Hamia kwenye habari

Ndugu na dada ulimwenguni pote walikusanyika kuadhimisha Ukumbusho

APRILI 21, 2022
HABARI ZA ULIMWENGUNI POTE

Mamilioni Waungana Kuadhimisha Ukumbusho wa Kifo cha Kristo

Mamilioni Waungana Kuadhimisha Ukumbusho wa Kifo cha Kristo

Akina ndugu wakisalimiana nchini Chile

Aprili 15, 2022, mamilioni ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote na wale walioalikwa walikumbuka Mlo wa Jioni wa Bwana. Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kuadhimisha Ukumbusho pamoja katika Jumba la Ufalme tangu mwaka wa 2019. Wale ambao hawakufaulu kuhudhuria kwenye Jumba la Ufalme waliunganishwa kwa njia ya mtandao.

Ukumbusho wa kifo cha Kristo ni tukio muhimu sana ambalo Mashahidi wa Yehova hufanya kila mwaka. Kwa sababu ya ugonjwa wa COVID-19, tukio hili la kila mwaka lilifanywa kupitia video mtandaoni kwa miaka miwili mfululizo. Zaidi ya watu milioni 21 walihudhuria Ukumbusho wa mwaka wa 2021.

Kwa baadhi ya watu, kama vile Markensia Remy nchini Haiti, ilikuwa mara yake ya kwanza kuhudhuria Ukumbusho katika Jumba la Ufalme. Markensia ambaye alibatizwa mwaka mmoja uliopita anasema hivi: “Nina furaha sana kwa kuwa nimehudhuria Ukumbusho katika Jumba la Ufalme. Hata siwezi kuelezea furaha yangu. Ninahisi kwamba mimi ni sehemu ya familia ya pekee.”

Tunamshukuru sana Yehova kwa baraka zake katika mwadhimisho wa Ukumbusho wa mwaka huu, na hasa tunamshukuru sana Yehova na Mwana wake, Yesu Kristo, kwa wonyesho mkubwa zaidi wa upendo ambao tumewahi kuonyeshwa.​—Yohana 3:16.

 

Argentina

Bolivia

Brazili

Kambodia

Jamhuri ya Afrika ya Kati

Visiwa vya Cook (Rarotonga)

Ekuado

Indonesia

Israel

Japani

Kazakhstan

Kosovo

Mexico

Paraguai

Peru

Filipino

Poland

Rumania

Hispania

Taiwan

Ukrainia

Marekani

Venezuela