Barua ya Kwanza kwa Wathesalonike 5:1-28

5  Sasa akina ndugu, hamhitaji kuandikiwa chochote kuhusu nyakati na majira.  Kwa maana ninyi wenyewe mnajua vema kwamba siku ya Yehova*+ inakuja kama vile mwizi anavyokuja usiku.+  Wakati watakapokuwa wakisema: “Amani na usalama!” ndipo uharibifu wa ghafla utakapowapata mara moja,+ kama vile maumivu ya kuzaa ya mwanamke mwenye mimba, nao hawataponyoka kamwe.  Lakini ninyi, akina ndugu, hamko gizani, hivi kwamba siku hiyo iwafikie ghafla kama vile ingewafikia wezi,  kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana.+ Sisi si wa usiku wala wa giza.+  Basi, tusiendelee kulala usingizi kama wengine wanavyofanya,+ bali tukae macho+ na kutunza akili zetu.+  Kwa maana wale wanaolala usingizi hulala usiku, na wale wanaolewa, hulewa usiku.+  Lakini sisi tulio wa mchana, na tutunze akili zetu na kuvaa bamba la kifuani la imani na upendo na tumaini la wokovu kama kofia ya chuma+  kwa sababu Mungu hakutuchagua ili tupatwe na hasira, bali tupate wokovu+ kupitia Bwana wetu Yesu Kristo. 10  Alikufa kwa ajili yetu,+ ili kama tuko macho au tumelala usingizi,* tuishi pamoja naye.+ 11  Kwa hiyo endeleeni kutiana moyo* na kujengana,+ kama vile kwa kweli mnavyofanya. 12  Sasa tunawaomba, akina ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu na wanaowasimamia katika Bwana na kuwaonya ninyi; 13  na mwafikirie kwa njia inayozidi ile ya kawaida katika upendo kwa sababu ya kazi yao.+ Dumisheni amani miongoni mwenu.+ 14  Kwa upande mwingine, tunawahimiza akina ndugu, waonyeni* wale wasiofuata utaratibu,+ wafarijini wale walioshuka moyo,* wasaidieni walio dhaifu, iweni na subira kwa watu wote.+ 15  Hakikisheni hakuna yeyote anayelipa ubaya kwa ubaya,+ bali sikuzote mwendelee kutendeana mema kati yenu na kwa wengine wote.+ 16  Shangilieni sikuzote.+ 17  Salini bila kuacha.+ 18  Toeni shukrani kuhusu kila jambo.+ Hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu. 19  Msiuzime moto wa roho.+ 20  Msitendee unabii kwa dharau.+ 21  Hakikisheni mambo yote;+ shikamaneni na yaliyo mema. 22  Epukeni kila aina ya uovu.+ 23  Mungu wa amani na awatakase kikamili. Na bila kasoro yoyote, roho na nafsi* na mwili wenu akina ndugu, na vihifadhiwe bila lawama wakati wa kuwapo kwa Bwana wetu Yesu Kristo.+ 24  Yule anayewaita ninyi ni mwaminifu, na kwa hakika atafanya hivyo. 25  Akina ndugu, endeleeni kusali kwa ajili yetu.+ 26  Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu. 27  Ninawaweka chini ya wajibu mzito kwa Bwana mhakikishe kwamba ndugu wote wanasomewa barua hii.+ 28  Fadhili zisizostahiliwa za Bwana wetu Yesu Kristo ziwe pamoja nanyi.

Maelezo ya Chini

Au “tumelala usingizi katika kifo.”
Au “kufarijiana.”
Au “mwakaripie.”
Au “wale waliovunjika moyo.” Tnn., “wale walio na nafsi ndogo.”
Au “uhai.” Angalia Kamusi.