Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha

Chapisho hili limekusudiwa kukusaidia uboreshe ustadi wako wa kusoma mbele ya watu na kuboresha ufundi wako wa kusema na kufundisha.

Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Tunafundisha ujumbe muhimu zaidi ambao wanadamu wamewahi kupewa.

SOMO LA 1

Utangulizi Wenye Matokeo

Utangulizi wenye matokeo hutimiza mambo mawili.

SOMO LA 2

Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi

Kutoa hotuba kwa njia ya maongezi huwafanya wasikilizaji wako wastarehe na kuwafanya wawe tayari kukubali ujumbe wako.

SOMO LA 3

Kutumia Maswali

Uliza maswali kwa busara ili kuchochea upendezi na kukazia mambo muhimu.

SOMO LA 4

Kutoa Utangulizi Mzuri wa Maandiko

Chunguza jinsi ya kutayarisha akili za wasikilizaji wako kabla ya kusoma andiko.

SOMO LA 5

Kusoma kwa Usahihi

Kusoma kwa usahihi ni sehemu muhimu ya kuwasilisha ujuzi kumhusu Yehova.

SOMO LA 6

Kuonyesha Waziwazi Matumizi ya Andiko

Hakikisha wasikilizaji wako wanaona waziwazi uhusiano kati ya andiko ulilosoma na jambo unalokazia.

SOMO LA 7

Kusema Mambo Sahihi na Yenye Kusadikisha

Mambo sahihi na yenye kusadikisha ni muhimu ili kuwasaidia wasikilizaji wako kufikia mkataa unaofaa.

SOMO LA 8

Mifano Inayofundisha

Boresha ufundishaji wako kwa kutumia mifano rahisi inayowavutia wasikilizaji wako na kufundisha mambo muhimu.

SOMO LA 9

Kutumia Picha na Video Vizuri

Tumia picha na video kuwasaidia wasikilizaji kukumbuka mambo makuu.

SOMO LA 10

Ubadilifu wa Sauti

Badili mwendo, kiasi, na nguvu ya sauti ili kuchochea hisia za wasikilizaji wako na kuwachochea kutenda.

SOMO LA 11

Shauku

Shauku huonyesha hisia zako kuhusu jambo unalosema na husaidia kuwafanya wasikilizaji wako waendelee kupendezwa na habari unayowaambia.

SOMO LA 12

Kuzungumza kwa Hisia

Ukizungumza kwa hisia, utaonyesha kwamba unawajali wasikilizaji wako.

SOMO LA 13

Kuonyesha Wasikilizaji Manufaa ya Habari Unayozungumzia

Wasaidie wasikilizaji wako waone jinsi mambo wanayojifunza yanavyohusu maisha yao, na uwaonyeshe jinsi wanavyoweza kuyatumia.

SOMO LA 14

Kukazia Mambo Makuu

Wasaidie wasikilizaji wafuatane na hotuba yako, na uweke wazi jinsi kila jambo kuu linavyohusiana na kichwa kikuu na jambo unalotaka kufundisha.

SOMO LA 15

Kuzungumza kwa Usadikisho

Zungumza kwa usadikisho. Onyesha kwa uthabiti kwamba unaamini yale unayosema ni muhimu.

SOMO LA 16

Uwe Mwenye Kujenga na Mwenye Kutia Moyo

Uwe mwenye kujenga badala ya kuwachambua wengine. Kazia uangalifu kweli za Neno la Mungu zenye kuburudisha.

SOMO LA 17

Habari Inayoeleweka

Wasaidie wasikilizaji wako wapate maana ya ujumbe wako. Wasilisha mambo makuu waziwazi.

SOMO LA 18

Kuwaelimisha Wasikilizaji

Chochea kufikiri kwa wasikilizaji wako. Wasaidie wajifunze jambo fulani lenye manufaa.

SOMO LA 19

Kujitahidi Kugusa Moyo

Wachochee wasikilizaji wampende Mungu na Neno lake, Biblia.

SOMO LA 20

Umalizio Wenye Matokeo

Umalizio wenye matokeo utawachochea wasikilizaji wako kukubali na kutumia mambo wanayojifunza.

Andika Maendeleo Yako

Andika maendeleo yako kadiri Unavyojitahidi kuborehsa ustadi wako wa kusoma na kufundisha.

Huenda Ukapenda Pia

MFULULIZO WA VIDEO

Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha​—Video

Sitawisha ustadi muhimu wa kusoma na kufundisha mbele ya watu.