Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

‘Nilitaka Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Dini Yangu’

‘Nilitaka Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Dini Yangu’

‘Nilitaka Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Dini Yangu’

WALIPOPEWA mgawo wa somo la historia shuleni, Ciara, mwenye umri wa miaka 12 kutoka Florida, Marekani, alichagua habari yenye kupendeza, yaani, mateso dhidi ya Mashahidi wa Yehova katika Ujerumani ya Nazi. Anasema, “Nilichagua habari hiyo kwa sababu nilitaka kujua mengi zaidi kuhusu historia ya dini yangu. Nilitaka kujua hasa mambo yaliyowapata Mashahidi wa Yehova wakati wa yale Maangamizi Makubwa.”

Baada ya kufanya utafiti mwingi, Ciara alitengeneza piramidi ya mbao ya rangi ya zambarau, ambayo iliwakilisha umbo la pembe tatu la zambarau lililoshonwa kwenye yunifomu za Mashahidi wa Yehova ili kuwatambulisha katika kambi. Ciara aliongeza picha zaidi pamoja na kuweka maelezo kwenye picha upande wa piramidi. Pia alitia ndani barua yenye kuhuzunisha na yenye kutia moyo, iliyoandikwa na Wolfgang Kusserow, mmoja wa Mashahidi wa Yehova, kabla tu hajauawa.−Ona gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 1, 1985, ukurasa wa 14, la Kiingereza.

Ciara alieleza waziwazi kwamba, tofauti na wafungwa wengine, Mashahidi wa Yehova walikuwa na uchaguzi: Ikiwa wangetia sahihi hati fulani na kukana imani yao, wangeachiliwa. Kwa kuwa wengi wao hawakutia sahihi hati hiyo, jambo hilo lilithibitisha utimilifu wa Mashahidi wa Yehova.

Ciara anasema kwamba alinufaika kwa kuchagua habari hiyo katika mgawo aliopewa. Bila shaka, habari hiyo ilimsaidia kujua mengi zaidi kuhusu dini yake. Anasema: “Licha ya kwamba Mashahidi wa Yehova walikuwa kikundi kidogo huko Ujerumani, walikuwa na imani yenye nguvu ambayo iliwasaidia kushinda mateso waliyopata.”

Ikiwa wewe ni kijana Shahidi wa Yehova shuleni, je, kuna njia unazoweza kutumia ili kuzungumzia historia ya dini yako?