Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 40

Endelea Kuwa na Mambo Mingi ya Kufanya Katika Sehemu ya Mwisho ya “Siku za Mwisho”

Endelea Kuwa na Mambo Mingi ya Kufanya Katika Sehemu ya Mwisho ya “Siku za Mwisho”

“Mukuwe imara, bila kutikisika, sikuzote mukiwa na mambo mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.”​—1 KO. 15:58.

WIMBO 58 Kutafuta Marafiki wa Amani

KIFUPI CHA HABARI *

1. Ni nini inatuhakikishia kama tunaishi mu “siku za mwisho”?

ULIZALIWA kisha mwaka wa 1914? Kama ni vile, umeishi maisha yako yote mu “siku za mwisho” za mupangilio huu wa mambo. (2 Ti. 3:1) Sisi wote tumesikia juu ya matukio yenye Yesu alitabiri kama itatokea wakati wetu. Ile matukio inatia ndani vita, upungufu wa chakula, matetemeko ya inchi, magonjwa ya kuambukiza, kuongezeka kwa uovu, na kuteswa kwa watu wa Yehova. (Mt. 24:3, 7-9, 12; Lu. 21:10-12) Pia, tumeona kama watu wamekuwa na tabia zenye mutume Paulo alitabiri. (Ona kisanduku “ Tabia za Watu Leo.”) Sisi watumishi wa Yehova, tuko hakika kama tunaishi mu “kipindi cha mwisho cha zile siku.”​—Mik. 4:1.

2. Inaomba tupate majibu ya maulizo gani?

2 Kwa sababu wakati murefu umepita tangu mwaka wa 1914, inaonekana wazi kama tunaishi mu sehemu ya mwisho ya “siku za mwisho.” Juu mwisho uko karibu sana, inaomba tupate majibu ya maulizo fulani ya maana yenye kufuata: Ni matukio gani yenye itatokea ku mwisho wa “siku za mwisho”? Na Yehova anatuomba tufanye nini wakati tunangojea ile matukio?

NI MAMBO GANI ITATOKEA KU MWISHO WA “SIKU ZA MWISHO”?

3. Kulingana na unabii wenye kuwa mu 1 Watesalonike 5:1-3, viongozi wa ulimwengu watafanya tangazo gani?

3 Soma 1 Watesalonike 5:1-3. Paulo anazungumuzia “siku ya Yehova.” Mu andiko hili, siku ya Yehova ni kipindi cha wakati chenye kitaanza wakati “Babiloni Mukubwa,” ni kusema, dini zote za uongo zitashambuliwa, na chenye kitaisha ku Armagedoni. (Ufu. 16:14, 16; 17:5) Mbele tu ile “siku” ianze, viongozi wa ulimwengu watatangaza “amani na usalama!” Wakati fulani, viongozi wa ulimwengu wanatumia maneno kama ile wakati wanazungumuza juu ya kufanya uhusiano kati ya mataifa ukuwe muzuri zaidi. * Lakini, tangazo la “amani na usalama” lenye Biblia inasema litakuwa tofauti. Juu ya nini? Wakati watatangaza vile, watu wengi watawaza kama viongozi wa ulimwengu wameweza kufanya ulimwengu ukuwe nafasi ya usalama kabisa. Lakini, kwa kweli “taabu kubwa” itaanza na kisha kutakuwa “uharibifu wa kushitukia.”​—Mt. 24:21.

Usidanganywe na tangazo la uongo la “amani na usalama” la viongozi wa ulimwengu (Picha hii inapatana na fungu la 3-6) *

4. (a) Ni mambo gani yenye hatujue juu ya tangazo la “amani na usalama”? (b) Ni mambo gani yenye tunajua tayari juu ya tangazo hilo?

4 Tunajua mambo fulani juu ya tangazo la “amani na usalama.” Lakini, kuko mambo ingine yenye hatujue. Hatujue ni nini itachochea viongozi wa ulimwengu wafanye tangazo hilo na hatujue litafanywa namna gani. Na hatujue kama itakuwa tangazo moja tu ao matangazo mingi yenye kufuatana. Kama itakuwa matangazo mingi ao tangazo moja tu, tunajua jambo hili: hatupaswe kudanganywa kwa kuwaza kama viongozi wa ulimwengu wanaweza kabisa kuleta amani mu dunia. Lakini, hilo njo tangazo lenye Biblia inatuambia tungojee. Ile njo alama yenye itaonyesha kama “siku ya Yehova” inataka kuanza!

