JIFUNZE KUTOKA KWA YESU

Tenga Muda wa Kumjua Mungu

Tenga Muda wa Kumjua Mungu

 Maisha yako yatakuwa mazuri zaidi ukitenga muda wa kumjua Mungu na kuwa rafiki yake. Unapofanya hivyo, unatosheleza uhitaji wako wa kiroho. Fikiria mambo ambayo Yesu alisema kuhusu kutosheleza uhitaji wetu wa kiroho.

Mambo ambayo Yesu alisema

 “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.”​—Mathayo 5:3.

  •   Sisi sote tungependa kupata majibu ya maswali kama vile: Kusudi la maisha ni nini? Kwa nini watu wanateseka sana? Ni nini hutupata tunapokufa? Tunapopata majibu ya maswali hayo, tunakuwa na furaha.

 “Mwanadamu hataishi kwa mkate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.”​—Mathayo 4:4.

  •   Kama tulivyo na uhitaji wa chakula cha kimwili, ndivyo tulivyo na uhitaji wa chakula cha kiroho. Yesu alifundisha kwamba tunahitaji kumtegemea Mungu ili atosheleze uhitaji wetu wa kiroho.

 “Neno lako ni kweli.”​—Yohana 17:17.

  •   Yesu alifundisha kwamba njia ya msingi ambayo Mungu hutosheleza uhitaji wetu wa kiroho ni kupitia Neno Lake, Biblia.

 Tunakutia moyo utenge wakati wa kumjua Mungu na kutosheleza uhitaji wako wa kiroho na hilo litakufanya uwe na furaha ya kudumu. Mambo yafuatayo yanaweza kukusaidia:

Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu. (Zaburi 83:18) Ona makala yenye kichwa “Yehova Ni Nani?