Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Maremagnum/Corbis Documentary via Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Je, Har-Magedoni Itaanzia Nchini Israel?​—Biblia Inasema Nini?

Je, Har-Magedoni Itaanzia Nchini Israel?​—Biblia Inasema Nini?

 Biblia haisemi kwamba Har-Magedoni ni vita ambavyo vitapiganwa katika eneo fulani dogo la dunia, bali ni vita vya serikali zote za wanadamu dhidi ya Mungu ambavyo vitahusisha ulimwengu wote.

  •   Yakawakusanya pamoja mahali panapoitwa katika Kiebrania Har-Magedoni.”​—Ufunuo 16:14, 16.

 Neno “Har-Magedoni” linatokana na neno la Kiebrania Har Meghid·dohnʹ, linalomaanisha “Mlima wa Megido.” Megido lilikuwa jiji katika eneo la Israeli la kale. Kwa sababu hiyo, watu fulani wanaamini kwamba Har-Magedoni itapiganwa nchini Israel. Hata hivyo, eneo la Megido si kubwa vya kutosha wala hakuna eneo lolote katika Mashariki ya Kati ambalo linaweza kuwatosha “wafalme wa dunia nzima inayokaliwa” pamoja na majeshi yao.

 Kitabu cha Ufunuo kiliandikwa kwa kutumia “ishara,” au lugha ya mfano. (Ufunuo 1:1) Har-Magedoni inarejelea, si eneo halisi, bali hali ya mataifa ulimwenguni pote kujaribu kwa mara ya mwisho kupinga utawala wa Mungu.​—Ufunuo 19:11-16, 19-21.