Namna ya Kuvala na Kujipamba ya Wengine Ilikuwa Nanikwaza
EILEEN BRUMBAUGH ANAELEZA MAISHA YAKE
NILIZALIWA mu dini ya Ndugu Wabatiste wa Alemanye wa Shirika ya Zamani. Ile dini iko sawa dini ya Waamishi na ya Wamenonite. Ilianzia Alemanye mu mwaka wa 1708. Ilikuwa na kusudi ya kusaidia watu walamuke kiroho. Kitabu The Encyclopedia of Religion inasema kama “ile dini ilianza juu watu fulani walitambua kama kila mwanadamu iko na lazima ya kusikia injili ya Kristo.” Ile ilifanya wamisionere wengi watumwe mu inchi za mingi.
Mu mwaka wa 1719, kikundi kidogo yenye iliongozwa na Alexander Mack ilifika mu eneo yenye inaitwa sasa Pennsylvania, katika Amerika. Tangu ile wakati, vikundi vingine vidogo vilianza na vikagawangika-gawanyika. Kila kikundi ilikuwa na namna yake ya kufasiria mafundisho ya Alexander Mack. Kikundi yetu ya kidogo ilikuwa na watu 50 hivi. Mu kikundi yetu, tulitiwa moyo kusoma Biblia na kufuata kabisa maamuzi ya kanisa.
Tangu zamani, watu wa familia yetu walikuwa mu ile dini. Na miye niliingia mu ile dini na nikabatizwa wakati nilikuwa na miaka 13. Nilifundishwa kama ilikuwa mubaya kuwa na ao kutumia gari, traktere, telefone, radio, ao kitu ingine yenye iliomba kutumia umeme. Wanamuke walikuwa navala manguo ya hali ya chini, hawakukuwa nakata nywele, na walikuwa nafunika kichwa. Wanaume hawakukuwa nakata ndevu. Tuliwaza kama juu ya kuonyesha kuwa hatukuwa sehemu ya ulimwengu, hatukupaswa kuvala manguo ya sasa, hatukupaswa kujipamba, ao kuvala vitu vya kujipamba. Tuliona kama kufanya vile ilikuwa zambi ya kiburi.
Tulifundishwa kama tunapaswa kuheshimia sana Biblia, yenye tuliona kuwa chakula yetu ya kiroho. Kila asubui, mbele ya kunywa chai, tulikuwa naikala karibu na papa na kumusikiliza wakati alikuwa nasoma sura moya ya Biblia na kuifasiria. Kisha tulikuwa napiga magoti wakati papa alikuwa nasali. Kisha pale, mama alikuwa narudilia sala ya Baba Yetu. Nilikuwa nangoya kwa hamu ibada yetu ya asubui, wakati familia yetu ilikuwa nakutana na kukaza akili juu ya mambo ya kiroho.
Tuliishi mu shamba, karibu na Delphi, Indiana, na kule tulikuwa nalima chakula mbalimbali. Tulikuwa natia ile chakula mu gari yenye kukotwa na farasi, kisha tulikuwa naipeleka mu muji na kuiuzisha mu barabara na nyumba kwa nyumba. Tuliona kama kufanya kazi kwa bidii ilikuwa pia “kumutumikia Mungu.” Kwa hiyo, tulitumika sana kila siku. Siku ya Yenga tu njo hatukukuwa natumika juu hatukupaswa kufanya kazi yoyote ya nguvu ile siku. Lakini, wakati fulani familia yetu ilitumika sana mupaka haikukuwa tena na wakati ya kukaza akili juu ya mambo ya kiroho.
Ndoa na Familia
Mu mwaka wa 1963, wakati nilikuwa na miaka 17, niliolewa na James mwenye naye alikuwa mu dini ya Ndugu Wabatiste. Familia yake pia ilikuwa mu dini ya Ndugu Wabatiste tangu wazazi wa wazazi wa wazazi wake. Siye wote tulipenda sana kumutumikia Mungu na tuliamini kama dini yetu tu njo ya kweli.
Kufikia mwaka ya 1975, tulikuwa tulishakuwa na watoto sita, na mu 1983, mutoto wetu wa saba alizaliwa; yeye njo alikuwa wa mwisho. Rebecca, mutoto wa pili, njo tu mutoto mwanamuke mwenye tulikuwa naye. Tulitumika sana, tulitumikisha makuta kidogo, na tuliishi maisha ya mwepesi. Tulijikaza kufundisha watoto wetu kanuni za Biblia zenye wazazi wetu na watu wengine wa dini ya Wabatiste wa Zamani walitufundishaka.
