Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Umuhimu wa Kuzingatia Kazi za Ajabu za Mungu”

“Umuhimu wa Kuzingatia Kazi za Ajabu za Mungu”

Njoo, usikilize hotuba ya watu wote bila malipo

“Umuhimu wa Kuzingatia Kazi za Ajabu za Mungu”

KUANZIA mwezi huu hotuba iliyoonyeshwa juu itatolewa ikiwa jambo kuu kwenye Mikusanyiko ya Wilaya 181 ya siku tatu huko Marekani ya Mashahidi wa Yehova yenye kichwa “Watekelezaji wa Neno la Mungu.” Mikusanyiko 38 kati yake itakuwa katika lugha ya Kihispania, na 17 katika lugha 12 mbali na Kiingereza. Kichwa hicho kitakaziwa katika mikusanyiko mingine zaidi ya 2,000 katika nchi zaidi ya 150 ulimwenguni pote.

Wanadamu wametimiza kazi nyingi za kustaajabisha katika karne ya 20 na bila shaka watatimiza nyingine zaidi katika karne ya 21. Lakini kazi hizo za wanadamu ni duni kama nini zilinganishwapo na kazi za Mungu! Si ajabu kwamba mtu mmoja wa kale mwenye hekima alisihi hivi: “Simama kimya, uzingatie kazi za ajabu za Mungu”!—Ayubu 37:14, NW.

Twapaswa kujifunza masomo gani kutokana na uumbaji unaotuzunguka, kama vile mawimbi, mvua, theluji, na upepo? Chanzo cha uumbaji huo chapasa kutuathirije leo? Maswali hayo na mengineyo yatajibiwa katika hotuba hiyo.

Wasiliana na Mashahidi wa Yehova walio karibu nawe au andikia wachapishaji wa gazeti hili kwa habari za mahali pa mkusanyiko palipo karibu nawe. Toleo la Februari 15 la gazeti-jenzi letu, Mnara wa Mlinzi, laorodhesha tarehe za mikusanyiko yote katika Burundi, Kongo (Kinshasa), Kenya, Rwanda, Tanzania, na Uganda.