Barua ya Kwanza kwa Wathesalonike 5:1-28
5 Sasa akina ndugu, hamhitaji kuandikiwa chochote kuhusu nyakati na majira.
2 Kwa maana ninyi wenyewe mnajua vema kwamba siku ya Yehova*+ inakuja kama vile mwizi anavyokuja usiku.+
3 Wakati watakapokuwa wakisema: “Amani na usalama!” ndipo uharibifu wa ghafla utakapowapata mara moja,+ kama vile maumivu ya kuzaa ya mwanamke mwenye mimba, nao hawataponyoka kamwe.
4 Lakini ninyi, akina ndugu, hamko gizani, hivi kwamba siku hiyo iwafikie ghafla kama vile ingewafikia wezi,
5 kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana.+ Sisi si wa usiku wala wa giza.+
6 Basi, tusiendelee kulala usingizi kama wengine wanavyofanya,+ bali tukae macho+ na kutunza akili zetu.+
7 Kwa maana wale wanaolala usingizi hulala usiku, na wale wanaolewa, hulewa usiku.+
8 Lakini sisi tulio wa mchana, na tutunze akili zetu na kuvaa bamba la kifuani la imani na upendo na tumaini la wokovu kama kofia ya chuma+
9 kwa sababu Mungu hakutuchagua ili tupatwe na hasira, bali tupate wokovu+ kupitia Bwana wetu Yesu Kristo.
10 Alikufa kwa ajili yetu,+ ili kama tuko macho au tumelala usingizi,* tuishi pamoja naye.+
11 Kwa hiyo endeleeni kutiana moyo* na kujengana,+ kama vile kwa kweli mnavyofanya.
12 Sasa tunawaomba, akina ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu na wanaowasimamia katika Bwana na kuwaonya ninyi;
13 na mwafikirie kwa njia inayozidi ile ya kawaida katika upendo kwa sababu ya kazi yao.+ Dumisheni amani miongoni mwenu.+
14 Kwa upande mwingine, tunawahimiza akina ndugu, waonyeni* wale wasiofuata utaratibu,+ wafarijini wale walioshuka moyo,* wasaidieni walio dhaifu, iweni na subira kwa watu wote.+
15 Hakikisheni hakuna yeyote anayelipa ubaya kwa ubaya,+ bali sikuzote mwendelee kutendeana mema kati yenu na kwa wengine wote.+
16 Shangilieni sikuzote.+
17 Salini bila kuacha.+
18 Toeni shukrani kuhusu kila jambo.+ Hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.
19 Msiuzime moto wa roho.+
20 Msitendee unabii kwa dharau.+
21 Hakikisheni mambo yote;+ shikamaneni na yaliyo mema.
22 Epukeni kila aina ya uovu.+
23 Mungu wa amani na awatakase kikamili. Na bila kasoro yoyote, roho na nafsi* na mwili wenu akina ndugu, na vihifadhiwe bila lawama wakati wa kuwapo kwa Bwana wetu Yesu Kristo.+
24 Yule anayewaita ninyi ni mwaminifu, na kwa hakika atafanya hivyo.
25 Akina ndugu, endeleeni kusali kwa ajili yetu.+
26 Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
27 Ninawaweka chini ya wajibu mzito kwa Bwana mhakikishe kwamba ndugu wote wanasomewa barua hii.+
28 Fadhili zisizostahiliwa za Bwana wetu Yesu Kristo ziwe pamoja nanyi.
Maelezo ya Chini
^ Angalia Nyongeza A5.
^ Au “tumelala usingizi katika kifo.”
^ Au “kufarijiana.”
^ Au “mwakaripie.”
^ Au “wale waliovunjika moyo.” Tnn., “wale walio na nafsi ndogo.”