Dini ya Ndugu Wabatiste ilikazia sana namna watu walionekana kwa inje. Tuliona kama juu hatuwezi kusoma moyo wa mutu, namna yake ya kuvala njo ilionyesha hali ya moyo wake. Kwa hiyo, kama mwanamuke alivimbisha sana nywele yake, ile ilikuwa alama ya kiburi. Kama mutu angevala nguo yenye iko na michoro ya kabambi-kabambi, ile ilikuwa pia alama ya kiburi. Wakati fulani tulikazia sana ile mambo kupita mambo yenye Biblia inasema.
Kufungwa mu Gereza
Ku mwisho wa miaka ya 1960, Jesse, ndugu ya bwana yangu, mwenye alikomalia pia mu dini ya Ndugu Wabatiste, alifungwa juu alikatala kazi ya jeshi. Wakati alikuwa mu gereza, alikutana na Mashahidi wa Yehova wenye wanaamini pia kama kujiingiza mu mambo ya vita inapingana na kanuni za Biblia. (Isaya 2:4; Matayo 26:52) Jesse alizungumuza sana na Mashahidi wa Yehova juu ya Biblia na alijionea sifa zao za muzuri. Kisha kujifunza sana Biblia, alibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova. Ile haikutufurahisha.
Jesse aliambia bwana yangu mambo yenye alikuwa amejifunza. Alifanya pia mipango juu bwana yangu akuwe napata kwa ukawaida gazeti Munara wa Mulinzi na Amuka! Ile magazeti ilifanya bwana yangu afurahie sana Biblia. Bwana yangu James alikuwa napenda sana kumutumikia Mungu, lakini mara mingi alikuwa najisikia kama iko mbali na Mungu. Kwa hiyo, alifurahia kitu yoyote yenye ingemusaidia amukaribie Mungu.
Wazee wetu walitutia moyo tusome magazeti ya dini ya Waamishi, ya Wamenonite, na ya dini zingine za Ndugu Wabatiste hata kama tuliona kuwa wako sehemu ya ulimwengu. Baba yangu alichukia sana Mashahidi. Hakupenda hata kidogo tusome gazeti Munara wa Mulinzi na Amuka! Kwa hiyo, niliogopa sana wakati niliona James iko nasoma ile magazeti. Niliwaza kama atapata ndani mafundisho ya uongo.
Lakini kwa muda murefu, James alikuwa ameshakia mafundisho fulani ya dini ya Ndugu Wabatiste yenye aliona kama inapingana na Biblia, zaidi sana fundisho yenye kusema kama ni zambi kufanya “kazi ya nguvu” Siku ya Yenga. Kwa mufano, dini ya Ndugu Wabatiste ilifundisha kama inaruhusiwa kupatia wanyama maji Siku ya Yenga, lakini hairuhusiwe kuongola hata liyani mu shamba. Wazee wa mu kanisa yetu hawakuweza kumuonyesha kwenye Biblia inasema vile. Polepole, na miye nikaanza kuwa na mashaka na ile mafundisho.
Tangu zamani, tuliamini kama dini yetu njo ya kweli, na tulijua mambo yenye ingetupata kama tungeiacha. Kwa hiyo, ilikuwa nguvu sana kutoka mu ile dini. Lakini, zamiri yetu haingeturuhusu tuendelee kuwa mu dini yenye haifuate kabisa-kabisa mambo yenye Biblia inasema. Mu mwaka wa 1983, tuliandikia kanisa yetu barua juu ya kuwafasiria juu ya nini tunatoka mu ile dini, na tukawaomba ile barua isomewe kanisa yote. Kisha, tukatengwa na kanisa.
Kutafuta Dini ya Kweli
Kisha pale, tulianza kutafuta dini ya kweli. Tulipenda kuwa mu dini yenye waamini wake wanafanyaka mambo yenye wanafundishaka wengine. Kwanza tulitia pembeni dini zote zenye zinajiingizaka mu vita. Lakini tulikuwa tungali tunafurahia dini zenye zilitia watu moyo waishi maisha ya mwepesi na wavale manguo ya hali ya chini, juu tuliona kama kufanya vile kulionyesha kama hawako sehemu ya ulimwengu. Kuanzia mwaka wa 1983 mupaka 1985, tuliamua kusafiri mu maeneo mbalimbali juu ya kuchunguza dini mbalimbali. Tulichunguza dini ya Wamenonite, dini ya Shirika ya Kidini ya Marafiki, na dini zingine zenye zilitia watu moyo waishi maisha ya mwepesi.