5. Andiko la 1 Watesalonike 5:4-6 linatuambia tufanye mambo gani ili tukuwe tayari kwa ajili ya “siku ya Yehova”?

5 Soma 1 Watesalonike 5:4-6. Shauri la Paulo linatuonyesha mambo yenye tunapaswa kufanya ili tukuwe tayari kwa ajili ya “siku ya Yehova.” Hatupaswe “kulala usingizi kama wengine.” Tunapaswa ‘kukaa macho’ na kuendelea kukesha. Kwa mufano, tunapaswa kuwa waangalifu ili tusiunge mukono upande fulani kwa kujiingiza mu mambo ya politike ya ulimwengu huu. Kama tunajiingiza mu mambo ya politike, tunaweza kuwa “sehemu ya ulimwengu.” (Yoh. 15:19) Tunajua kama ni Ufalme wa Mungu tu njo utaleta amani katika ulimwengu.

6. Tunapenda kusaidia wengine wafanye nini, na juu ya nini?

6 Zaidi ya kukaa macho, tunapenda pia kusaidia wengine wajue mambo yenye Biblia ilitabiri kama itatokea mu dunia. Tukumbuke kama wakati tu taabu kubwa itaanza, haitawezekana tena watu waanze kumutumikia Yehova. Njo maana kazi yetu ya kuhubiri inapaswa kufanywa haraka sana! *

ENDELEA KUWA NA MAMBO MINGI YA KUFANYA KATIKA KAZI YA KUHUBIRI

Leo wakati tunahubiria watu, tunawaonyesha kama Ufalme wa Mungu tu njo unaweza kufanya dunia ikuwe na usalama wa kweli (Picha hii inapatana na fungu la 7-9)

7. Yehova anatuomba tufanye nini leo?

7 Katika wakati kidogo wenye unabakia mbele “siku” yake ianze, Yehova anatuomba tukuwe na mambo mingi ya kufanya katika kazi ya kuhubiri. Tunapaswa kuhakikisha kama ‘tuko na mambo mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.’ (1 Ko. 15:58) Yesu alitabiri mambo yenye tunapaswa kufanya. Wakati alizungumuzia matukio yote makubwa yenye ingetokea mu siku za mwisho, aliongeza hivi: “Tena, katika mataifa yote, lazima habari njema ihubiriwe kwanza.” (Mk. 13:4, 8, 10; Mt. 24:14) Waza kidogo: Kila wakati unaenda ku mahubiri, unasaidia kutimiza unabii huo wa Biblia!

8. Ni nini inaonyesha kama kazi ya kuhubiri Ufalme iko inaendelea mbele?

8 Kazi ya kuhubiri Ufalme inaendelea namna gani? Kila mwaka, kazi hiyo iko inaendelea mbele. Kwa mufano, fikiria namna wahubiri wa Ufalme wameongezeka mu dunia yote katika siku hizi za mwisho. Katika mwaka wa 1914, kulikuwa wahubiri 5 155 mu inchi 43. Leo, kuko wahubiri milioni 8 na nusu hivi mu inchi 240! Hata hivyo, kazi yetu haijafikia mwisho. Tunapaswa kuendelea kuhubiria watu kama ni Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza magumu yote ya wanadamu.​—Zb. 145:11-13.

9. Juu ya nini tunapaswa kuendelea kuhubiri ujumbe wa Ufalme?

9 Kazi yetu ya kuhubiri Ufalme itaendelea mupaka wakati Yehova atasema kama inaisha. Watu wanabakia na muda gani ili wajifunze juu ya Yehova Mungu na Yesu Kristo? (Yoh. 17:3) Hatujue. Tunajua kama, mbele taabu kubwa ianze, watu wote wenye kuwa na “muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele” wangali na nafasi ya kukubali habari njema. (Mdo. 13:48) Tunaweza kufanya nini ili kusaidia watu hao mbele ikuwe kuchelewa sana?

