Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Zinaeleza Mengi Sana”

“Zinaeleza Mengi Sana”

“Zinaeleza Mengi Sana”

MAELEZO hayo kuhusu picha zinazopatikana katika vitabu na magazeti ya Mashahidi wa Yehova, yalitolewa kwenye maonyesho ya kimataifa ya sanaa huko Kassel, Ujerumani. Katja, mwenye umri wa miaka 16, anaeleza yaliyotukia wakati yeye na wanafunzi wenzake walipotembelea maonyesho hayo na kutazama baadhi ya sanaa za kidini:

“Yule aliyetutembeza aliwauliza wanafunzi ikiwa wamewahi kuchunguza magazeti ya Mashahidi wa Yehova. Wote waliposema hawajawahi, alianza kusifu picha za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Alisema kwamba picha hizo huchorwa vizuri na kuchaguliwa vizuri, na kwamba ‘zinaeleza mengi sana.’

“Alituambia kwamba inafaa kuchunguza kwa makini picha hizo zenye kupendeza,” akisema kwamba zinaonyesha matukio ya Biblia kwa njia inayotusaidia kuelewa haraka jinsi yanavyohusiana na wakati wetu. Kisha akawasihi wanafunzi wakubali kuchukua magazeti hayo wanapopewa, akisema kwamba hawapaswi kutazama picha tu bali pia kusoma makala zenye kuarifu na za kupendeza.