Mika 1:1-16
1 Neno la Yehova lililomjia Mika+ wa Moreshethi, katika siku za Yothamu,+ Ahazi,+ Hezekia,+ wafalme wa Yuda,+ ambalo aliona katika maono kuhusu Samaria+ na Yerusalemu:+
2 “Sikieni, enyi vikundi vya watu, ninyi nyote; kazeni uangalifu, Ee dunia na vyote vinavyokujaza,+ naye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova na awe shahidi juu yenu,+ Yehova katika hekalu lake takatifu.+
3 Maana, tazama! Yehova anatoka mahali pake,+ naye atashuka na kukanyaga mahali pa juu pa dunia.+
4 Na milima itayeyuka chini yake,+ na nchi tambarare za chini zitapasuka, kama nta kwa sababu ya moto,+ kama maji yanayomwagwa kwenye mteremko mkali.
5 “Ni kwa sababu ya maasi ya Yakobo kwamba kuna hayo yote, kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli.+ Maasi ya Yakobo ni nini? Je, si Samaria?+ Ni mahali gani pa juu pa Yuda?+ Je, si Yerusalemu?
6 Nami nitalifanya Samaria kuwa rundo la mabomoko ya shambani,+ mahali pa kupanda mizabibu; nami nitamwaga mawe yake katika bonde, na misingi yake nitaifunua.+
7 Na sanamu zake zote za kuchongwa zitavunjwa vipande-vipande,+ na zawadi zote alizopewa kuwa malipo yake zitateketezwa katika moto;+ na sanamu zake zote nitazifanya kuwa mahame yaliyo ukiwa. Maana alizikusanya kutoka kwa vitu vilivyotolewa kuwa malipo ya kahaba, nazo zitarudi zikiwa kitu kilichotolewa kuwa malipo ya kahaba.”+
8 Kwa sababu hiyo nitaomboleza na kupiga mayowe;+ nitatembea miguu wazi na uchi.+ Nitaomboleza kama mbwa-mwitu, na kuomboleza kama mbuni-jike.
9 Maana jeraha lililo juu yake haliwezi kupona;+ maana limefika mpaka Yuda,+ pigo hilo limefika mpaka lango la watu wangu, mpaka Yerusalemu.+
10 “Msiseme hili katika Gathi; msilie hata kidogo.+
“Katika nyumba ya Afra gaagaa mavumbini.+
11 Vuka, Ee mwanamke mkaaji wa Shafiri, katika uchi wenye aibu.+ Mwanamke mkaaji wa Saanani hajaondoka. Maombolezo ya Beth-ezeli yatawaondolea ninyi mahali pake pa kusimama.
12 Maana mwanamke mkaaji wa Marothi amengojea mema,+ lakini mabaya yameshuka kutoka kwa Yehova mpaka kwenye lango la Yerusalemu.+
13 Funga gari kwenye kikundi cha farasi, Ee mwanamke mkaaji wa Lakishi.+ Yeye alikuwa mwanzo wa dhambi kwa binti Sayuni,+ maana ndani yako maasi ya Israeli yamepatikana.+
14 Kwa hiyo utampa Moresheth-gathi zawadi za kuaga.+ Nyumba za Akzibu+ zilikuwa kama kitu chenye udanganyifu kwa wafalme wa Israeli.
15 Bado nitakuletea mnyang’anyi,+ Ee mwanamke mkaaji wa Maresha.+ Utukufu wa Israeli utakuja mpaka Adulamu.+
16 Fanya upara, unyoe nywele zako kwa sababu ya wana wa furaha yako tele.+ Panua upara wako kama ule wa tai, kwa sababu wameondoka kwako kwenda uhamishoni.”+