Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Mawasiliano Nimeona ni lazima niandike kuhusu mfululizo wa makala “Mawasiliano Ni Muhimu kwa Uhai.” (Septemba 22, 2003) Makala hizo zilifafanua jambo ambalo viumbe hufanya kwa kawaida, yaani, kusaidiana. Hata mimea huonya mimea mingine kunapokuwa na hatari! Litakuwa jambo lenye kupendeza wakati wanadamu watakapojifunza kusaidiana.

C. C., Marekani

Nilifurahia maelezo yenu kuhusu jinsi wanyama wanavyowasiliana. Ni lazima tukubali kwamba kuna Mungu ambaye alianzisha mambo hayo yote yenye kustaajabisha.

R. Z., Ujerumani

Sijui nitaelezaje furaha niliyopata niliposoma makala hizo. Ni pendeleo kubwa sana kuweza kuwasiliana na Mungu!

A. W., Afrika Kusini

Nilikuwa nimeshuka moyo nilipoanza kusoma makala hiyo asubuhi ya leo. Lakini ile sehemu iliyozungumzia jinsi wadudu wanavyowasiliana ilinichekesha. Nilienda kazini nikitabasamu.

L. L., Ufaransa

Alama za Chanjo Asanteni sana kwa makala “Vijana Huuliza . . . Je, Nitiwe Alama ya Chanjo?” (Septemba 22, 2003) Nilifikiri kwamba alama za chanjo zinapendeza na nilitaka kujibandika alama ya chanjo inayoweza kutoka. Hata hivyo, taarifa iliyosema kwamba hatungetaka kujitia alama mwilini mwetu ambazo zinamshushia Mungu heshima “hata kama ni kwa muda mfupi tu” ilinifanya nifikiri. Nilipowazia kwamba kujitia alama ya chanjo kutawakwaza wengine na kuwafanya wanione kuwa mwasi, niliamua kutofanya hivyo.

A. K., Japani

Nilitaka sana kuwa na alama ya chanjo. Lakini makala hiyo ilinisaidia nitambue kwamba huenda nikajuta baadaye. Pia mlitaja hatari za afya ambazo sikuwa nimefikiria. Asanteni kwa makala hiyo yenye kusadikisha.

D. T., Ufaransa

Piñata Nilifurahia kusoma makala “Desturi ya Kale ya Piñata.” (Septemba 22, 2003) Baada ya kuisoma, nilipata maswali fulani. Uhusiano wa desturi hiyo na dini za uwongo umethibitishwa kabisa. Lakini makala hiyo ilielekea kuonyesha kwamba desturi hiyo ni sawa maadamu haisumbui dhamiri ya mtu. Vipi juu ya siku za kuzaliwa na sikukuu kama Krismasi?

S. W., Marekani

“Amkeni!” linajibu: Wakristo huepuka sherehe au desturi zozote zinazoendelea kuhusisha imani ya dini za uwongo au shughuli zinazovunja kanuni za Biblia. Kwa mfano, Biblia huonyesha waziwazi kwamba sherehe za siku za kuzaliwa hazifai. (Mwanzo 40:20; Mathayo 14:6-10) Hata hivyo, ikiwa ni wazi kabisa kwamba desturi fulani haihusiani na dini za uwongo wala haivunji kanuni za Biblia, kila Mkristo anapaswa kujiamulia ikiwa atafuata desturi hiyo au la.

Simulizi la Mwanasayansi Asanteni sana kwa makala nzuri sana yenye kichwa “Dini Yangu Ilikuwa Sayansi.” (Septemba 22, 2003) Kenneth Tanaka hakuogopa kukubali mambo ya kweli. Pia, alikubali kwa unyenyekevu kwamba mambo aliyokuwa ameamini kwa miaka mingi hayakuwa ya kweli. Ana mwelekeo unaofaa.

S. A., Urusi

Nimeshuka moyo kwa muda fulani, nikipambana na hisia za kutaka kufa. Kisha nikasoma swali hili katika makala iliyomzungumzia Kenneth Tanaka, “Ikiwa ulimwengu utakoma hatimaye, basi maisha yana kusudi gani?” Jambo hilo liligusa moyo wangu. Ni kana kwamba Mungu alikuwa akiniambia, “Endelea kuishi!”

C. I., Japani