajenga Mnara Mkubwa

Mungu hakupendezwa, na adhabu aliyotoa bado huwaathiri wanadamu hadi leo.

HADITHI YA 13

Ibrahimu​—Rafiki ya Mungu

Kwa nini Ibrahimu aliacha makao yake ya starehe na kuanza kuishi katika mahema?

HADITHI YA 14

Mungu Anajaribu Imani ya Ibrahimu

Kwa nini Mungu alimwomba Ibrahimu amtoe mwana wake Isaka kuwa dhabihu?

HADITHI YA  15

Mke wa Lutu Alitazama Nyuma

Kile alichofanya kinatufundisha somo muhimu.

HADITHI YA 16

Isaka Anapata Mke Mzuri

Ni nini kilichofanya Rebeka awe mke mzuri? Je, ni urembo au ni jambo lingine?

HADITHI YA 17

Mapacha Waliokuwa Tofauti

Baba yao, Isaka, alimpenda sana Esau, lakini mama yao Rebeka, alimpenda sana Yakobo.

HADITHI 18

Yakobo Anakwenda Harani

Yakobo alimwoa Lea kwanza ingawa alimpenda sana Raheli.

HADITHI YA 19

Yakobo Ana Jamaa Kubwa

Je, majina ya makabila 12 ya Israeli yalitokana na wana 12 wa Yakobo?

HADITHI YA 20

Dina Anaingia Katika Taabu

Yote yalisababishwa na kuchagua marafiki wasiofaa.

HADITHI YA 21

Yusufu Anachukiwa na Ndugu Zake

Ni nini kiliwachochea baadhi yao watake kumuua ndugu yao?

HADITHI YA 22

Yusufu Anawekwa Katika Gereza

Afungwa gerezani, si kwa sababu alivunja sheria, lakini kwa sababu alifanya yaliyo sawa.

HADITHI YA 23

Ndoto za Farao

Kuna ufanani kati ya ng’ombe saba na masuke saba ya nafaka.

HADITHI YA 24

Yusufu Anajaribu Ndugu Zake

Atajuaje ikiwa wamebadilika tangu walipomuuza kama mtumwa?

HADITHI YA 25

Jamaa Inahamia Misri

Kwa nini familia ya Yakobo inaitwa Waisraeli na si Wayakobo?

HADITHI YA 26

Ayubu ni Mwaminifu kwa Mungu

Ayubu alipoteza mali, afya, na watoto. Je, Mungu alikuwa akimwadhibu?

HADITHI YA  27

Mfalme Mbaya Anatawala Misri

Kwa nini aliamuru watu wake wawaue watoto wote wa kiume wa Waisraeli?

HADITHI YA  28

Namna Mtoto Musa Alivyookolewa

Mama yake alitafuta njia ya kukwepa amri iliyoamuru watoto wavulana wa Waisraeli wauawe.

HADITHI YA  29

Sababu Musa Alikimbia

Musa alifikiria kwamba alikuwa tayari kuwaokoa Waisraeli alipokuwa na umri wa miaka 40, lakini hakuwa tayari.

HADITHI YA  30

Mti Mdogo Unaowaka

Kwa kutumia mfuatano wa miujiza, Mungu anamwambia Musa muda umefika wa Musa kuwaongoza Waisraeli kutoka Misri.

HADITHI YA 31

Musa na Haruni Wanamwona Farao

Kwa nini Farao hamsikilizi Musa na kuwaachilia Waisraeli?

HADITHI YA 32

Mapigo 10

Mungu alileta mapigo kumi kwa sababu Farao, mtawala wa Misri kwa kiburi aliwakataza Waisraeli wasiondoke.

HADITHI YA 33

Kuvuka Bahari Nyekundu

Musa atenganisha Bahari Nyekundu kwa nguvu za Mungu na Waisraeli wavuka na kwenda nchi kavu.

HADITHI 34

Aina Mpya ya Chakula

Chakula hiki cha pekee kinatoka mbinguni.

HADITHI 35

Yehova Anatoa Sheria Zake

Ni sheria gani mbili ambazo ni kuu kuliko zile Amri Kumi?

HADITHI 36

Ndama ya Dhahabu

Kwa nini watu waliabudu mfano uliotengenezwa kwa hereni zilizoyeyushwa?

HADITHI 37

Hema ya Ibada

Sanduku la agano lilikuwa katika chumba cha ndani.

HADITHI 38

Wapelelezi 12

Wapelelezi kumi wanasema jambo moja, na wawili jambo tofauti. Waisraeli wanawaamini nani?

