Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umesoma kwa makini matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:

Ili waweze kuwasaidia watoto wao kiroho, kwa nini wazazi wahamiaji wanapaswa kufikiria suala la lugha?

Inaelekea watoto watajifunza lugha ya wenyeji wakiwa shuleni, au kwenye ujirani. Mtoto anaweza kunufaika kwa kujua lugha zaidi ya moja. Wazazi wanapaswa kufikiria ikiwa watashirikiana na kutaniko la lugha ya wenyeji au kutaniko linalotumia lugha yao ili watoto wao waielewe kweli vizuri na kufanya maendeleo ya kiroho. Wazazi Wakristo hutanguliza hali ya kiroho ya watoto wao kuliko mapendezi ya kibinafsi.—w17.05, uku. 9-11.

Yesu alimuuliza Petro hivi: “Je, unanipenda kuliko hawa?” Neno “hawa” lilirejelea nini? (Yoh. 21:15)

Inaelekea Yesu alikuwa akirejelea samaki waliokuwa kando yao na/au biashara ya uvuvi. Baada ya Yesu kufa, Petro alirudia kazi yake ya awali ya uvuvi. Wakristo wanapaswa kujichunguza ili waone kazi yao ya kimwili inachukua nafasi gani mioyoni mwao.—w17.05, uku. 22-23.

Kwa nini Abrahamu alimwomba mke wake aseme yeye ni dada yake? (Mwa. 12:10-13)

Ukweli ni kwamba Sara alikuwa dada nusu wa Abrahamu. Ikiwa Sara angesema Abrahamu ni mume wake, huenda Abrahamu angeuawa na hivyo hangetokeza uzao ambao Mungu alikuwa amemwahidi.—wp17.3, uku. 14-15.

Elias Hutter alibuni mbinu gani ambayo ingewasaidia watu waliotaka kujifunza Kiebrania?

Alitaka kuwasaidia wanafunzi watofautishe kati ya mizizi ya maneno katika Biblia na viambishi vingine vyovyote vilivyotumiwa. Ili kutimiza hilo, alichapisha mizizi ya maneno kwa wino uliokolezwa, na viambishi akavichapisha kwa njia ya kawaida. Mbinu hiyo imetumiwa pia katika maelezo ya chini katika Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya marejezo.—wp17.4, uku. 11-12.

Mkristo anapaswa kuzingatia mambo gani anapofikiria ikiwa atamiliki silaha kama vile bastola au bunduki ili kujilinda na wanadamu wengine?

Anapaswa kufikiria mambo kama vile: Mungu huona uhai kuwa mtakatifu. Yesu hakuwahimiza wafuasi wake wabebe panga ili kujilinda. (Luka 22:36, 38) Tunapaswa kufua panga zetu ziwe miundu. Uhai una thamani kuliko vitu vya kimwili. Tunaheshimu dhamiri za wengine, na tungependa kuwa vielelezo bora. (2 Kor. 4:2)—w17.07, uku. 31-32.

Kwa nini masimulizi ya Mathayo na Luka kuhusu maisha ya awali ya Yesu yanatofautiana?

Mathayo anazungumza zaidi kumhusu Yosefu, kama vile jinsi alivyotenda baada ya kujua kwamba Maria ana mimba na kuhusu mwongozo aliopokea kutoka kwa Mungu kwamba wakimbilie Misri na baadaye warudi. Luka anazungumza zaidi kumhusu Maria; kwa mfano, anazungumza kuhusu Maria alipomtembelea Elisabeti na jinsi alivyotenda wakati kijana Yesu alipobaki hekaluni.—w17.08, uku. 32.

Biblia imedumu licha ya mambo gani?

Maana ya maneno na misemo iliyotumiwa katika Biblia imebadilika kadiri wakati unavyopita. Mabadiliko ya kisiasa yameathiri lugha iliyotumiwa na watu wengi. Kumekuwa na vipingamizi vya kutafsiri Biblia katika lugha zinazotumiwa na watu wengi.—w17.09, uku. 19-21.

Je, una malaika anayekulinda?

Hapana. Yesu alisema kwamba wanafunzi wake wana malaika wanaoutazama uso wa Mungu. (Mt. 18:10) Alikuwa akimaanisha kwamba malaika wanamhangaikia kila mwanafunzi wake, si kwamba wanamlinda kimuujiza kila mmoja wao.—wp17.5, uku. 5.

Upendo ulio bora zaidi ni upi?

Upendo wa a·gaʹpe unapotegemea kanuni zinazofaa, ndio upendo ulio bora zaidi. Unaweza kutia ndani hisia na shauku. Lakini mtu anapoonyesha upendo huo, anadhihirisha viwango vya juu kama vile matendo yasiyo ya ubinafsi yanayowanufaisha wengine.—w17.10, uku. 7.