Ezra 1:1-11

1  Na katika mwaka wa kwanza wa Koreshi+ mfalme wa Uajemi, ili neno la Yehova kwa kinywa cha Yeremia+ litimizwe, Yehova aliiamsha+ roho ya Koreshi mfalme wa Uajemi, hivi kwamba akatangaza mwito+ katika utawala wake wote, na pia kwa maandishi,+ akisema:  “Koreshi mfalme wa Uajemi amesema hivi,+ ‘Yehova Mungu wa mbinguni+ amenipa falme zote za dunia,+ naye mwenyewe amenipa utume nimjengee nyumba katika Yerusalemu,+ huko Yuda.  Yeyote aliye katikati yenu ninyi watu wake wote, Mungu wake na awe pamoja naye.+ Basi na apande na kwenda Yerusalemu, huko Yuda, na kuijenga upya nyumba ya Yehova Mungu wa Israeli—yeye ndiye Mungu wa kweli+—iliyokuwa Yerusalemu.+  Na yeyote aliyebaki mahali popote anapokaa akiwa mgeni,+ watu wa mahali pake na wamsaidie kwa fedha na kwa dhahabu na kwa mali na kwa wanyama wa kufugwa pamoja na toleo la hiari+ kwa ajili ya nyumba ya Mungu wa kweli, iliyokuwa Yerusalemu.’”  Ndipo vichwa+ vya upande wa baba vya Yuda na vya Benyamini na makuhani na Walawi wakasimama, ndiyo, kila mmoja ambaye Mungu wa kweli aliiamsha roho+ yake, ili kwenda kujenga upya nyumba ya Yehova,+ iliyokuwa Yerusalemu.  Na wale wote waliowazunguka wakaitia nguvu+ mikono yao kwa vyombo vya fedha, kwa dhahabu, kwa mali na kwa wanyama wa kufugwa na kwa vitu bora, mbali na vyote vilivyotolewa kwa hiari.+  Pia, Mfalme Koreshi mwenyewe akaleta vyombo vya nyumba ya Yehova,+ ambavyo Nebukadneza alikuwa ameleta kutoka Yerusalemu+ na kuviweka katika nyumba ya mungu wake.+  Basi Koreshi mfalme wa Uajemi akavitoa na kuviweka chini ya Mithredathi mweka-hazina na kuvihesabu na kumpa Sheshbazari+ mkuu wa Yuda.+  Basi hii ndiyo hesabu yake: vyombo 30 vya dhahabu vyenye umbo la kikapu, vyombo 1,000 vya fedha vyenye umbo la kikapu, vyombo 29 vya akiba, 10  mabakuli+ madogo 30 ya dhahabu, mabakuli madogo ya namna ya pili, 410 ya fedha, vyombo vingine 1,000. 11  Vyombo vyote vya dhahabu na vya fedha vilikuwa 5,400. Sheshbazari+ alileta kila kitu pamoja na wale waliohamishwa+ ambao walitoka Babiloni kwenda Yerusalemu.

Maelezo ya Chini