Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu ya Maswali ya Biblia

Majibu ya Maswali ya Biblia

Ibilisi alitoka wapi?

Mungu hakumuumba Ibilisi. Badala yake, Mungu alimuumba malaika ambaye baadaye aligeuka na kuwa Ibilisi, pia anayeitwa Shetani. Yesu alionyesha kwamba wakati fulani Ibilisi alikuwa mnyoofu na asiye na hatia. Hivyo basi, mwanzoni Ibilisi alikuwa malaika, mwana mkamilifu wa Mungu.—Soma Yohana 8:44.

Malaika angegeukaje na kuwa Ibilisi?

Malaika aliyegeuka na kuwa Ibilisi aliamua kumpinga Mungu na akawashawishi wanadamu wawili wa kwanza wajiunge naye. Alijifanya mwenyewe kuwa Shetani, jina linalomaanisha “Mpinzani.”—Soma Mwanzo 3:1-5; Ufunuo 12:9.

Kama viumbe wengine wa Mungu wenye akili, malaika aliyegeuka na kuwa Ibilisi alikuwa na uhuru wa kuchagua kufanya mema au mabaya, lakini alisitawisha tamaa ya kuabudiwa. Alitamani sana kupata utukufu kuliko kumpendeza Mungu.—Soma Mathayo 4:8, 9; Yakobo 1:13, 14.

Ibilisi ameendeleaje kuwashawishi wanadamu? Je, unapaswa kumwogopa? Unaweza kupata majibu ya maswali hayo katika Biblia.