Ona video zinazopatikana

Habari Kuhusu Noa na Garika Kubwa​—Ni Mambo ya Kuwazia-wazia Tu?

Habari Kuhusu Noa na Garika Kubwa​—Ni Mambo ya Kuwazia-wazia Tu?

Jibu ya Biblia

 Garika ilikuwa tukio ya kweli. Mungu aliitumia juu ya kuharibu watu wabaya, lakini alimuambia Noa ajenge safina juu ya kuokoa watu wazuri na wanyama. (Mwanzo 6:11-20) Tunaweza kuwa hakika kama Garika ilitokea juu Biblia inaizungumuzia, na Biblia ni kitabu yenye ‘iliongozwa na roho ya Mungu.’​—2 Timoteo 3:16.

 Garika ni habari ya kweli ao ya kuwazia-wazia tu?

 Biblia inaonyesha kama Noa alikuwaka na garika ilitokeaka, haiko mambo ya uongo ao ya kuwazia-wazia.

  •   Waandikaji wa Biblia waliamini kama Noa alikuwaka. Kwa mufano, waandikaji wa Biblia, Ezra na Luka, walifanya utafiti kwa uangalifu sana juu ya kuandika historia ya Noa mwenye alikuwa mu liste ya familia za taifa ya Israeli. (1 Mambo ya Nyakati 1:4; Luka 3:36) Ile inaonyesha kama Noa alikuwaka. Waandikaji wa Injili, Matayo na Luka, waliandika mambo yenye Yesu alisema kuhusu Noa na Garika.​—Matayo 24:37-39; Luka 17:26, 27.

     Tena, nabii Ezekieli na mutume Paulo walisema kama Noa alikuwa na imani na alikuwa mwenye haki. (Ezekieli 14:14, 20; Waebrania 11:7) Ingewezekana wale waandikaji wazungumuzie mutu fulani mwenye hayakuwaka na kuonyesha kama yeye ni mufano wa kuiga? Kusema kweli, Noa na wanaume na wanamuke wengine wenye imani ni mifano ya kuiga juu ni watu wenye walikuwaka kabisa.​—Waebrania12:1; Yakobo 5:17.

  •   Biblia inatoa habari mbalimbali kuhusu Garika. Habari ya Biblia kuhusu Garika haianze na maneno “Kulikuwaka,” sawa vile hadisi fulani zinaanzaka. Lakini, Biblia inaonyesha mwaka, mwezi, na siku yenye matukio yenye inapatana na Garika ilitokeaka. (Mwanzo 7:11; 8:4, 13, 14) Inazungumuzia pia vipimo vya safina yenye Noa alijenga. (Mwanzo 6:15) Zile habari zote zinaonyesha kama Biblia inazungumuzia Garika kuwa jambo ya kweli, na hapana jambo ya kuwazia-wazia tu.

 Juu ya nini Garika ilitokeaka?

 Sawa vile Biblia inaonyesha, mbele Garika itokee “uovu wa mwanadamu ulikuwa mwingi.” (Mwanzo 6:5) Inaongezea kama “dunia ilikuwa imeharibika mbele ya macho ya Mungu wa kweli” juu ilikuwa nayala jeuri na uasherati.​—Mwanzo 6:11; Yuda 6, 7.

 Biblia inasema kama mingi kati ya ile matendo ya mubaya ilifanywa na malaika waovu wenye walitoka mbinguni na kuya hapa ku dunia ili kufanya ngono na wanamuke. Wale malaika walizala watoto wenye waliitwa Wanefili, wenye waliumiza na kutesa sana watu wenye walikuwa naishi ile wakati. (Mwanzo 6:1, 2, 4) Mungu aliamua kuharibu waovu wenye kuwa ku dunia na kuruhusu watu wazuri waanze tena kuishi bila kuchochewa na wale watu wabaya.​—Mwanzo 6:6, 7, 17.

 Watu walijua kama Garika ingetokea?

 Ndiyo. Mungu alimuambia Noa mambo yenye ingetokea na alimuagiza ajenge safina ili kulinda familia yake na wanyama. (Mwanzo 6:13, 14; 7:1-4) Noa aliambia watu juu ya uharibifu wenye ungekuya, lakini watu walikatala kumusikiliza. (2 Petro 2:5) Biblia inasema: “Hawakuhangaika mupaka Garika ikakuja na kuwaharibu wote.”​—Matayo 24:37-39.

 Safina ya Noa ilikuwa namna gani?

 Safina ilikuwa sanduku kubwa, yenye kuwa na urefu wa metre 133 hivi, upana wa metre 22 hivi, na urefu wa metre 13 hivi. * Safina ilijengwa na mbao za miti yenye utomvu, na ilifunikwa inje na ndani na kabulimbo. Ilikuwa na gorofa tatu na vyumba mbalimbali. Ilikuwa na mulango na inaonekana kulikuwa pia dirisha kwenye sehemu ya juu ya safina. Inawezekana safina ilikuwa na sehemu ya juu yenye kuchongoka katikati ili kusaidia maji ishuke kwa vyepesi.​—Mwanzo 6:14-16.

 Noa alijenga safina mu siku ngapi?

 Biblia haionyeshe kama ilimukamata Noa siku ngapi juu ajenge safina, lakini inaonekana kuwa alipitisha miaka mingi juu ya kuijenga. Noa alikuwa na zaidi ya miaka 500 wakati alizala mutoto wake wa kwanza mwanaume, na wakati Garika ilitokea, alikuwa na miaka 600. *​—Mwanzo 5:32; 7:6.

 Wakati Mungu aliambia Noa ajenge safina, watoto wanaume wa Noa walikuwa tayari walishakomala na kuoa, na inawezekana ilikamata miaka 50 ao 60 hivi. (Mwanzo 6:14, 18) Kama ni vile, tunaweza kusema kama kazi ya kujenga safina ilikamata miaka 40 ao 50.

^ Biblia inaonyesha vipimo ya safina kwa kutumia mikono.“Mukono wa Waebrania ulikuwa santimetre 44.45.”​—The Illustrated Bible Dictionary, Toleo Yenye Kurekebishwa, Sehemu ya 3, ukurasa wa 1635.

^ Kuhusu miaka ya watu sawa vile Noa, ona habari yenye kichwa “Je, Kweli Watu wa Nyakati za Biblia Waliishi kwa Muda Mrefu Sana?” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 12, 2010.