10. Yehova anatupatia mambo gani ili tufundishe watu kweli?

10 Kupitia tengenezo lake, Yehova iko anatupatia mambo yote yenye tuko nayo lazima ili kufundisha wengine kweli. Kwa mufano, tunapata mazoezi kila juma ku mukutano wa katikati ya juma. Mukutano huo unatusaidia kujua mambo ya kusema wakati tunatembelea watu kwa mara ya kwanza na wakati tunawarudilia. Mukutano huo unatufundisha pia namna ya kuongoza mafunzo ya Biblia. Tengenezo la Yehova limetupatia pia Vyombo vya Kufundishia. Vyombo hivyo vinatusaidia . . .

  • kuanzisha mazungumuzo,

  • kuchochea watu wapendezwe,

  • kusaidia watu wakuwe na hamu ya kujua mambo mingi zaidi,

  • kufundisha kweli wakati tunaongoza mafunzo ya Biblia, na

  • kutia moyo watu wenye kupendezwa wafungue site yetu ya Enternete ao watembelee Majumba yetu ya Ufalme.

Kwa kweli, haitoshe tu kuwa na vyombo hivyo. Tunapaswa kuvitumia. * Kwa mufano, ikiwa, kisha kuzungumuza muzuri na mutu mwenye kupendezwa, unamuachia trakte ao gazeti, anaweza kusoma zaidi mupaka wakati atamurudilia. Kila mumoja wetu iko na daraka la kufanya mambo mingi mu kazi ya kuhubiri kila mwezi kulingana na uwezo wake.

11. Juu ya nini sehemu Ujifunze Biblia ku Enternete ilianzishwa?

11 Mufano mwingine wenye kuonyesha namna Yehova iko anasaidia watu wajifunze kweli ni sehemu Ujifunze Biblia ku Enternete yenye kuwa ku jw.org®. (Fungua sehemu MAFUNDISHO YA BIBLIA > UJIFUNZE BIBLIA KU ENTERNETE.) Juu ya nini ile sehemu ilianzishwa? Kila mwezi, watu wengi sana mu dunia yote wanafungua Enternete ili kutafuta habari za kuwasaidia kujifunza Biblia. Sehemu Ujifunze Biblia ku Enternete yenye kuwa ku site yetu inaweza kusaidia watu hao wavumbue kweli ya Neno la Mungu. Watu fulani wenye unazungumuza nao wanaweza kusita kukubali funzo la Biblia. Kama ni vile, uwaonyeshe sehemu hiyo ku site yetu ya Enternete ao uwatumie kiunganishi (lien) cha kuwapeleka ku sehemu hiyo. *

12. Mutu anaweza kujua nini wakati anajifunza habari zenye ziko katika sehemu Ujifunze Biblia ku Enternete?

12 Sehemu Ujifunze Biblia ku Enternete iko na habari hizi: “Biblia na Muandikaji Wake,” “Watu Wenye Kuzungumuziwa Sana Katika Biblia,” na “Ujumbe wa Biblia Wenye Unatoa Tumaini.” Wakati mutu anajifunza habari zenye ziko katika sehemu hiyo, atajua:

  • Namna Biblia inaweza kusaidia mutu

  • Yehova, Yesu, na malaika ni nani

  • Juu ya nini Mungu aliumba wanadamu

  • Juu ya nini kuko mateso na mambo ya mubaya

Ile sehemu inazungumuzia pia namna Yehova . . .

  • atamaliza mateso na kifo,

  • atafufua watu wenye wamekufa, na

  • kutosha serikali za wanadamu zenye zimeshindwa na kuweka Ufalme wake pa nafasi ya serikali hizo.

13. Sehemu Ujifunze Biblia ku Enternete inakamata nafasi ya mupango wa funzo la Biblia? Fasiria.

13 Sehemu Ujifunze Biblia ku Enternete haikamate nafasi ya mupango wa funzo la Biblia. Yesu ametupatia pendeleo la kufanya wanafunzi. Tunatumaini kama watu wenye kupendezwa watajifunza habari zenye ziko katika sehemu hiyo, watafurahia mambo yenye watajifunza, na watakuwa na hamu ya kujua mambo mingi zaidi. Kama ni vile, pengine watakubali funzo la Biblia. Ku mwisho wa kila somo, musomaji anatiwa moyo atume ombi ili apate mutu wa kujifunza naye Biblia. Kupitia site yetu ya Enternete, tuko tunapata ombi za kujifunza Biblia zaidi ya 230 kila siku kutoka mu dunia yote! Kujifunza Biblia na mutu moja kwa moja ni jambo la lazima!

