Mika 2:1-13
2 “Ole wao wanaopanga mambo yenye kudhuru, na wale wanaozoea kufanya lililo baya, vitandani mwao!+ Wao hulifanya kwenye nuru ya asubuhi,+ kwa sababu hilo liko katika uwezo wa mikono yao.+
2 Nao wametamani mashamba na kuyanyakua;+ nyumba pia, nao wamezichukua; nao wamempunja mwanamume na nyumba yake,+ mtu na fungu lake la urithi.+
3 “Kwa hiyo Yehova amesema hivi, ‘Tazama, nakusudia msiba+ juu ya familia hii+ ambao hamtaziondoa shingo zenu+ ndani yake, ili msitembee kwa majivuno;+ kwa sababu ni wakati wa msiba.+
4 Siku hiyo mtu atapaaza neno la kimethali+ kuwahusu ninyi naye ataomboleza, ndiyo, maombolezo.+ Mtu atasema: “Hakika tumeporwa!+ Anabadili fungu la watu wangu.+ Jinsi anavyoliondoa kwangu! Anawagawia wasio waaminifu mashamba yetu wenyewe.”
5 Kwa hiyo hutakuwa na yeyote anayetupa kamba, kwa kura,+ katika kutaniko la Yehova.
6 Ninyi msiache maneno yaanguke.+ Wanaacha maneno yaanguke. Hawataacha maneno yaanguke kuhusu mambo haya. Fedheha hazitaondoka.+
7 “ ‘Je, inasemwa, Ee nyumba ya Yakobo:+ “Roho ya Yehova imekosa kuridhika, au haya ndiyo matendo yake?”+ Je, maneno yangu mwenyewe hayafanyi mema+ kwa yeye anayetembea kwa unyoofu?+
8 “ ‘Na jana watu wangu mwenyewe walisimama kama adui mkaidi.+ Vueni pambo lenye utukufu kutoka mbele ya vazi, kutoka kwa wale wanaopita wakiwa na uhakika, kama wale wanaorudi kutoka vitani.
9 Mnawafukuza wanawake wa watu wangu kutoka katika nyumba ambamo mwanamke ana furaha tele. Mnachukua utukufu wangu+ kutoka kwa watoto wake, mpaka wakati usio na kipimo.+
10 Ondoka uende,+ kwa sababu hapa si mahali pa kupumzika.+ Kwa sababu ya uhakika wa kwamba amekuwa asiye safi,+ kuna kuvunja-vunja; na kazi hiyo ya kuvunja-vunja ina maumivu.+
11 Ikiwa mwanamume, anayetembea akifuata upepo na uwongo, amesema uwongo:+ “Nitakuangushia maneno kuhusu divai na kuhusu kileo,” yeye pia atakuwa yule anayewaangushia watu hawa maneno.+
12 “ ‘Hakika nitamkusanya Yakobo, ninyi nyote;+ bila shaka nitawakusanya pamoja wanaobaki wa Israeli.+ Nitawaunganisha, kama kundi zizini, kama kundi la wanyama katikati ya malisho yake;+ huko kutakuwa na kelele za wanadamu.’+
13 “Anayepenyeza atakuja mbele yao:+ watapenya. Nao watapita kati ya lango, nao watatoka nje kwa hilo.+ Na mfalme wao atapita kati mbele yao, Yehova akiwa mbele yao.”+