Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Majibu Ya Maswali Ya Biblia

Majibu Ya Maswali Ya Biblia

Ni nini kinachowachochea watu wengi wachunguze kuwepo kwa Muumba?

Uhai ni muujiza!

Miaka 3,000 hivi iliyopita, mshairi mmoja aliandika hivi: “Nimeumbwa kwa njia ya ajabu yenye kuogopesha.” (Zaburi 139:14) Unapofikiria jinsi chembe moja ndogo inavyokua na kuwa mtoto, je, jambo hilo halikushangazi? Watu wengi wanakubali kwamba vitu vilivyo hai viliumbwa na Mungu.—Soma Zaburi 139:13-17; Waebrania 3:4.

Muumba wa ulimwengu na dunia ndiye mwanzilishi wa uhai. (Zaburi 36:9) Amewasiliana na wanadamu na hata amejitambulisha kwao.—Soma Isaya 45:18.

Je, wanadamu wametokana na wanyama?

Ni kweli kwamba wanadamu na wanyama wanafanana kwa njia fulani. Lakini hali iko hivyo kwa sababu wanadamu na pia wanyama waliumbwa na Mungu waishi duniani. Mwanadamu wa kwanza aliumbwa kutokana na mavumbi na si kutokana na mnyama.—Soma Mwanzo 1:24; 2:7.

Wanadamu wanatofautiana na wanyama katika njia mbili kuu. Kwanza, wanadamu wana uwezo wa kumjua, kumpenda, na kumheshimu Mungu. Pili, tofauti na wanadamu, wanyama hawakuumbwa waishi milele. Lakini sasa, wanadamu wanakufa kwa sababu Adamu alikataa kutii mwongozo wa Muumba.—Soma Mwanzo 1:27; 2:15-17.