Mika 5:1-15
5 “Wakati huu unajikatakata,+ Ee binti uliyevamiwa; yeye ametuzingira sisi.+ Watalipiga kwa fimbo shavu la mwamuzi wa Israeli.+
2 “Nawe, Ee Bethlehemu Efratha,+ wewe uliye mdogo sana kuwa kati ya maelfu ya Yuda,+ kutoka kwako+ atanijia yeye atakayekuwa mtawala katika Israeli,+ ambaye asili yake ni kutoka nyakati za kale, kutoka siku za wakati usio na kipimo.+
3 “Kwa hiyo atawatoa+ mpaka wakati ambapo yeye anayezaa anapozaa.+ Na wale ndugu zake wengine watarudi kwa wana wa Israeli.
4 “Naye atasimama na kuchunga kwa nguvu za Yehova,+ katika ukuu wa jina la Yehova Mungu wake.+ Nao wataendelea kukaa,+ maana sasa atakuwa mkuu mpaka miisho ya dunia.+
5 Na huyu atakuwa amani.+ Lakini wakati Mwashuru atakapokuja katika nchi yetu na kukanyaga juu ya minara yetu ya makao,+ sisi pia tutasimamisha juu yake wachungaji saba, ndiyo, watawala wadogo wanane kutoka kati ya wanadamu.
6 Nao wataichunga nchi ya Ashuru kwa upanga,+ na nchi ya Nimrodi+ katika malango yake. Naye atatukomboa kutoka kwa Mwashuru,+ anapokuja katika nchi yetu na anapokanyaga juu ya eneo letu.
7 “Na mabaki ya Yakobo+ watakuwa katikati ya makabila mengi ya watu kama umande kutoka kwa Yehova,+ kama manyunyu mengi ya mvua juu ya mimea,+ ambayo hayamtumaini mwanadamu wala kuwangojea wana wa mtu wa udongo.+
8 Na mabaki ya Yakobo watakuwa kati ya mataifa, katikati ya makabila mengi ya watu, kama simba katikati ya wanyama wa msituni, kama mwana-simba mwenye manyoya shingoni katikati ya makundi ya kondoo, ambaye, anapopita kati, hukanyaga-kanyaga na pia hurarua vipande-vipande;+ wala hakuna mkombozi.
9 Mkono wako utainuliwa juu ya wapinzani wako,+ na adui zako wote watakatiliwa mbali.”+
10 “Na itatukia katika siku hiyo,” asema Yehova, “kwamba nitakatilia mbali farasi zako kutoka katikati yako na kuharibu magari yako.+
11 Nami nitakatilia mbali majiji ya nchi yako na kubomoa mahali pako pote penye ngome.+
12 Nami nitakatilia mbali ulozi kutoka mkononi mwako, nawe hutaendelea tena kuwa na watu wowote wanaofanya uchawi.+
13 Nami nitakatilia mbali sanamu zako za kuchongwa na nguzo zako kutoka katikati yako, nawe hutainamia tena kazi ya mikono yako.+
14 Nami nitang’oa miti yako mitakatifu+ kutoka katikati yako na kuangamiza majiji yako.
15 Na katika hasira na ghadhabu nitalipiza kisasi juu ya mataifa ambayo hayakutii.”+