Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 27

Maktaba ya Jumba la Ufalme Inaweza Kutunufaisha Jinsi Gani?

Maktaba ya Jumba la Ufalme Inaweza Kutunufaisha Jinsi Gani?

Israeli

Jamhuri ya Cheki

 

Benin

Visiwa vya Cayman

Je, ungependa kufanya utafiti ili uielewe Biblia vizuri zaidi? Je, ungependa kujua mengi zaidi kuhusu andiko, mtu, eneo, au jambo lolote katika Biblia? Au, je, ungependa kujua ikiwa Neno la Mungu linaweza kukusaidia kushughulikia jambo fulani linalokuhangaisha? Ikiwa ndivyo, unaweza kutumia maktaba ya Jumba la Ufalme.

Kuna vifaa vya utafiti. Labda huna machapisho yote ya Biblia ya Mashahidi wa Yehova katika lugha yako. Hata hivyo, maktaba ya Jumba la Ufalme ina machapisho mengi ya karibuni. Huenda pia kukawa na tafsiri mbalimbali za Biblia, kamusi, na vitabu vya marejeo. Unaweza kutumia maktaba hiyo kabla au baada ya mikutano. Ikiwa kuna kompyuta huenda ikawa na programu ya Watchtower Library. Programu hiyo ina machapisho mengi na ni rahisi kuitumia kufanya utafiti kuhusu jambo lolote, neno, au hata andiko la Biblia.

Inasaidia wanafunzi katika Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo. Unaweza kutumia maktaba ya Jumba la Ufalme unapotayarisha migawo yako. Mwangalizi wa Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ndiye msimamizi wa maktaba. Yeye ana jukumu la kuhakikisha machapisho mapya yanawekwa na kupangwa vizuri. Yeye au yule anayejifunza Biblia pamoja nawe anaweza kukuonyesha namna ya kutafuta habari unayohitaji. Hata hivyo, hatupaswi kuchukua vitabu vya maktaba ya Jumba la Ufalme na kwenda navyo. Pia, tunapaswa kutunza vitabu hivyo na kuepuka kuvichora au kuvitia alama yoyote.

Biblia inaeleza kwamba ili “[tupate] ujuzi kumhusu Mungu” ni lazima tuutafute kama tunavyotafuta “hazina zilizofichika.” (Methali 2:1-5) Maktaba ya Jumba la Ufalme inaweza kukusaidia kutimiza jambo hilo.

  • Ni vifaa gani vya utafiti vinavyopatikana katika maktaba ya Jumba la Ufalme?

  • Ni nani anayeweza kukusaidia kutumia maktaba hiyo vizuri?