Mika 7:1-20
7 Ole wangu,+ kwa maana nimekuwa kama mkusanyo wa matunda ya wakati wa kiangazi, kama masalio ya mkusanyo wa zabibu!+ Hakuna kishada cha zabibu za kula, hakuna tini ya mapema, ambayo nafsi yangu inaweza kutamani!+
2 Mshikamanifu ameangamia kutoka duniani, na kati ya wanadamu hakuna mnyoofu.+ Wote huvizia ili kumwaga damu.+ Huwinda, kila mmoja ndugu yake mwenyewe, kwa wavu wa kukokota.+
3 Mikono yao iko juu ya lililo baya, ili kulifanya vema;+ mkuu anaomba kitu, naye mwenye kuhukumu hufanya hivyo ili kupata thawabu,+ na mkubwa anasema tamaa iliyo katika nafsi yake mwenyewe;+ nao huisokota.
4 Mtu aliye bora zaidi kwao ni kama mchongoma, aliye mnyoofu zaidi kwao ni mbaya kuliko ukuta wa miiba.+ Siku ya walinzi wako, siku yenu ya kukaziwa fikira, itakuja.+ Sasa kuhangaishwa kwao kutatokea.+
5 Msimwamini mwenzi. Msimtegemee rafiki msiri.+ Linda milango ya kinywa chako kutokana na yeye anayelala kifuani pako.+
6 Kwa maana mwana anamdharau baba, binti anasimama kumpinga mama yake;+ binti-mkwe kumpinga mama-mkwe wake;+ adui za mtu ni watu wa nyumba yake.+
7 Lakini mimi, nitaendelea kumtazamia Yehova.+ Nitaonyesha mtazamo wa kumngojea Mungu wa wokovu wangu.+ Mungu wangu atanisikia.+
8 Usishangilie juu yangu, Ee mwanamke adui yangu.+ Ijapokuwa nimeanguka, nitasimama;+ ijapokuwa ninakaa gizani,+ Yehova atakuwa nuru kwangu.+
9 Ghadhabu ya Yehova nitaivumilia—kwa maana nimemtendea dhambi+—mpaka atakapoendesha kesi yangu na kutekeleza haki kwa ajili yangu.+ Atanileta kwenye nuru; nitautazama uadilifu wake.+
10 Na adui yangu ataona, aibu itamfunika,+ yeye aliyekuwa akiniambia: “Yuko wapi, Yehova Mungu wako?”+ Macho yangu mwenyewe yatamtazama huyo mwanamke.+ Sasa atakuwa mahali pa kukanyaga-kanyaga, kama matope ya barabarani.+
11 Siku ya kujenga kuta zako za mawe, siku hiyo amri itakuwa mbali kabisa.+
12 Siku hiyo watakujia hata kutoka Ashuru na majiji ya Misri, na kutoka Misri hata kufika ule Mto;+ na kutoka bahari mpaka bahari, na kutoka mlima mpaka ule mlima.+
13 Na nchi itakuwa mahame yenye ukiwa kwa sababu ya wakaaji wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.+
14 Wachunge watu wako kwa fimbo yako,+ kundi la urithi wako, yeye aliyekuwa akikaa peke yake msituni—katikati ya shamba la matunda.+ Na walishe katika Bashani na Gileadi+ kama katika siku za zamani.+
15 “Nitamwonyesha mambo ya ajabu kama katika zile siku ulipokuwa ukitoka nchi ya Misri.+
16 Mataifa yataona na kuonea aibu uwezo wao wote.+ Wataweka mkono wao juu ya vinywa vyao;+ masikio yao yatakuwa na uziwi.
17 Wataramba mavumbi kama nyoka;+ kama watambaaji wa dunia watatoka katika maboma+ yao wakitetemeka. Watamjia Yehova Mungu wetu wakitetemeka, nao watakuogopa.”+
18 Ni nani aliye Mungu kama wewe,+ anayesamehe kosa na kuuachilia ukosaji+ wa mabaki ya urithi wake?+ Hatashikilia hasira yake milele, kwa maana yeye hupendezwa na fadhili zenye upendo.+
19 Atatuonyesha rehema tena;+ atayatiisha makosa yetu.+ Nawe utazitupa dhambi zao zote+ katika vilindi vya bahari.
20 Utatoa ukweli aliopewa Yakobo, fadhili zenye upendo alizopewa Abrahamu, ambazo uliwaapia mababu zetu tangu siku za zamani za kale.+