Mika 2:1-13

2  “Ole wao wanaopanga mambo yenye kudhuru, na wale wanaozoea kufanya lililo baya, vitandani mwao!+ Wao hulifanya kwenye nuru ya asubuhi,+ kwa sababu hilo liko katika uwezo wa mikono yao.+  Nao wametamani mashamba na kuyanyakua;+ nyumba pia, nao wamezichukua; nao wamempunja mwanamume na nyumba yake,+ mtu na fungu lake la urithi.+  “Kwa hiyo Yehova amesema hivi, ‘Tazama, nakusudia msiba+ juu ya familia hii+ ambao hamtaziondoa shingo zenu+ ndani yake, ili msitembee kwa majivuno;+ kwa sababu ni wakati wa msiba.+  Siku hiyo mtu atapaaza neno la kimethali+ kuwahusu ninyi naye ataomboleza, ndiyo, maombolezo.+ Mtu atasema: “Hakika tumeporwa!+ Anabadili fungu la watu wangu.+ Jinsi anavyoliondoa kwangu! Anawagawia wasio waaminifu mashamba yetu wenyewe.”  Kwa hiyo hutakuwa na yeyote anayetupa kamba, kwa kura,+ katika kutaniko la Yehova.  Ninyi msiache maneno yaanguke.+ Wanaacha maneno yaanguke. Hawataacha maneno yaanguke kuhusu mambo haya. Fedheha hazitaondoka.+  “ ‘Je, inasemwa, Ee nyumba ya Yakobo:+ “Roho ya Yehova imekosa kuridhika, au haya ndiyo matendo yake?”+ Je, maneno yangu mwenyewe hayafanyi mema+ kwa yeye anayetembea kwa unyoofu?+  “ ‘Na jana watu wangu mwenyewe walisimama kama adui mkaidi.+ Vueni pambo lenye utukufu kutoka mbele ya vazi, kutoka kwa wale wanaopita wakiwa na uhakika, kama wale wanaorudi kutoka vitani.  Mnawafukuza wanawake wa watu wangu kutoka katika nyumba ambamo mwanamke ana furaha tele. Mnachukua utukufu wangu+ kutoka kwa watoto wake, mpaka wakati usio na kipimo.+ 10  Ondoka uende,+ kwa sababu hapa si mahali pa kupumzika.+ Kwa sababu ya uhakika wa kwamba amekuwa asiye safi,+ kuna kuvunja-vunja; na kazi hiyo ya kuvunja-vunja ina maumivu.+ 11  Ikiwa mwanamume, anayetembea akifuata upepo na uwongo, amesema uwongo:+ “Nitakuangushia maneno kuhusu divai na kuhusu kileo,” yeye pia atakuwa yule anayewaangushia watu hawa maneno.+ 12  “ ‘Hakika nitamkusanya Yakobo, ninyi nyote;+ bila shaka nitawakusanya pamoja wanaobaki wa Israeli.+ Nitawaunganisha, kama kundi zizini, kama kundi la wanyama katikati ya malisho yake;+ huko kutakuwa na kelele za wanadamu.’+ 13  “Anayepenyeza atakuja mbele yao:+ watapenya. Nao watapita kati ya lango, nao watatoka nje kwa hilo.+ Na mfalme wao atapita kati mbele yao, Yehova akiwa mbele yao.”+

Maelezo ya Chini