Mika 3:1-12
3 Nami nikasema: “Tafadhali sikieni, ninyi vichwa vya Yakobo na ninyi viongozi wa nyumba ya Israeli.+ Je, si wajibu wenu kujua haki?+
2 Ninyi mnaochukia yaliyo mema+ na mnaopenda ubaya,+ mnaochuna ngozi kutoka kwa watu na nyama kutoka kwa mifupa yao;+
3 ninyi ambao pia mmekula nyama ya watu wangu,+ na mmeichuna ngozi yao kutoka kwao, mkaivunja vipande-vipande mifupa yao, na kuiponda vipande-vipande kama kitu kilicho katika chungu chenye mdomo mpana na kama nyama ndani ya chungu cha kupikia.+
4 Wakati huo watamwomba Yehova msaada, lakini hatawajibu.+ Naye atauficha uso wake kutoka kwao wakati huo,+ kulingana na walivyotenda ubaya kwa matendo yao.+
5 “Yehova amesema hivi juu ya manabii ambao wanawapoteza watu wangu,+ ambao wanauma kwa meno yao+ na ambao hupaaza sauti, ‘Amani!’+ ambao, mtu yeyote asipoweka kitu vinywani mwao, pia hutakasa vita juu yake,+
6 ‘Basi ninyi mtakuwa na usiku,+ kusiweko maono;+ nanyi mtakuwa na giza, ili msifanye uaguzi. Nalo jua litatua juu ya manabii, na mchana utakuwa mweusi juu yao.+
7 Waonaji+ wataona aibu,+ na waaguzi+ watakata tamaa. Nao wote watafunika masharubu,+ kwa maana hakuna jibu kutoka kwa Mungu.’ ”+
8 Nami nimejaa nguvu, kwa roho ya Yehova, na ya haki na uwezo,+ ili nimwambie Yakobo maasi yake na Israeli dhambi yake.+
9 Tafadhali sikieni hili, ninyi vichwa vya nyumba ya Yakobo nanyi viongozi wa nyumba ya Israeli,+ mnaochukia haki na mnaopotoa hata kila kitu ambacho kimenyooka;+
10 mnaojenga Sayuni kwa matendo ya umwagaji wa damu na Yerusalemu kwa ukosefu wa uadilifu.+
11 Walio vichwa vyake hutoa hukumu ili wale rushwa+ tu, na makuhani wake hufundisha ili tu wapate malipo,+ na manabii wake hufanya uaguzi ili tu wapate pesa;+ hata hivyo wao huendelea kujiegemeza kwa Yehova, wakisema: “Je, Yehova hayuko katikati yetu?+ Hakuna msiba utakaotupata.”+
12 Basi kwa sababu yenu Sayuni utalimwa kama shamba, na Yerusalemu litakuwa marundo ya mabomoko,+ na mlima wa nyumba hiyo utakuwa kama mahali pa juu pa msitu.