Mika 4:1-13

4  Na itatukia katika siku za mwisho+ kwamba mlima+ wa nyumba+ ya Yehova utawekwa imara juu ya kilele cha milima, nao utainuliwa juu ya vilima;+ na vikundi vya watu vitamiminika huko.+  Na mataifa mengi hakika yatakwenda na kusema: “Njooni,+ twendeni juu kwenye mlima wa Yehova na kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo;+ naye atatufundisha njia zake,+ nasi tutatembea katika mapito yake.”+ Kwa maana sheria itatoka katika Sayuni, na neno la Yehova katika Yerusalemu.+  Naye hakika atafanya hukumu kati ya vikundi vingi vya watu,+ na kunyoosha mambo+ kuhusu mataifa yenye nguvu yaliyo mbali.+ Nao watafua panga zao ziwe majembe na mikuki yao iwe miundu.+ Hawatainua upanga, taifa juu ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.+  Nao wataketi, kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake,+ wala hakutakuwa na mtu yeyote anayewatetemesha;+ kwa maana kinywa cha Yehova wa majeshi kimesema hivyo.+  Kwa maana vikundi vyote vya watu vitatembea kila kimoja katika jina la mungu wake;+ bali sisi tutatembea katika jina la Yehova Mungu wetu+ mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+  “Katika siku hiyo,” asema Yehova, “nitamkusanya yeye aliyekuwa akichechemea;+ naye aliyekuwa ametawanywa nitamkusanya pamoja,+ yeye ambaye nimemtendea vibaya.  Nami nitamfanya yeye aliyekuwa akichechemea awe mabaki,+ na yeye aliyekuwa ameondolewa mbali awe taifa lenye uwezo;+ na Yehova atatawala juu yao akiwa mfalme katika Mlima Sayuni, kutoka sasa na kuendelea mpaka wakati usio na kipimo.+  “Wewe nawe, Ee mnara wa kundi, kilima cha binti Sayuni,+ mpaka kwako itakuja, ndiyo, mamlaka ya kwanza itakuja hakika,+ ufalme wa binti Yerusalemu.+  “Basi ni kwa nini unaendelea kupiga kelele?+ Je, hamna mfalme ndani yako, au je, mshauri wako mwenyewe ameangamizwa, hata maumivu kama yale ya mwanamke anayezaa yakakushika?+ 10  Ee binti Sayuni, uwe na maumivu makali na utaabike, kama mwanamke anayezaa,+ maana sasa utaenda kutoka katika mji, nawe utakaa katika shamba.+ Nawe utaenda mpaka Babiloni.+ Huko utakombolewa.+ Huko Yehova atakununua kutoka mkononi mwa adui zako.+ 11  “Na sasa mataifa mengi yatakusanywa juu yako, wale wanaosema, ‘Acheni atiwe uchafu, nayo macho yetu yautazame Sayuni.’+ 12  Lakini wao nao, hawajapata kujua fikira za Yehova, wala hawajapata kuelewa shauri lake;+ maana atawakusanya pamoja kwenye uwanja wa kupuria kama mafungu ya nafaka iliyokatwa hivi karibuni.+ 13  “Simama upure, Ee binti Sayuni;+ maana nitaibadili pembe yako iwe chuma, na kwato zako nitazibadili ziwe shaba, nawe utaponda kabisa vikundi vingi vya watu;+ na kwa kupiga marufuku utamtolea Yehova faida yao isiyo ya haki,+ na mali zao kwa Bwana wa kweli wa dunia yote.”+

Maelezo ya Chini