HADITHI 39

Fimbo ya Haruni Inamea Maua

Inawezekanaje maua yamee kwenye fimbo kwa usiku mmoja?

HADITHI 40

Musa Anaupiga Mwamba

Musa anapata matokeo mazuri, lakini alimkasirisha Yehova.

HADITHI 41

Nyoka wa Shaba

Kwa nini Mungu aliwatuma nyoka wenye sumu wawaume Waisraeli?

HADITHI 42

Punda Anasema

Punda anaona kitu ambacho Balaamu haoni.

HADITHI 43

Yoshua Anakuwa Kiongozi

Musa bado ana nguvu, hivyo kwa nini Yoshua anakuwa kiongozi?

HADITHI 44

Rahabu Anaficha Wapelelezi

Rahabu aliwasaidiaje wanaume wawili, naye wafanye nini?

HADITHI 45

Kuvuka Mto Yordani

Muujiza unatokea makuhani wanapokanyaga maji.

HADITHI 46

Kuta za Yeriko

Kamba inazuiaje ukuta usianguke?

HADITHI 47

Mwivi Katika Israeli

Je, mtu mmoja mbaya anaweza kusababisha matatizo kwa taifa zima?

HADITHI YA 48

Wagibeoni Wenye Hekima

Walimdanganya Yoshua na Waisraeli ili wawape ahadi, hata hivyo Waisraeli walitimiza ahadi yao.

HADITHI YA 49

Jua Linasimama Tu

Yehova anamfanyia Yoshua jambo ambalo hakuwahi kufanya na hajawahi kufanya tena tangu wakati huo.

HADITHI 50

Wanawake Hodari Wawili

Baraki anaongoza jeshi la Waisraeli vitani, hivyo kwa nini Yaeli anasifiwa?

HADITHI 51

Ruthu na Naomi

Ruthu anaacha kwao ili aishi na Naomi na kumtumikia Yehova.

HADITHI 52

Gideoni na Wanaume Wake 300

Mungu alichagua jeshi hili dogo kwa njia isiyo ya kawaida.

HADITHI 53

Ahadi ya Yeftha

Ahadi yake kwa Yehova iliathiri si yeye tu bali binti yake pia.

HADITHI 54

Mwanamume Mwenye Nguvu Kuliko Wote

Delila alijuaje siri ya nguvu za Samsoni?

HADITHI 55

Mvulana Mdogo Anamtumikia Mungu

Mungu anamtuma Samweli kumwambia Kuhani Mkuu Eli ujumbe mzito.

HADITHI 56

Sauli​—Mfalme wa Kwanza wa Israeli

Mungu alimchagua na kisha akamkataa, tunaweza kujifunza somo muhimu kutoka kwa Sauli.

HADITHI 57

Mungu Anamchagua Daudi

Mungu aliona nini katika Daudi ambacho Samweli hakuona?

HADITHI 58

Daudi na Goliathi

Daudi alimpiga Sauli, si kwa kombeo lake tu bali kwa silaha yenye nguvu zaidi.

HADITHI 59

Sababu Yampasa Daudi Akimbie

Sauli alimpenda Daudi mwanzoni, lakini baadaye alimwonea wivu akataka kumuua. Kwa nini?

HADITHI 60

Abigaili na Daudi

Abigaili asema kwamba mume wake ni mpumbavu, hata hivyo hilo linaokoa uhai wa mume wake kwa muda mfupi.

HADITHI 61

Daudi Anafanywa Mfalme

Daudi anathibitisha kwamba anastahili kuwa mfalme wa Israeli kwa yale anayofanya na anayokataa kufanya.

HADITHI 62

Matata Katika Nyumba ya Daudi

Kwa kosa moja, Daudi anajiletea yeye na familia yake matatizo kwa miaka mingi.

HADITHI YA 63

Sulemani Mfalme Mwenye Akili

Je kweli angemkata mtoto vipande viwili?

HADITHI YA 64

Sulemani Anajenga Hekalu

Licha ya kuwa na hekima nyingi, Sulemani alishawishiwa kufanya jambo la kipumbavu na lenye kosa.

HADITHI YA 65

Ufalme Unagawanywa

Mara tu Yeroboamu alipoanza kutawala, aliwaongoza watu kuvunja amri za Mungu.

HADITHI YA 66

Yezebeli - Malkia Mbaya Sana

Angetumia njia yoyote ile ili apate anachotaka.

HADITHI YA 67

Yehoshafati Anamtumaini Yehova

Kwa nini jeshi lingeenda kwenye pambano likiwa na waimbaji wasio na silaha wakiongoza njia?

