Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Ufalme Wako Uje”—​Sala Ambayo Mamilioni ya Watu Husali

“Ufalme Wako Uje”—​Sala Ambayo Mamilioni ya Watu Husali

Je, umewahi kuomba Ufalme wa Mungu uje? Kwa miaka mingi, mamilioni ya watu wamekuwa wakiomba “Ufalme Wako Uje,” maneno ambayo ni sehemu ya ile inayojulikana kama sala ya Baba Yetu. Kwa nini watu hurudia maneno hayo mara kwa mara? Kwa sababu Yesu aliwaambia wafuasi wake wasali kuhusu Ufalme wa Mungu.

Mwanzoni, wafuasi wa Yesu hawakuelewa mambo yote ambayo Yesu alizungumza kuhusu Ufalme. Wakati fulani walimuuliza hivi: “Bwana, je, unaurudisha ufalme kwa Israeli wakati huu?” Inawezekana walishangaa kwa sababu Yesu hakuwaambia wakati hususa ambao Ufalme wa Mungu utakuja. (Matendo 1:6, 7) Je, hilo linamaanisha kwamba hatuwezi kujua Ufalme wa Mungu ni nini na utakuja lini? La hasha!

Toleo hili la Mnara wa Mlinzi litakusaidia kupata majibu ya maswali yafuatayo:

  • Kwa nini tunahitaji Ufalme wa Mungu?

  • Mfalme wa Ufalme wa Mungu ni nani?

  • Ufalme wa Mungu utaanza kutawala dunia lini?

  • Ufalme wa Mungu utatimiza nini?

  • Kwa nini tunapaswa kuunga mkono Ufalme wa Mungu sasa?

  • Ufalme wa Mungu ni nini?