Ileile wakati, Mashahidi wa Yehova walitutembelea mu shamba yetu, karibu na Camden, Indiana. Tulikuwa nawasikiliza na kuwaomba watumikishe tu tafsiri ya Biblia ya King James. Niliheshimia mawazo ya Mashahidi wa Yehova ya kukatala kabisa kujiingiza mu vita. Lakini ilikuwa nguvu kwangu kuwasikiliza juu hawakuona kama ni lazima kuvala manguo ya hali ya chini juu ya kuonyesha kama wanajitenga na ulimwengu. Kwa hiyo, niliona kama dini yao haiko ya kweli. Niliona kama kiburi njo ilifanya watu wavale tofauti na siye. Niliamini kama vitu vilifanya watu wakuwe na kiburi.
James alianza kuenda ku Jumba ya Ufalme, na alikuwa nabeba watoto wetu fulani. Ile ilinikasirisha sana. Aliniomba niende naye, lakini nilikatala. Siku moya alisema hivi: “Hata kama haukubaliane na mafundisho yao yote, uende tu na ujionee namna wanatendeanaka.” Namna Mashahidi wa Yehova walikuwa natendeana ilikuwa imemugusa sana.
Ku mwisho, niliamua kuenda naye, lakini nilikuwa muangalifu sana. Niliingia mu Jumba ya Ufalme na ninavala kanzu ya hali ya chini na kofia. Watoto wetu fulani hawakukuwa navala viatu, na wao pia walikuwa navala manguo ya hali ya chini. Lakini Mashahidi wa Yehova walikuya kwenye tulikuwa na wakatutendea kwa njia ya upendo. Nilijiambia hivi: ‘Tuko tofauti, lakini wanatukubali tu vile tuko.’
Upendo wao ulinigusa moyo. Lakini niliamua kuendelea kuwachunguza kwanza. Sikukuwa nasimama ao hata kuimba nyimbo zao. Kisha mukutano, nilikuwa nawamwangia mvua ya maulizo. Nilikuwa nawauliza kuhusu mambo yenye sikufurahia ao kuhusu maana ya maandiko fulani. Hata kama sikuonyesha busara, kila mutu mwenye niliuliza alinijibia kwa upole. Kitu ingine yenye ilinigusa moyo, ni kuona kama wote wenye niliuliza ulizo ileile, walinipatia majibu ileile. Wakati fulani walikuwa naniandikia majibu, na ile ilinisaidia sana juu ningeweza kuisoma miye peke wakati ingine.
Mu kipingi ya joto ya mwaka wa 1985, familia yetu ilienda ku mukusanyiko wa Mashahidi wa Yehova katika Memphis, Tennessee, juu tu ya kuangalia namna mambo ilikuwa natendeka. James alikuwa angali na mandevu yake, na miye nilikuwa ningali navala manguo yangu ya hali ya chini. Wakati wa mapumuziko, kila mara watu walikuwa nakuya kutusalimia. Walituonyesha upendo, walituhangaikia na walitukubali. Ile ilitugusa sana. Kitu ingine yenye ilitugusa sana ni umoja wao, juu fasi yote kwenye tulikuwa naenda ku mikutano, mafundisho ilikuwa ileile.
James alifurahia namna Mashahidi wa Yehova walimuhangaikia sana. Kwa hiyo, alikubali kujifunza Biblia. Alichunguza kila kitu. Alipenda akuwe hakika kama mambo yenye iko najifunza ni ya kweli. (Matendo 17:11; 1 Watesalonike 5:21) Kisha wakati fulani, aliona kama amepata kweli. Lakini miye nilivurugika. Sikupenda kuacha maisha yangu ya hali ya chini, juu niliona ile ingefanya nionekane kuwa mutu wa “ulimwengu.” Wakati nilikubali kwa mara ya kwanza kujifunza Biblia, nilikuwa na tafsiri ya King James Version ku ligoti moya, na Tafsiri ya Ulimwengu Mupya ku ligoti ingine. Nilikuwa nachunguza kila andiko mu tafsiri zote mbili juu ya kuhakikisha kama hawako nanidanganya.
