Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 16

Watumishi wa Huduma Wana Majukumu Gani?

Watumishi wa Huduma Wana Majukumu Gani?

Myanmar

Mkutano

Kikundi cha utumishi

Udumishaji wa Jumba la Ufalme

Biblia hutaja vikundi viwili vya wanaume Wakristo ambao hushughulikia majukumu ya kutaniko, yaani, “waangalizi na watumishi wa huduma.” (Wafilipi 1:1) Kwa kawaida, katika kila kutaniko kuna wazee na watumishi wa huduma kadhaa. Watumishi wa huduma wanafanya kazi gani kwa faida yetu?

Wanalisaidia baraza la wazee kutanikoni. Watumishi wa huduma ni wanaume wa kiroho, wenye kutegemeka, na wenye bidii. Baadhi yao ni vijana na wengine wana umri mkubwa. Wanafanya kazi za kawaida lakini ambazo ni muhimu kutanikoni. Utumishi wao huwawezesha wazee kupata wakati wa kukazia fikira ufundishaji na uchungaji.

Wanatimiza huduma muhimu. Baadhi ya watumishi wa huduma hupewa mgawo wa kuwakaribisha wote wanaofika mikutanoni. Wengine hushughulikia mfumo wa sauti, vitabu na magazeti, hesabu za kutaniko, na migawo ya maeneo kutanikoni. Pia, wao husaidia katika kudumisha Jumba la Ufalme. Wazee wanaweza kuwaomba wawasaidie ndugu na dada waliozeeka. Hata iwe wana migawo gani, wanastahili kuheshimiwa na wote kutanikoni kwa sababu ya roho yao ya kutumikia.—1 Timotheo 3:13.

Wanaweka mfano mzuri. Watumishi wa huduma huwekwa rasmi kwa sababu ya sifa zao nzuri za kiroho. Wanaposhughulikia migawo yao katika mikutano, wanaimarisha imani yetu. Wanapoongoza katika kazi ya kuhubiri, wanatuchochea kuwa wenye bidii. Roho yao ya ushirikiano huchangia shangwe na umoja. (Waefeso 4:16) Baada ya muda, huenda wao pia wakastahili kutumikia wakiwa wazee.

  • Watumishi wa huduma ni watu wa aina gani?

  • Watumishi wa huduma wanalisaidiaje kutaniko?