Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Wakumbuka?

Je, Wakumbuka?

Je, Wakumbuka?

Je, umethamini kusoma makala za karibuni za Mnara wa Mlinzi? Ebu ona kama unaweza kuyajibu maswali yafuatayo:

Ni nini kilichofanya Krismasi ikubaliwe kwa urahisi nchini Korea?

Kulikuwa na imani ya kale nchini Korea na nchi nyinginezo kuhusu mungu fulani wa jikoni ambaye alidhaniwa kuwa alikuwa akija kupitia dohani na kuleta zawadi mnamo Desemba. Pia, baada ya Vita ya Ulimwengu ya Pili, wanajeshi wa Marekani walitoa zawadi na misaada katika makanisa ya huko.—12/15, ukurasa wa 4 na 5.

Kwa utimizo wa Isaya 21:8, Mungu amekuwa na “mlinzi” gani wakati wetu?

Wakristo watiwa-mafuta kwa roho, wakitumikia wakiwa jamii ya mlinzi, wamewatahadharisha watu juu ya maana ya matukio ya ulimwengu yanayotimiza unabii wa Biblia. Pia wamesaidia wanafunzi wa Biblia kutambua na kuepuka mafundisho na matendo yasiyo ya kimaandiko.—1/1, ukurasa wa 8 na 9.

“Ndugu wa Poland” walikuwa nani?

Walikuwa kikundi kidogo cha kidini katika karne ya 16 na 17 nchini Poland waliowatia watu moyo kushikamana na Biblia na hivyo kukataa mafundisho ya kanisa yaliyoenea wakati huo, kama Utatu, ubatizo wa vitoto vichanga, na moto wa helo. Baada ya muda, walinyanyaswa kikatili na kutawanywa katika nchi nyinginezo.—1/1, ukurasa wa 21-23.

Kwa nini unabii wa Biblia ndio upasao kutumainiwa badala ya matabiri ya wataalamu au wanajimu?

Wanadamu wanaojidai kuwa manabii hawategemeki kwa sababu wao humpuuza Yehova na Biblia. Ni unabii wa Biblia pekee unaoweza kukusaidia kujua jinsi matukio yanavyohusiana na kusudi la Mungu, na kukunufaisha wewe na familia yako milele.—1/15, ukurasa wa 3.

Ni zipi baadhi ya sababu zinazothibitisha kwamba twaishi katika siku za mwisho?

Twaweza kuona matokeo ya kuondolewa kwa Shetani mbinguni. (Ufunuo 12:9) Twaishi wakati wa huyo “mfalme” wa mwisho anayetajwa katika Ufunuo 17:9-11. Idadi ya Wakristo wa kweli watiwa-mafuta inapungua, lakini inaonekana kwamba baadhi yao watakuwa wangali duniani dhiki kubwa ianzapo.—1/15, ukurasa wa 12 na 13.

Kitabu cha Habakuki kiliandikwa lini, na kwa nini twapasa kupendezwa nacho?

Kitabu hiki cha Biblia kiliandikwa wapata mwaka wa 628 K.W.K. Kina hukumu ya Yehova dhidi ya Yuda la kale na dhidi ya Babiloni. Pia kina hukumu za Mungu ambazo karibuni zitaupata mfumo mwovu wa sasa.—2/1, ukurasa wa 8.

Ni wapi katika Biblia tuwezapo kupata shauri la mama lenye hekima juu ya wake wema?

Sura ya mwisho ya kitabu cha Mithali, sura ya 31, ina shauri hilo bora.—2/1, ukurasa wa 30 na 31.

Kwa nini tunaweza kuwa wenye shukrani kwamba Yehova ametufunulia “akili ya Kristo”? (1 Wakorintho 2:16)

Kupitia rekodi ya Gospeli, Yehova ametuwezesha kujifunza mawazo ya Yesu, hisia zake, utendaji wake na mambo aliyotanguliza. Hiyo yaweza kutusaidia kuwa kama Yesu zaidi, hasa kuhusu mkazo tunaotilia kazi ya kuhubiri yenye kuokoa uhai.—2/15, ukurasa wa 25.

Je, Mungu hujibu sala leo?

Ndiyo. Ingawa Biblia yaonyesha kwamba Mungu hajibu sala zote, mambo yaliyoonwa siku hizi yathibitisha kwamba mara nyingi amejibu watu ambao wamesali wapate faraja na msaada katika mambo kama vile kutatua matatizo ya ndoa.—3/1, ukurasa wa 3-7.

Tunaweza kufanya nini ili tupate nguvu za Mungu?

Tunaweza kuomba nguvu hizo kupitia sala, na kupata nguvu za kiroho kutokana na Biblia, na kuimarishwa kupitia ushirika wa Kikristo.—3/1, ukurasa wa 15 na 16.

Wazazi wanaweza kuwasaidiaje watoto wao wanufaike zaidi na mikutano ya Kikristo?

Wanaweza kuwasaidia watoto wao wasilale usingizi, labda kwa kuwafanya walale usingizi kwa muda mfupi kabla ya mikutano. Watoto wanaweza kutiwa moyo “kuandika,” kama vile kutia alama kwenye karatasi kila wakati maneno wanayoyafahamu yanapotajwa.—3/15, ukurasa wa 17 na 18.

Tunaweza kujifunza mambo yapi kutokana na mfano wa Yobu?

Yobu alitanguliza uhusiano wake pamoja na Mungu, hakuwa mwenye upendeleo aliposhughulika na wanadamu wenzake, alijitahidi kuwa mwaminifu kwa mke wake, alihangaikia hali ya kiroho ya familia yake, naye alivumilia kwa uaminifu alipojaribiwa.—3/15, ukurasa wa 25-27.

Je, Biblia ina ujumbe wa siri unaotupa ufahamu wa mambo fulani ya siri?

La. Vitabu vingine vya kilimwengu vyaweza pia kudaiwa kuwa na ujumbe unaodhaniwa kuwa wa siri. Ule udhaniwao kuwa ujumbe wa siri katika Biblia hauwezi kufaulu kwa sababu ya tofauti za mwendelezo katika hati za Kiebrania.—4/1, ukurasa wa 30 na 31.