Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umefurahia kusoma matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona kama unaweza kujibu maswali yafuatayo:

• Ni nini kinachoweza kumsaidia Mkristo wa kweli mpendwa wake anapomwacha Yehova?

Ni kujiimarisha yeye mwenyewe kiroho na kuwaimarisha watu wengine wa familia ambao ni waaminifu. Kujishughulisha na mambo ya kiroho. Kuwa tayari kuwasaidia wengine. Kuendelea kutumaini kwamba mpendwa huyo atarudi. Kutojilaumu. Kuheshimu mpango wa Yehova wa nidhamu, na kuwaeleza marafiki jinsi unavyohisi.—9/1, ukurasa wa 18-21.

• Maandiko yanatusaidia kutambua “siku za mwisho” kwa njia gani mbili?

Biblia ilitabiri mambo ambayo yangetukia wakati wa “umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 24:3, 7, 8; Luka 21:11) Ilitabiri pia mabadiliko ya mitazamo na matendo ya watu wa “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1-5) Jambo lingine muhimu ni kwamba habari njema ya ufalme ingehubiriwa katika siku za mwisho.—9/15, ukurasa wa 4-6.

• Kutaniko lina daraka gani ikiwa Mkristo anayeendesha gari anahusika katika msiba wa barabarani unaosababisha kifo cha watu wengine?

Wazee wanaochunguza kisa hicho wanaweza kuamua kwamba Mkristo huyo hana hatia ya damu kwa sababu hangeweza kuzuia hali zilizosababisha msiba huo. Lakini ikithibitishwa kwamba ana hatia ya damu, naye akitubu, atapewa karipio la Kimaandiko linalofaa na hatakubaliwa kuwa na mapendeleo kutanikoni.—9/15, ukurasa wa 30.

• Kwa nini uzima wa milele hautegemei maendeleo ya kisayansi?

Kuna jitihada zinazofanywa katika nyanja za uchunguzi wa kisayansi ili kuongeza urefu wa maisha. Zinatia ndani majaribio ya kufanya chembe za mwili ziendelee kujitokeza bila kukoma au ya kupandikiza wagonjwa viungo vipya vinavyofaana nao. Lakini Biblia inaonyesha kwamba dhabihu ya Yesu ndiyo njia pekee ya kuwawezesha wanadamu kupata uzima wa milele.—10/1, ukurasa wa 3-5.

• Je, ubatizo wa Kikristo ulitokana na zoea la Wayahudi la kuoga kidesturi?

Hapana. Wayahudi walijitakasa wao wenyewe kidesturi, lakini katika ubatizo wa Yohana, haikuwa hivyo. Chini ya Sheria ya Musa, mtu alihitajiwa kujitakasa tena na tena, lakini ubatizo wa Kikristo unafanywa mara moja tu.—10/15, ukurasa wa 12-13.

• Shule ya Mazoezi ya Kihuduma ni nini?

Ni mafunzo ya majuma manane kwa ajili ya wazee na watumishi wa huduma waseja ambao wanaweza kuombwa wakatumikie mahali penye uhitaji mkubwa. Wanaweza kuombwa watumikie katika kutaniko walikotoka, katika eneo lingine nchini mwao, au katika nchi nyingine.—11/15, ukurasa wa 10-11.

• Mpinga-Kristo anayetajwa katika 1 Yohana 2:18; 4:3 ni nani?

Katika maana pana, “mpinga-Kristo” anatia ndani watu wote wanaompinga Kristo au wanaodai kwa uwongo kuwa Kristo au wawakilishi wake. Maneno ya Yesu na ya Yohana yanaonyesha kwamba mpinga-Kristo ni jamii ya watu mmoja-mmoja ambao ni wapinga-Kristo wanaoeneza uwongo wa kidini na kuupinga Ufalme wa Mungu.—12/1, ukurasa wa 4-6.