ENDELEA KUJIKAZA ILI KUFANYA WANAFUNZI

14. Kulingana na maagizo ya Yesu yenye kuwa mu Matayo 28:19, 20, tunapaswa kujikaza ili kufanya nini, na juu ya nini?

14 Soma Matayo 28:19, 20. Wakati tunaongoza mafunzo ya Biblia, tunapaswa kujikaza sana ili ‘kufanya wanafunzi . . . , na kuwafundisha kushika mambo yote yenye [Yesu] ameamuru.’ Tunapaswa kusaidia watu waelewe kama ni jambo la maana sana wachague kumutumikia Yehova na kuunga mukono Ufalme wake. Maana yake, tunapaswa kuchochea watu watumie mambo yenye wanajifunza katika maisha yao, watoe maisha yao kwa Yehova, na kubatizwa. Kama tu wanafanya vile, wataokoka siku ya Yehova.​—1 Pe. 3:21.

15. Hatupaswe kuendelea kufanya nini, na juu ya nini?

15 Kama vile tumeona, kunabakia wakati kidogo tu mbele mupangilio huu wa mambo uishe. Njo maana, hatupaswe kuendelea kujifunza Biblia na watu wenye hawana kabisa nia ya kuwa wanafunzi wa Kristo. (1 Ko. 9:26) Kazi yetu ni ya haraka! Kuko watu wengi wenye wangali na lazima ya kusikia ujumbe wa Ufalme mbele haijakuwa kuchelewa sana.

ACHANA KABISA NA MAMBO YOTE YENYE KUWA NA UPATANO NA DINI YA UONGO

16. Kulingana na Ufunuo 18:2, 4, 5, 8, tunapaswa kufanya nini? (Ona pia maelezo ya chini.)

16 Soma Ufunuo 18:2, 4, 5, 8. Mistari hii inaonyesha jambo lingine lenye Yehova anaomba waabudu wake wafanye. Wakristo wote wa kweli wanapaswa kuhakikisha kama wameachana na mambo yote yenye kuwa na upatano na Babiloni Mukubwa. Pengine mwanafunzi wa Biblia alikuwa katika dini fulani ya uongo mbele ya kujifunza kweli. Pengine alikuwa anashiriki katika ibada za dini hiyo na katika mambo ya dini. Ao pengine alikuwa anatoa muchango wa feza ili kutegemeza dini hiyo. Mbele mwanafunzi wa Biblia akubaliwe kuwa muhubiri mwenye hajabatizwa, anapaswa kuvunja uhusiano wowote na dini ya uongo. Anapaswa kuandika barua na kuitumia kanisa lake la zamani ili kuwaonyesha kama haiko tena mushiriki wa kanisa hilo ao wa shirika lolote lenye kuwa na upatano na Babiloni Mukubwa. *

17. Mukristo anapaswa kuepuka kazi gani, na juu ya nini?

17 Mukristo wa kweli anapaswa kuhakikisha kama kazi yake ya kimwili haina upatano wowote na Babiloni Mukubwa. (2 Ko. 6:14-17) Kwa mufano, hapaswe kuwa mufanyakazi wa dini fulani. Tena, Mukristo mwenye iko mufanyakazi ku kompanyi fulani hapaswe kukubali kazi ya wakati murefu kwenye jengo lenye linaendelesha ibada ya uongo. Na kama iko na kazi yake mwenyewe, hapaswe kutafuta ao kukubali kazi yenye kuwa na upatano na Babiloni Mukubwa. Juu ya nini tunapaswa kuepuka kabisa kazi hizo? Juu hatupendi kuunga mukono matendo na zambi za dini za uongo zenye haziko safi mbele ya macho ya Mungu.​—Isa. 52:11. *

