Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Asanteni kwa Mfululizo Huo!”

“Asanteni kwa Mfululizo Huo!”

“Asanteni kwa Mfululizo Huo!”

● Watu kutoka sehemu zote ulimwenguni wameshukuru sana kwa mfululizo unaoitwa “Mazungumzo ya Familia” unaotokea katika kila toleo la Amkeni! kwenye ukurasa wa 30 na 31. Picha na maswali yanayohusisha mazungumzo, kadi ya kukata na kuhifadhi, sehemu ya watoto kutafuta picha, na sehemu ya utendaji wa familia ni zenye kuelimisha na zinafurahisha familia yote. Fikiria maelezo yafuatayo:

“Mimi huongoza funzo la Biblia pamoja na wajukuu wangu wawili wenye umri wa miaka 12 kupitia barua. Kwa kutumia sehemu yenye kichwa ‘Mazungumzo ya Familia,’ mimi huwaambia wajaze majibu yao na wanirudishie kurasa hizo. Inaonekana kwamba wajukuu wanafurahia sana funzo hilo, na katika barua mimi hueleza zaidi kuhusiana na mambo yanayozungumziwa. Asanteni kwa mfululizo huo!”

V. C., Marekani

“Hivi karibuni, mwana wangu mwenye umri wa miaka mitano aliniomba tupitie sehemu yenye kichwa ‘Picha Hii Ina Kasoro Gani?’ kabla ya kulala. Nilichukua gazeti moja na tukaanza kuzungumzia picha hiyo. Mwana wangu alisikiliza kwa makini niliposoma simulizi hilo moja kwa moja kutoka kwa Biblia. Sasa karibu kila usiku anataka kujifunza. Mimi na familia yangu tunawashukuru sana kutoka moyoni kwa kuwasaidia watoto wetu kuifurahia Biblia.”

M. F., Ufaransa

“Nilikutana na David, aliye na umri wa miaka 12 na Jennifer, mwenye umri wa miaka 6, kwenye kituo cha basi. Baba yao aliona kwamba nilikuwa nikiwatolea wasafiri gazeti Amkeni!, kwa hiyo aliwaruhusu wanikaribie ili wachunguze. Huku baba na mwana walipoanza kusoma magazeti yao, mimi na Jennifer tulifurahia kuangalia picha zenye kuvutia na picha za ndege na za wanyama. Tulizungumza kuhusu mambo yote mazuri ambayo Yehova Mungu ametufanyia ili tufurahie. Tulipofika kwenye ukurasa wa 31 tulijaribu ile sehemu ‘Watoto Watafute Picha.’ Nilipokuwa nikijaribu kupata picha ya kwanza, Jennifer alifungua kurasa haraka na kuipata kwa sekunde chache. Tulijaribu kupata picha ya pili na ya tatu, naye alizipata zote kabla yangu. Kwa kweli, Jennifer alitaka tuendelee kufanya sehemu hiyo katika magazeti mengine kumi! Mwishowe Jennifer aliomba nakala mbili za ziada awapelekee baba na kaka yake. Nilipokuwa nikiondoka, wote watatu walinishukuru kwa habari hiyo nzuri sana.”

M. C., Ekuado