Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

JW LIBRARY

Tumia Alama za Kukumbuka Ukurasa​—Android

Tumia Alama za Kukumbuka Ukurasa​—Android

Kwenye JW Library kuna vialamisho, yaani, alama za kukumbuka ukurasa. Unaweza kuzitumia kukumbuka ukurasa wa chapisho lolote kama tu unaposoma kitabu kilichochapishwa. Kila chapisho kwenye JW Library lina vialamisho kumi.

Fuata maelekezo yafuatayo ili kutumia vialamisho:

 Tia Alama ya Kukumbuka Ukurasa

Unaweza kutia alama ya kukumbuka ukurasa wa makala, sura, fungu, au mstari hususa wa Biblia.

Ili kutia alama makala au sura, bofya kitufe cha Vialamisho. Orodha itafunguka inayoonyesha vialamisho vya chapisho unalosoma. Bofya sehemu moja ili kutia alama makala au sura.

Ili kutia alama fungu hususa au mstari hususa wa Biblia, bofya maandishi; kisha bofya kitufe cha Vialamisho kinachojitokeza.

 Tafuta Alama Uliyoweka

Ili upate alama uliyoweka, fungua chapisho lililo na alama hiyo ya kukumbuka ukurasa; kisha bofya kitufe cha Vialamisho. Bofya alama ya ukurasa unaotaka kusoma.

 Badili au Futa Alama Ulizoweka

Ikiwa umetia alama ukurasa fulani, unaweza kufuta alama hiyo au kuibadili na nyingine.

Ukitaka kufuta alama bofya kitufe cha Vialamisho; kisha bofya nukta tatu za Mengineyo zilizo kwenye sehemu ya alama unayotaka kufuta. Kisha bofya Ondoa.

Ili kubadili alama ya ukurasa, bofya kitufe cha Vialamisho; kisha bofya nukta tatu za Mengineyo zilizo kwenye sehemu ya alama unayotaka kubadili. Bofya Badili. Alama hiyo itabadilishwa na ya ukurasa mpya unaotaka kukumbuka. Alama hizo ni muhimu unapotaka kukumbuka umefikia wapi katika usomaji wa chapisho fulani. Kwa mfano, unaweza kutia alama ya mahali ulipofika katika usomaji wako wa Biblia.

Sehemu hizo mbalimbali zilipatikana Mei 2014 kwenye JW Library toleo la 1.2, ambalo linafanya kazi vizuri kwenye vifaa vinavyotumia mfumo wa Android 2.3 au wa karibuni zaidi. Ikiwa huoni mambo haya, tafadhali fuata mwelekezo kwenye makala “Anza Kutumia JW Library​—Android,” kwenye Pata Habari za Karibuni Zaidi.