18. Namna gani ndugu mumoja alishikamana na kanuni za Biblia juu ya kazi ya kimwili?

18 Miaka fulani yenye imepita, fundi fulani wa kazi alimuomba muzee mumoja wa kutaniko mwenye alikuwa na kazi yake mwenyewe atumike kazi ya kidogo ya useremala ku kanisa mu muji kwenye muzee huyo alikuwa anaishi. Fundi huyo wa kazi alijua kama sikuzote ndugu huyo alikuwa anakataa kufanya kazi ku makanisa. Lakini, mara hiyo fundi huyo alikuwa anatafuta sana mutu wa kufanya ile kazi. Hata hivyo, ndugu huyo alishikamana na kanuni za Biblia na akakataa kazi hiyo. Juma lenye lilifuata, gazeti moja katika eneo hilo lilionyesha picha ya seremala fulani mwenye alikuwa anatia musalaba ku kanisa. Kama ndugu yetu hangeshikamana na kanuni za Biblia, ni picha yake njo ingeonyeshwa katika gazeti hilo. Wazia namna jambo hilo lingeumiza sana Wakristo wenzake! Pia, wazia namna Yehova angejisikia.

TUMEJIFUNZA NINI?

19-20. (a) Tumejifunza nini? (b) Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

19 Kulingana na unabii wa Biblia, tukio kubwa lenye litatokea mu dunia hivi karibuni ni tangazo la “amani na usalama” lenye viongozi wa ulimwengu watafanya. Mambo yenye Yehova ametufundisha inatusaidia kujua kama viongozi wa ulimwengu hawataleta amani ya kweli na yenye kudumu. Tunapaswa kufanya nini mbele tukio hilo lifike na mbele ya uharibifu wa kushitukia wenye utafuata? Yehova anatuomba tuendelee kufanya mambo mingi katika kazi ya kuhubiri ujumbe wa Ufalme na kujikaza kufanya wanafunzi wengi zaidi. Wakati uleule, tunapaswa kujitenga na dini zote za uongo. Hilo linamaanisha pia kama tunapaswa kutoka mu Babiloni Mukubwa na kukataa kazi zenye kuwa na uhusiano naye.

20 Kuko matukio ingine yenye itatokea katika sehemu ya mwisho ya “siku za mwisho.” Na kuko mambo ingine yenye Yehova anatuomba tufanye. Ni mambo gani, na namna gani tunaweza kujitayarisha juu ya mambo yote yenye itatokea hivi karibuni? Tutazungumuzia jambo hilo katika habari yenye kufuata.

WIMBO 71 Sisi Ni Jeshi la Yehova!

^ fu. 5 Hivi karibuni, tutasikia tangazo la viongozi wa ulimwengu la kusema kama wameleta “amani na usalama!” Ile njo itakuwa alama ya kuonyesha kama taabu kubwa inataka kuanza. Yehova anatuomba tufanye nini kuanzia leo mupaka wakati huo? Habari hii itatusaidia kupata jibu.

^ fu. 3 Kwa mufano, ku site ya Enternete ya Umoja wa Mataifa, shirika hilo linasema kama “linaendelesha amani na usalama kati ya mataifa.”

^ fu. 10 Ili kupata habari zaidi juu ya namna ya kutumia Vyombo vyetu vya Kufundishia, ona habari “Tufundishe Kweli” katika Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 10, 2018.

^ fu. 11 Kwa sasa, ile sehemu inapatikana mu luga ya Kiingereza na ya Kireno (Portugais); itapatikana mu luga zingine siku zenye kuja.

^ fu. 16 Tunapaswa pia kuepuka mashirika fulani, kama vile kambi za vijana ao majengo yenye kuwa na upatano na dini ya uongo kwenye watu wanafanyia mambo ya kujifurahisha. Kwa mufano, juu ya kujiunga na shirika la Kikristo la vijana wanaume (YMCA), ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 4, 1979 (katika Kifaransa). Tunapaswa pia kuepuka kujiunga na shirika la Kikristo la vijana wanamuke (YWCA). Hata kama ile mashirika ya vijana ya eneo lenu inaweza kusema kama mambo yao haina upatano wowote na dini, kwa kweli, ile mashirika inaendelesha mawazo na miradi ya kidini.

^ fu. 17 Ili kupata habari zaidi juu ya mawazo ya Maandiko kuhusu kazi zenye ziko na upatano na dini, ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 4, 1999.

^ fu. 83 MAFASIRIO YA PICHA: Watu wenye wanakuja kunywa kahawa mu restora wanashangaa wakati wanasikia habari ku televizyo juu ya tangazo la “amani na usalama.” Ndugu mumoja na bibi yake, wenye wako wanapumuzika kisha mahubiri, hawadanganywe na habari hiyo.