Namna Nilifikia Kukubali Kweli
We were looking for good fruitage, and we found it. Jesus said: “ByWakati nilikuwa najifunza na Mashahidi, tulijifunza kama Baba wa mbinguni ni Mungu mumoja, haiko miungu tatu mu Mungu mumoja, na kama mutu yeye peke njo nafsi. Hana nafsi yenye haikufake. (Mwanzo 2:7; Kumbukumbu la Torati 6:4; Ezekieli 18:4; 1 Wakorinto 8:5, 6) Tulijifunza tena kama moto wa mateso haukuwake, na kama wakati mutu anakufa anaenda mu kaburi. (Yobu 14:13; Zaburi 16:10; Muhubiri 9:5, 10; Matendo 2:31) vKujifunza kweli juu ya moto wa mateso ilikuwa jambo ya pekee sana, juu mu kanisa ya Ndugu Wabatiste yenye tulikuwaka ndani, watu walikuwaka napingana sana juu ile fundisho.
Lakini, niliendelea kujiuliza ikiwa Mashahidi wa Yehova walikuwa dini ya kweli. Juu mu kichwa yangu, nilikuwa naona kama wangali sehemu ya ulimwengu. Hawakukuwa naishi maisha ya mwepesi, yenye niliona kama ni ya maana sana. Lakini, niliona kama walikuwa wanatii amri ya Yesu ya kuhubiria watu wote habari njema ya Ufalme. Kwa hiyo, nilivurugika!—Matayo 24:14; 28:19, 20.
Mu ile hali, yenye sikujua nifanye nini, upendo wa Mashahidi wa Yehova ulinisaidia niendelee kuchunguza mambo. Kutaniko yote ilihangaikia familia yetu. Ndugu na dada mbalimbali wa mu kutaniko walikuwa nakuya kututembelea. Wamoja walikuwa nakuya kwetu kuuza maziwa na mayai, juu tu waonane na siye. Juu Shahidi fulani alikuwa najifunza na siye Biblia, ile haikuzuia Mashahidi wengine wakuye kututembelea. Kila mara, wakati watu wa mu kutaniko walikuwa karibu na kwetu, walipita kutuangalia. Tulikuwa kabisa na lazima ya kupitisha nao wakati vile juu tufikie kuwajua muzuri, na tulifikia kufurahia sana namna walituhangaikia na kutupenda.
Haiko Mashahidi wa Yehova wa mukutaniko ya karibu njo tu walituhangaikia. Wakati nilikuwa naendelea kujiuliza maulizo juu ya namna ya muzuri ya kuvala na kujipamba, Kay Briggs, Shahidi wa Yehova wa kutaniko jirani, mwenye naye alipendelea tu kuvala manguo ya hali ya chini na hakukuwa najipamba, alikuya kunitembelea. Nilijisikia huru sana kuzungumuza naye. Kisha siku moya, Lewis Flora, mwenye naye alikuwaka mu dini yenye inafundisha watu kuisha maisha ya mwepesi, alikuya kunitembelea. Aliona namna nilikuwa nimevurugika, na juu ya kunifariji alinitumia barua ya kurasa kumi. Nilisoma barua yake mara mingi.
Niliomba mwangalizi mwenye kusafiri, Ndugu O’Dell, anifasirie maana ya Isaya 3:18-23 na 1 Petro 3:3, 4. Nilimuuliza hivi: “Hii maandiko si inaonyesha kama kuvala manguo ya hali ya chini ni jambo ya lazima ili kumupendeza Mungu?” Aliniuliza hivi: “Ni mubaya kuvala kofia? Ni mubaya kusukiwa?” Mu kanisa ya Ndugu Wabatiste, watoto wanamuke walikuwa nasukiwa, na wanamuke wenye kukomala walikuwa navala kofia. Nilitambua kama tulikuwa najipinga siye wenyewe. Nilifurahi sana kuona namna ule mwangalizi alinitendea; alinivumilia na kunitendea kwa upole.
Polepole, nilianza kuamini. Lakini kulikuwa jambo ingine yenye ilikuwa ingali nanisumbua sana: Wanamuke walikuwa nakata nywele. Wazee Wakristo walinisaidaia kuelewa kama wanamuke fulani wanakuwaka na nywele za mufupi, na wengine wanakuwaka na nywele za murefu. Ile inafanya nywele za wanamuke fulani zikuwe za muzuri zaidi kuliko za wengine? Walinisaidia pia kuelewa kama kila mutu anapaswa kuheshimia zamiri yake mu mambo ya kuvala na kujipamba. Walinipatia habari ya kusoma ku nyumba.
