Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Barua kutoka Baraza Linaloongoza

Barua kutoka Baraza Linaloongoza

Kwako Msomaji Unayempenda Yehova:

Yesu alisema: “Mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.” (Yohana 8:32) Maneno hayo yanatia moyo kwelikweli! Ndiyo, inawezekana kuijua kweli, hata katika hizi “siku za mwisho” zilizo hatari, ambapo uwongo umekuwa mwingi. (2 Timotheo 3:1) Je, unakumbuka mara ya kwanza ulipotambua kwamba umeipata kweli kama inavyofafanuliwa katika Neno la Mungu? Hiyo ilikuwa pindi yenye kusisimua kama nini!

Hata hivyo, ingawa ni muhimu kupata ujuzi sahihi wa kweli na kushiriki kwa ukawaida kuwaambia wengine kuihusu, ni lazima pia tujiendeshe kupatana na hiyo kweli. Ili kufanya hivyo, tunahitaji kujitunza katika upendo wa Mungu. Hilo linahusisha nini? Maneno ambayo Yesu alisema usiku kabla ya kifo chake yanajibu swali hilo. Aliwaambia mitume wake waaminifu hivi: “Mkishika amri zangu, mtakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba na kukaa katika upendo wake.”—Yohana 15:10.

Ona kwamba Yesu aliendelea kukaa katika upendo wa Mungu kwa kuzishika amri za Baba yake. Ndivyo inavyopaswa kuwa kwetu pia. Ili kukaa katika upendo wa Mungu, tunahitaji kuishi kulingana na kweli hiyo. Jioni hiyohiyo, Yesu alisema: “Ikiwa mnajua mambo haya, wenye furaha ni ninyi ikiwa mnayatenda.”—Yohana 13:17.

Tunatumaini kwamba kitabu hiki kitakusaidia kuendelea kutumia kweli maishani mwako na hivyo kujitunza mwenyewe “katika upendo wa Mungu . . . kwa kutazamia uzima wa milele.”—Yuda 21.

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova