Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 12

Kuzungumza kwa Hisia

Kuzungumza kwa Hisia

1 Wathesalonike 2:7, 8

MUHTASARI: Zungumza na wasikilizaji kwa njia inayoonyesha unawapenda na unataka kuwasaidia.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Wafikirie wasikilizaji wako. Unapojitayarisha, jaribu kuwazia jinsi wasikilizaji wako wanavyohisi na matatizo wanayokabili. Unapofanya hivyo, utazungumza kwa hisia.

  • Chagua maneno yako kwa uangalifu. Tafuta maneno ya kuwaburudisha, kuwafariji, na kuwaimarisha wasikilizaji wako. Epuka kutumia maneno yatakayowaudhi wasikilizaji bila sababu ya msingi, na usizungumze vibaya kuwahusu watu wasiomwabudu Yehova au kuhusu mambo wanayoamini.

  • Onyesha upendezi. Kwa sauti ya fadhili na ishara zinazofaa za mwili, waonyeshe wasikilizaji wako kwamba unawapenda. Hakikisha kwamba uso wako unaonyesha hivyo pia. Jaribu kutabasamu mara nyingi.