Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MAISHA YA MKRISTO

Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Wasaidie Wanafunzi wa Biblia Wajiweke Wakfu na Kubatizwa

Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Wasaidie Wanafunzi wa Biblia Wajiweke Wakfu na Kubatizwa

KWA NINI NI MUHIMU: Ili kupata kibali cha Yehova, ni lazima wanafunzi wa Biblia wajiweke wakfu na kubatizwa. (1Pe 3:21) Kisha wale wanaoishi kupatana na wakfu wao watapata ulinzi wa kiroho. (Zb 91:1, 2) Mkristo anajiweka wakfu kwa Yehova—si kwa mwanadamu, kazi, au tengenezo. Hivyo basi, wanafunzi wanahitaji kusitawisha uthamini na upendo wao kwa Mungu.Ro 14:7, 8.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Mnapojifunza, mwonyeshe habari hiyo inafunua nini kumhusu Yehova. Kazia umuhimu wa kusoma Biblia kila siku na kusali kwa Yehova “bila kuacha.”1Th 5:17; Yak 4:8

  • Mtie moyo mwanafunzi wako awe na mradi wa kujiweka wakfu na kubatizwa. Anapojitahidi kufikia mradi huo, msaidie afikie miradi mingine, kama vile kutoa maelezo katika mikutano au kuwahubiria majirani na wafanyakazi wenzake. Kumbuka kwamba Yehova hamlazimishi yeyote amtumikie. Kujiweka wakfu ni uamuzi wa mtu binafsi.Kum 30:19, 20

  • Mtie moyo mwanafunzi wako afanye mabadiliko yanayohitajika ili ampendeze Yehova na kustahili kubatizwa. (Met 27:11) Kwa sababu tabia na mazoea fulani huwa yamekita mizizi, huenda mwanafunzi wa Biblia akaendelea kuhitaji msaada kuvua utu wa zamani na kuvaa utu mpya. (Efe 4:22-24) Mwonyeshe makala za mfululizo zenye kichwa “Biblia Inabadili Maisha” kwenye Mnara wa Mlinzi

  • Mweleze kuhusu shangwe ambayo wewe umepata kwa kumtumikia Yehova.—Isa 48:17, 18