Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Ni Nini Kimekosekana Katika Picha Hizi?

Soma Methali 18:10 na 26:17. Kisha utazame picha. Ni vitu gani vimekosekana? Andika majibu yako kwenye mistari iliyo hapa chini. Unganisha nukta zilizopo ili ukamilishe picha hizi, kisha uzipake rangi.

1. ․․․․․

2. ․․․․․

[Michoro]

(Ona nakala iliyochapishwa)

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Unajifunza nini katika mistari hiyo? Je, kujua tu jina la Mungu kunatosha ili mtu apate kibali chake?

DOKEZO: Soma Zaburi 91:2; Methali 3:5, 6.

Kwa nini ni jambo la hekima kuepuka kujiingiza katika mambo ya watu wengine?

DOKEZO: Soma Wagalatia 6:5-7; 1 Wathesalonike 4:11; 1 Petro 4:15.

Kisha, soma Methali 26:18, 19. Je, kuna ubaya wowote kuwatendea watu mambo mabaya kwa utani?

DOKEZO: Soma Methali 14:13; 15:21; Mathayo 7:12.

UTENDAJI WA FAMILIA:

Someni pamoja Methali 31:10-31. Mtu mmoja katika familia aigize shughuli ambazo mke mwenye uwezo anapaswa kutimiza zinazoelezwa hapo, bila kuzungumza. Wengine katika familia wajaribu kukisia anafanya nini. Zungumzieni kazi mbalimbali ambazo mnaweza kujifunza ili mzitimize vizuri zaidi.

Kusanya na Ujifunze

Kata, kunja katikati, na uhifadhi

KADI YA BIBLIA 10 SULEMANI

MASWALI

A. Sulemani hakuomba apewe utajiri au aishi muda mrefu, bali aliomba nini?

B. Jaza mapengo haya. Sulemani alikuwa na uwezo wa kusema methali ․․․․․, na nyimbo zake zilikuwa ․․․․․.

C. Sulemani alipewa jina gani lingine?

[Chati]

4026 K.W.K. 1 W.K. 98 W.K.

Adamu aumbwa Aliishi miaka ya Kitabu cha mwisho

1000 K.W.K. cha Biblia chaandikwa

[Ramani]

Malkia wa Sheba alisafiri kilomita 2,400 hivi kusikiliza hekima ya Sulemani

SHEBA

Yerusalemu

SULEMANI

MAMBO MACHACHE KUMHUSU

Mwana wa pili wa Daudi na Bath-sheba. Sulemani alitawala Israeli kwa miaka 40. Alijenga nyumba kubwa kwa ajili ya ibada ya Yehova. (1 Wafalme 5:2-5) Yehova alimtumia Sulemani kuandika kitabu cha Methali, Mhubiri, na cha Wimbo wa Sulemani. Kushirikiana na wake wa kigeni kuligeuza moyo wake kutoka kwa Yehova.—1 Wafalme 11:1-6.

MAJIBU

A. Moyo mtiifu.—1 Wafalme 3:5-14.

B. 3,000, 1,005.—1 Wafalme 4:29, 32.

C. Yedidia, linalomaanisha “Apendwaye na Yehova.”—2 Samweli 12:24, 25.

Watu na Nchi

3. Jina langu ni Chloe. Nina umri wa miaka 9, na ninaishi nchini Kanada. Kuna Mashahidi wangapi wa Yehova wanaoishi nchini Kanada? Ni 55,000, 88,000, au 110,000?

4. Ni nukta gani inayoonyesha eneo ninaloishi? Chora duara kuizunguka na utie nukta kuonyesha eneo unaloishi kisha uone kwenu ni umbali gani kutoka Kanada.

A

B

C

D

Watoto Watafute Picha

Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.

Ili kuchapisha nakala zaidi za “Mazungumzo ya Familia,” tembelea Tovuti ya www.jw.org

● “MAZUNGUMZO YA FAMILIA” majibu kwenye ukurasa wa 24

MAJIBU YA UKURASA WA 30 NA 31

1. Mnara wenye nguvu.

2. Mbwa.

3. 110,000.

4. A.