Ezra 7:1-28

7  Na baada ya mambo hayo katika utawala wa Artashasta+ mfalme wa Uajemi, Ezra+ mwana wa Seraya+ mwana wa Azaria mwana wa Hilkia+  mwana wa Shalumu+ mwana wa Sadoki mwana wa Ahitubu+  mwana wa Amaria+ mwana wa Azaria+ mwana wa Merayothi+  mwana wa Zeraya+ mwana wa Uzi+ mwana wa Buki+  mwana wa Abishua+ mwana wa Finehasi+ mwana wa Eleazari+ mwana wa Haruni+ mkuu wa makuhani+  huyo Ezra alitoka Babiloni; naye alikuwa mwandikaji stadi+ katika sheria ya Musa,+ ambayo Yehova Mungu wa Israeli alikuwa ametoa, hata mfalme akampa maombi yake yote, kulingana na mkono wa Yehova Mungu wake juu yake.+  Kwa hiyo baadhi ya wana wa Israeli na wa makuhani+ na Walawi+ na waimbaji+ na watunza-malango+ na Wanethini+ wakaenda Yerusalemu katika mwaka wa saba wa Mfalme Artashasta.+  Mwishowe akaja Yerusalemu mwezi wa tano, yaani, katika mwaka wa saba wa huyo mfalme.  Kwa maana katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza yeye mwenyewe alipanga safari ya kutoka Babiloni, na katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano akaja Yerusalemu, kulingana na mkono mwema wa Mungu wake juu yake.+ 10  Kwa maana Ezra mwenyewe alikuwa ameutayarisha+ moyo wake kutafuta shauri katika sheria ya Yehova+ na kuifanya+ na kufundisha+ sharti+ na haki+ katika Israeli. 11  Na hii ni nakala ya barua ambayo Mfalme Artashasta alimpa Ezra kuhani, mwandikaji,+ mwandikaji wa maneno ya sheria za Yehova na masharti yake kwa Israeli: 12  “Artashasta,+ mfalme wa wafalme,+ kwa Ezra kuhani, mwandikaji wa sheria ya Mungu wa mbinguni:+ Amani na ikamilishwe.+ Basi 13  mimi nimetoa agizo+ kwamba kila mtu katika utawala wangu+ ambaye ni mmoja wa watu wa Israeli na makuhani wao na Walawi, ambaye yuko tayari kwenda Yerusalemu pamoja nawe, aende.+ 14  Kwa kuwa agizo lilitolewa kutoka mbele ya mfalme na washauri wake saba+ ili kuchunguza+ kuhusu Yuda na Yerusalemu katika sheria+ ya Mungu wako+ iliyo mkononi mwako, 15  na kuleta fedha na dhahabu ambayo mfalme na washauri wake wamejitolea kutoa+ kwa Mungu wa Israeli, ambaye makao yake yako Yerusalemu,+ 16  na fedha na dhahabu yote ambayo utapata katika wilaya yote ya utawala ya Babiloni pamoja na zawadi ya watu+ na makuhani ambao wanatoa kwa hiari kwa nyumba ya Mungu wao,+ iliyoko Yerusalemu; 17  kwa hiyo utanunua kwa pesa hizo mara moja ng’ombe-dume,+ kondoo-dume,+ wana-kondoo+ na matoleo yao ya nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji+ nawe utavileta kwenye madhabahu ya nyumba ya Mungu wenu,+ iliyoko Yerusalemu.+ 18  “Na lolote linaloonekana kuwa jema kwako na kwa ndugu zako kuifanyia ile fedha na dhahabu iliyobaki,+ kulingana na mapenzi+ ya Mungu wenu, fanyeni.+ 19  Na vyombo+ unavyopewa kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wako, uvipeleke vyote mbele za Mungu katika Yerusalemu.+ 20  Na mahitaji mengineyo ya nyumba ya Mungu wako ambayo una wajibu wa kutoa, utayatoa kutoka katika nyumba ya hazina za mfalme.+ 21  “Nami mwenyewe, Mfalme Artashasta, nimetoa agizo+ kwa waweka-hazina+ wote walioko ng’ambo ya Mto,+ kwamba kila kitu anachowaomba Ezra+ kuhani, mwandikaji wa sheria ya Mungu wa mbinguni, kitafanywa mara moja, 22  hata kufikia talanta mia moja+ za fedha na vipimo vya kori+ mia moja vya ngano na vipimo vya bathi+ mia moja vya divai+ na vipimo vya bathi mia moja vya mafuta,+ na chumvi+ bila kikomo. 23  Mambo yote yaliyoagizwa+ na Mungu wa mbinguni na yafanywe kwa bidii+ kwa ajili ya nyumba ya Mungu wa mbinguni,+ ili ghadhabu isije juu ya utawala wa mfalme na wanawe.+ 24  Nanyi mnajulishwa kwamba hairuhusiwi kutoza kodi,+ wala ushuru+ wala ada yoyote juu ya yeyote wa makuhani+ na Walawi,+ wanamuziki,+ watunza-milango,+ Wanethini,+ na wafanyakazi wa hii nyumba ya Mungu. 25  “Na wewe, Ezra, kulingana na hekima+ ya Mungu wako iliyo katika mkono wako, weka mahakimu na waamuzi ili sikuzote wawahukumu+ watu wote walio ng’ambo ya Mto, yaani, wale wote wanaojua sheria za Mungu wako; na kila mtu ambaye hajazijua, ninyi mtamfundisha.+ 26  Na kila mtu ambaye hatatenda sheria ya Mungu wako+ na sheria ya mfalme, na ahukumiwe mara moja, iwe ni kifo+ au ni kufukuzwa,+ au kutozwa pesa+ au kifungo.” 27  Na abarikiwe Yehova Mungu wa mababu zetu,+ ambaye ameweka jambo hili katika moyo+ wa mfalme, kuirembesha+ nyumba ya Yehova, iliyoko Yerusalemu! 28  Naye amenipa fadhili zenye upendo+ mbele ya mfalme na washauri+ wake na kuhusu wakuu wote wa mfalme wenye nguvu. Mimi nami nikajitia nguvu kulingana na mkono+ wa Yehova Mungu wangu juu yangu, nami nikawakusanya wakuu kutoka katika Israeli ili waende pamoja nami.

Maelezo ya Chini