Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Tazama Picha!”

“Tazama Picha!”

Ni mara ngapi umesema au kuwaambia wengine maneno hayo unapofungua kurasa za toleo jipya la gazeti hili? Michoro na picha zinazovutia zinazotayarishwa kwa makini sana huwekwa humo kwa kusudi fulani. Ni misaada muhimu ya kufundishia inayochochea fikira na hisia zetu. Picha hizo zinaweza kutusaidia hasa tunapotayarisha na kushiriki kutoa maelezo katika Funzo la Mnara wa Mlinzi.

Kwa mfano, fikiria kwa makini ni kwa nini picha ya kwanza katika kila makala ya funzo ilichaguliwa kwa ajili ya makala hiyo. Inakazia nini? Inahusianaje na kichwa cha makala au andiko la msingi? Fikiria jinsi kila picha inavyohusiana na habari inayozungumziwa na jinsi inavyohusu maisha yako binafsi.

Kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi hulipatia fursa kutaniko kutoa maelezo kuhusu kila picha, kueleza jinsi inavyohusiana na jambo kuu au jinsi inavyohusu maisha yao binafsi. Nyakati fulani, kuna maelezo yanayoonyesha jinsi picha inavyohusiana na fungu fulani hususa. Nyakati nyingine, anayeongoza anaweza kuamua picha inafaa kuzungumziwa katika fungu gani. Kwa njia hiyo, wote watafaidika kikamili na jitihada zilizofanywa ili kumsaidia msomaji kupiga picha akilini mambo anayojifunza katika Neno la Mungu.

Ndugu mmoja alisema hivi: “Baada ya kusoma makala iliyoandikwa kwa njia nzuri sana, picha huongeza ladha ya makala.”