Habari Njema Kutoka kwa Mungu!

Kuna habari gani njema kutoka kwa Mungu? Kwa nini tuamini habari hizo? Broshua hii inajibu maswali ya Biblia yanayoulizwa na watu wengi.

Jinsi Unavyoweza Kufaidika na Broshua Hii

Broshua hii itakusaidia ufurahie kujifunza moja kwa moja kutoka katika Neno la Mungu, Biblia. Ona jinsi unavyoweza kutumia Biblia yako kupata maandiko yaliyorejelewa.

SOMO 1

Habari Njema Ni Nini?

Jifunze uone kuna habari gani kutoka kwa Mungu, kwa nini habari hizo ni muhimu leo, na kile unachopaswa kufanya.

SOMO 2

Mungu Ni Nani?

Je, Mungu ana jina na je, anatujali?

SOMO 3

Je, Kweli Habari Njema Imetoka kwa Mungu?

Tunawezaje kuwa na uhakika kwamba ujumbe wa Biblia ni wa kweli?

SOMO 4

Yesu Kristo Ni Nani?

Soma ujue kwa nini Yesu alikufa, fidia ni nini, na kile ambacho Yesu anafanya sasa.

SOMO 5

Mungu Ana Kusudi Gani Kuelekea Dunia?

Biblia inaelezea kwa nini Mungu aliiumba dunia, kuteseka kutaisha lini, na hali ya dunia na wakaaji wake itakavyokuwa wakati ujao.

SOMO 6

Kuna Tumaini Gani kwa Wafu?

Ni nini hutokea tunapokufa? Je, tutakuja kuwaona tena wapendwa wetu waliokufa?

SOMO 7

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Mfalme wa Ufalme wa Mungu ni nani, na Ufalme huo utatimiza nini?

SOMO 8

Kwa Nini Mungu Anaruhusu Uovu na Kuteseka?

Uovu ulianzaje, na kwa nini Mungu ameruhusu uendelee kuwepo? Je, kweli kuteseka kutaisha?

SOMO 9

Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha

Yehova, Mungu mwenye furaha, anataka familia ziwe na furaha. Soma uone ushauri mzuri wa Biblia kwa waume, wake, wazazi, na watoto.

SOMO 10

Unawezaje Kuitambua Ibada ya Kweli?

Je, kuna dini moja tu ya kweli? Chunguza mambo matano yanayoitambulisha ibada ya kweli.

SOMO 11

Kanuni za Biblia Zinatunufaishaje?

Yesu alifafanua kwa nini tunahitaji mwongozo na kutaja kanuni mbili za Biblia ambazo ni muhimu zaidi.

SOMO 12

Unaweza Kumkaribia Mungu Jinsi Gani?

Chunguza uone ikiwa Mungu husikiliza sala zote, jinsi ya kusali, na mambo mengine ya kufanya ili tumkaribie Mungu.

SOMO 13

Kuna Habari Gani Kuhusu Dini?

Je, kweli wakati utafika ambapo watu wote wataungana kumtumikia Mungu wa kweli?

SOMO 14

Kwa Nini Mungu Ana Kikundi au Tengenezo la Watu Wanaomwabudu?

Biblia inatueleza kwa nini Wakristo wa kweli wamepangwa kitengenezo na jinsi walivyopangwa.

SOMO 15

Kwa Nini Uendelee Kujifunza Kuhusu Habari Njema?

Ujuzi wako kumhusu Mungu na Neno lake unaweza kuwanufaishaje wengine? Unaweza kufurahia uhusiano wa gani na Mungu?