Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

 HABARI KUU | UNAWEZA KUMKARIBIA MUNGU

Hii Ni Njia Bora ya Maisha

Hii Ni Njia Bora ya Maisha

Unapaswa kufanya nini ili umkaribie Mungu? Tumechunguza hatua kadhaa unazoweza kuchukua ili uwe rafiki ya Mungu:

  1. Unahitaji kujua na kulitumia jina la Mungu, Yehova.

  2. Zungumza naye kwa ukawaida kwa kusali na kusoma Neno lake, Biblia.

  3. Endelea kufanya mambo yanayompendeza Yehova.

Ili umkaribie Mungu unahitaji kutumia jina lake, usali kwake, kujifunza Biblia, na kufanya mambo yanayompendeza

Kwa msingi wa mambo hayo, je, unafikiri kwamba unafanya mambo yanayohitajika ili kumkaribia Mungu? Je, unahisi kuna mambo unayohitaji kurekebisha? Kwa kweli, jitihada inahitajika, lakini utapata matokeo mazuri.

Jennifer mwanamke anayeishi Marekani anasema hivi: “Kila jitihada unayofanya ili kumkaribia Mungu ina faida. Urafiki na Mungu unaleta baraka nyingi kutia ndani: kumtumaini, kumjua vizuri zaidi, na zaidi ya yote, kumpenda. Hii ni njia bora ya maisha!”

Ikiwa ungependa kuwa na uhusiano mzuri na Mungu, Mashahidi wa Yehova watafurahia kukusaidia ufanye hivyo. Watapanga kujifunza Biblia pamoja nawe, bila malipo. Pia unakaribishwa kuhudhuria mikutano yao ya Biblia kwenye Jumba la Ufalme, ambapo utafurahia kushirikiana na watu wanaothamini uhusiano wao na Mungu. * Unapoendelea kufanya hivyo, wewe pia utahisi kama alivyohisi mtunga-zaburi aliyeimba hivi: “Lakini mimi, kumkaribia Mungu ni kwema kwangu.”—Zaburi 73:28.

^ fu. 9 Ili kuomba ufundishwe Biblia au kujua mahali lilipo Jumba la Ufalme lililo karibu nawe, tafadhali zungumza na mtu aliyekuletea gazeti hili au tembelea Tovuti yetu, www.jw.org/sw, na utazame kichwa WASILIANA NASI.