HADITHI YA 68

Wavulana Wawili Wanaokuwa Hai Tena

Je mtu aliyekufa anaweza kuwa hai tena? Imewahi kutokea!

HADITHI YA 69

Msichana Anamsaidia Mwanamume Mwenye Nguvu

Alikuwa na ujasiri wa kusema, na matokeo yake yalikuwa ni muujiza.

HADITHI YA 70

Yona na Samaki Mkubwa

Yona alijifunza somo muhimu kuhusu kutii maagizo ya Yehova.

HADITHI YA 71

Mungu Anatoa Ahadi ya Paradiso

Paradiso ya kwanza ilikuwa ndogo; paradiso hii itaijaza dunia yote.

HADITHI YA 72

Mungu Anamsaidia Mfalme Hezekia

Katika usiku mmoja, malaika aua wanajeshi 185,000 wa Ashuru.

HADITHI YA 73

Mfalme Mzuri wa Mwisho wa Israeli

Akiwa tineja, Yosia alitenda kijasiri.

HADITHI YA 74

Mwanamume Asiyeogopa

Yeremia alifikiri alikuwa mdogo sana kuwa nabii, lakini Mungu alijua kwamba angeweza kuwa nabii.

HADITHI YA 75

Wavulana Wanne Babeli

Walifanikiwa licha ya kuwa mbali na familia zao.

HADITHI YA 76

Yerusalemu Unaharibiwa

Kwa nini Mungu aliwaruhusu maadui wa Israeli, Wababeli, waharibu Yerusalemu?

HADITHI YA 77

Walikataa Kuabudu

Je, Mungu atawaokoa vijana hawa watatu waliomtii kutoka katika tanuru ya moto?

HADITHI YA 78

Mwandiko wa Mkono Ukutani

Nabii Danieli akifafafanua maneno manne ya kifumbo.

HADITHI YA 79

Danieli Katika Shimo la Simba

Danieli alihukumiwa adhabu ya kifo, lakini je, angeweza kuiepuka?

HADITHI YA 80

Watu wa Mungu Wanatoka Babeli

Mfalme Koreshi wa Uajemi alitimiza unabii mmoja alipoteka Babiloni, na sasa anatimiza unabii mwingine.

HADITHI YA 81

Kuutumainia Msaada wa Mungu

Waisraeli wavunja amri za wanadamu ili kumtii Mungu. Je Mungu atawabariki?

HADITHI YA 82

Mordekai na Esta

Malkia Vashti alikuwa mrembo, lakini Mfalme Ahasuero alimchagua Esta kama malkia wake mpya. Kwa nini?

HADITHI YA 83

Kuta za Yerusalemu

Wakijenga upya kuta, wafanya-kazi walipaswa kuweka panga na mikuki yao tayari usiku na mchana.

HADITHI YA 84

Malaika Anatembelea Mariamu

Analeta ujumbe kutoka kwa Mungu: Mariamu atapata mtoto ambaye atakuwa mfalme milele.

HADITHI YA 85

Yesu Anazaliwa Katika Boma la Ng’ombe

Kwa nini mfalme anayekuja azaliwe mahali ambapo wanyama wanalishiwa?

HADITHI YA 86

Wanaume Walioongozwa na Nyota

Ni nani aliyewaongoza mamajusi kwa Yesu? Jibu linaweza kukushangaza.

HADITHI YA 87

Kijana Yesu Katika Hekalu

Ana mambo ambayo yanawashangaza hata watu wazima wanaofundisha katika hekalu.

HADITHI YA 88

Yohana Anambatiza Yesu

Yohana amekuwa akiwabatiza watenda dhambi, lakini Yesu hajatenda dhambi kamwe. Kwa nini Yohana alimbatiza?

HADITHI YA 89

Yesu Anasafisha Hekalu

Yesu anaonyesha aina ya upendo ambao unamsukuma kuwa na hasira.

HADITHI YA 90

Pamoja na Mwanamke Penye Kisima

Maji ambayo Yesu atampa yatawezaje kumfanya asione kiu tena kamwe?

HADITHI YA 91

Yesu Anafundisha Juu ya Mlima

|Jifunze hekima isiyopitwa na wakati kutoka katika Mahubiri ya Mlimani ya Yesu.

HADITHI YA 92

Yesu Anafufua Wafu

Kwa kutumia nguvu za Mungu, Yesu alisema maneno mawili rahisi na kumfufua binti ya Yairo.