Kutumikisha Mambo Yenye Tulikuwa Najifunza
Tulikuwa natafuta watu wenye wanatumikishaka mambo yenye wanafundishaka, na tuliwapata. Yesu alisema hivi: “Kwa jambo hili wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu—kama muko na upendo kati yenu.” (Yohana 13:35) Tulikuwa hakika kama Mashahidi wa Yehova wanaonyeshanaka upendo wa kweli. Lakini, watoto wetu wakubwa wawili, Nathan na Rebecca, walivurugika pia, juu walikuwa walishakubali dini ya Ndugu Wabatiste na walikuwa walishabatizwa mu ile dini. Kweli za Biblia zenye tulikuwa nawafundisha ziliwagusa sana na pia upendo wa Mashahidi wa Yehova.
Kwa mufano, tangu zamani, Rebecca alikuwaka napenda sana kuwa rafiki ya Mungu. Aliona kama ni mwepesi kusali kwake wakati alijifunza kama Mungu hapangake mbele ya wakati namna maisha ya mutu itakuwa. Tena alimukaribia Mungu zaidi wakati alijifunza kama haiko Utatu wenye haueleweke, lakini ni mutu wa kweli kabisa mwenye angeweza kuiga. (Waefeso 5:1) Alifurahi pia kujua kama wakati iko nasali kwa Mungu, haikukuwa lazima atumie maneno ya zamani yenye ilikuwa mu Biblia ya King James Version. Wakati alijifunza namna Mungu anapenda tusali, na kama Mungu anapenda wanadamu waishi milele mu dunia paradiso, ile ilifanya ajisikie kuwa karibu sana na Muumbaji wake.—Zaburi 37:29; Ufunuo 21:3, 4.
Mapendeleo Yenye Tumepata
Miye na James na watoto watano wakubwa, Nathan, Rebecca, George, Daniel, na John tulibatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova mu kipindi ya joto ya mwaka wa 1987. Harley alibatizwa mu mwaka wa 1989, na Simon mu mwaka wa 1994. Familia yetu yote inaendelea kufanya kazi yenye Yesu Kristo alipatia wanafunzi wake, ni kusema, kazi ya kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu.
Watoto wetu wanaume watano, Nathan, George, Daniel, John, na Harley, na pia mutoto wetu mwanamuke Rebecca, walishakatumikia ku biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova ya Amerika. George angali natumikia kule ku biro ya tawi, na alishafanya kule miaka 14. Na Simon, mwenye alimaliza masomo mu 2001, ameanza naye kutumikia ku biro ya tawi. Watoto wetu wanaume ni wazee ao watumishi wa huduma mu makutaniko ya Mashahidi wa Yehova. Bwana yangu ni muzee mu kutaniko ya Thayer, katika Missouri, na miye ninaendelea kuhubiri kwa bidii.
Sasa tuko na wajukuu watatu, Jessica, Latisha, na Caleb. Na tuko na furaha sana juu wazazi wao wamewafundisha kumupenda Yehova tangu wakati walikuwa wadogo. Siye wote mu familia tunafurahi sana juu Yehova alituvuta kwake na alitusaidia kutambua watu wenye kuitwa kwa jina yake kupitia upendo wao.
Tunasikilia huruma watu wenye wanapenda kumufurahisha Mungu, lakini wamefundishwa kuheshimia sana kanuni za dini kuliko mambo yenye Biblia inasema. Tunatumaini kama nao watapata furaha yenye tumepata. Tulikuwaka naenda nyumba kwa nyumba juu ya kuuzishia watu mboga, lakini sasa tuko naenda nyumba kwa nyumba juu ya kuhubiria watu habari njema juu ya Ufalme wa Mungu na mambo ya muzuri yenye utafanya. Wakati ninakumbukaka uvumilivu na upendo wenye watu wa Yehova walituonyesha, ninaliaka kwa furaha!
[Picha]
Wakati nilikuwa na miaka saba hivi, na wakati nilishakuwa mutu muzima
[Picha]
James, George, Harley, na Simon, na wanavala manguo ya hali ya chini
[Picha]
Hii picha yenye inanionyesha na niko napeleka chakula ku soko, ilichapishwa mu gazeti fulani ya mu eneo yetu
[Kwenye Picha Ilitoka]
Journal and Courier, Lafayette, Indiana
[Picha]
Familia yetu leo