HADITHI YA 93

Yesu Analisha Watu Wengi Chakula

Kwa kuwalisha maelfu ya watu kimuujiza, Yesu alithibitisha jambo gani muhimu?

HADITHI YA 94

Anapenda Watoto Wadogo

Yesu aliwafundisha mitume kwamba wana mengi ya kujifunza si tu kuhusu watoto wadogo bali pia kutoka kwa watoto wadogo.

HADITHI YA 95

Namna Yesu Anavyofundisha

Mfano wa Yesu wa jirani Msamaria ni mmoja kati ya mifano mingi inayoonyesha njia yake ya kufundisha aliyoitumia kwa ukawaida.

HADITHI YA 96

Yesu Anaponya Wagonjwa

Yesu anatimiza nini kupitia miujiza yote anayofanya?

HADITHI YA 97

Yesu Aja Kama Mfalme

Umati mkubwa unamkaribisha Yesu, lakini si wote wanaofurahishwa na jambo hilo.

HADITHI YA 98

Juu ya Mlima wa Mizeituni

Yesu aliwaambia mitume wake wanne mambo ambayo yanatukia katika siku zetu.

HADITHI YA 99

Katika Chumba cha Juu

Kwa nini Yesu anawaambia mitume wake waadhimishe mlo huu wa pekee kila mwaka?

HADITHI YA 100

Yesu Katika Bustani

Kwa nini Yuda alimsaliti Yesu kwa kumbusu?

HADITHI YA 101

Yesu Anauawa

Akiwa ametundikwa juu ya mti wa mateso, Yesu alitoa ahadi kuhusu paradiso.

HADITHI YA 102

Yesu Yuko Hai

Baada ya malaika kuliviringisha jiwe kutoka katika kaburi la Yesu, askari waliokuwa wakilinda walishtushwa na kile walichoona ndani ya kaburi.

HADITHI YA 103

Ndani ya Chumba Kilichofungwa

Kwa nini wanafunzi wake hawakumtambua baada Yesu ya kufufuliwa?

HADITHI YA 104

Yesu Anarudi Mbinguni

Kabla Yesu hajapaa angani, anawapa wanafunzi wake amri moja ya mwisho.

HADITHI YA 105

Kungojea Yerusalemu

Kwa nini Yesu aliwamwagia wanafunzi wake roho takatifu katika siku ya Pentekoste?

HADITHI YA 106

Wanafunguliwa Katika Gereza

Viongozi wa kidini Wayahudi wanawaweka mitume gerezani ili kusimamisha kazi yao ya kuhubiri, lakini Mungu ana mpango mwingine tofauti.

HADITHI YA 107

Stefano Anapigwa kwa Mawe

Alipokuwa akiuawa, Stefano alitoa sala ya pekee sana.

HADITHI YA 108

Wakienda Damasko

Mwangaza unaopofusha na sauti kutoka mbinguni vyabadili maisha ya Sauli.

HADITHI YA 109

Petro Anamtembelea Kornelio

Je Mungu anawaona watu kutoka jamii au taifa moja kuwa bora kuliko wale wa jamii au mataifa mengine?

HADITHI YA 110

Timotheo—Msaidizi Mpya wa Paulo

Timotheo anaondoka nyumbani na kujiunga na Paulo katika safari yenye kusisimua ya kuhubiri.

HADITHI YA 111

Mvulana Aliyelala Usingizi

Eutiko analala usingizi wakati wa hotuba ya kwanza ya Paulo, lakini si wakati wa hotuba ya pili. Kilichotukia katikati ya hotuba hizo ni, muujiza.

HADITHI YA 112

Meli Inaharibika Katika Kisiwa

Mara tu inapoonekana hakuna tumaini, Paulo anapokea ujumbe kutoka kwa Mungu unaompa matumaini.

HADITHI YA 113

Paulo Katika Roma

Paulo angewezaje kufanya kazi yake kama mtume huku akiwa mfungwa?

HADITHI YA 114

Mwisho wa Mabaya Yote

Kwa nini Mungu analituma jeshi lake likiongozwa na Yesu katika vita vya Har—Magedoni?

HADITHI YA 115

Paradiso Mpya Duniani

Wakati fulani watu waliishi katika Paradiso, hilo litatukia tena.

HADITHI YA 116

Tunavyoweza Kuishi Milele

Je inatosha kumjua Yehova na Yesu? Ikiwa sivyo, ni nini kingine kinachohitajiwa?

Maswali ya Funzo Katika Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia

SMaandiko na maswali ya funzo yameandaliwa ili kuwasaidia vijana wafaidike zaidi kutokana na kila hadithi ya Biblia.